Hatima ya Askari hawa ni nini?

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,754
Heshima mbele wakuu..Kufuatia Askari watatu waliokuwa miongoni mwa watuhumiwa katika kesi inayomhusu ACP Abdallah Zombe na wenzake kuachiwa huru na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Salum Masati(baada ya kutokutwa na hatia)...Kinachonitatiza mimi ni je,ni nini hasa hatma ya Askari hawa CPL.Nyngerela Morris,PC.Noel Leonard na PC.Felix Sandeys???,wanaweza kurudishwa kazini???(sheria inasemaje kuhusu hili,mimi sijui hapa jamani),vipi kuhusu mafao yao na mishahara yao kwa kipindi chote walichokuwa mahabusu????...Na mwisho je,wanaweza kufungua kesi ya madai kutaka walipwe fidia kwa kipindi chote walichokaa mahabusu wakituhumiwa kwa makosa ambayo Mahakama Kuu imethibitsha kwamba hawakuyafanya????...Naomba msaada katika haya wakuu....Be blessed
 
Tunaomba wanasheria humu au wale ambao wanajua sheria watusaidie hapa. Sidhani kama watakuwa wamefukuazwa kazi maana walikuwa ni watuhumiwa, they were still innocent until proved otherwise. Sielewi kama familia zao zilikuwa zinapokea mishahara yao. Ila nakumbuka kumsikia mke mdogo wa Zombe akisema ametoka kupokea fedha ya uniform ya mumewe, December 2008. Hivyo, naamini bado wote walikuwa ni watumishi wa Jeshi la Police hadi kesi itakapohukumu. Kwa mawazo yangu nafikiri walioachiwa huru wana haki ya kurudishwa kazini. Wakitaka kuandika madai sijui yatakuwa ya nini. Hapa wanasheria karibuni mtupe mwanga. Asante.
 
Tunaomba wanasheria humu au wale ambao wanajua sheria watusaidie hapa. Sidhani kama watakuwa wamefukuazwa kazi maana walikuwa ni watuhumiwa, they were still innocent until proved otherwise. Sielewi kama familia zao zilikuwa zinapokea mishahara yao. Ila nakumbuka kumsikia mke mdogo wa Zombe akisema ametoka kupokea fedha ya uniform ya mumewe, December 2008. Hivyo, naamini bado wote walikuwa ni watumishi wa Jeshi la Police hadi kesi itakapohukumu. Kwa mawazo yangu nafikiri walioachiwa huru wana haki ya kurudishwa kazini. Wakitaka kuandika madai sijui yatakuwa ya nini. Hapa wanasheria karibuni mtupe mwanga. Asante.
Nashukuru kwa taarifa mkuu...Hope wanasheria ndani ya JF watatusaidia zaidi kwa michango mingine
 
Swali la nyongeza, na wale askari ambao bado wanaendelea kutajwa kwenye ushahidi/utetezi wa washtakiwa waliosalia, mwelekeo unakuwaje? Wanaweza kurudishwa tena ili hali mahakama ilishaona kuwa hawakuhusika?
 
Tunaomba wanasheria humu au wale ambao wanajua sheria watusaidie hapa. Sidhani kama watakuwa wamefukuazwa kazi maana walikuwa ni watuhumiwa, they were still innocent until proved otherwise. Sielewi kama familia zao zilikuwa zinapokea mishahara yao. Ila nakumbuka kumsikia mke mdogo wa Zombe akisema ametoka kupokea fedha ya uniform ya mumewe, December 2008. Hivyo, naamini bado wote walikuwa ni watumishi wa Jeshi la Police hadi kesi itakapohukumu. Kwa mawazo yangu nafikiri walioachiwa huru wana haki ya kurudishwa kazini. Wakitaka kuandika madai sijui yatakuwa ya nini. Hapa wanasheria karibuni mtupe mwanga. Asante.

Wale watatu walioachiwa walishafukuzwa kazi kwa mujibu wa taratibu za ajira katika jeshi la Polisi, hili lilithibitishwa na Chagonja last week. Taratibu zinasema kuwa askari yeyote atakayeshitakiwa katika mahakama ya kiraia atatakiwa kufukuzwa kazi mara moja. Lakini wana haki ya kukata rufaa katika bodi ya ajira ya jeshi la polisi, inayoongozwa na IGP.
Kuhusu Zombe, yeye taratibu za ajira yake zipo tofauti kwa sababu alishafika katika cheo cha ngazi za juu. Yeye kufukuzwa kwake inabidi mpaka kipatikane kibali kutoka ngazi za juu serikalini (sina uhakika ni ngazi ipi hasa), ndio maana anahesabika kuwa amesimamishwa kazi mkapa kesi yake itakapomalizika ndipo hatima yake itakapojulikana
 
Mimi si mwanasheria lakini shria ya kawaida ya kazi ni kuwa mfanyakazi anapokuwa ameshitakiwa kwa jinai basi atasimamishwa kazi na atakuwa analipwa mshahara kamili, akikutwa na hatia atafukuzwa kazi, akiwa hana hatia atarudishwa kazini na mishara yakeyote atalipwa.

Tatizo la hili suala la Polisi ni kuwa Majeshi yetu yanatawaliwa na sheria za kijeshi na si za kawaida za kazi!
 
Wale watatu walioachiwa walishafukuzwa kazi kwa mujibu wa taratibu za ajira katika jeshi la Polisi, hili lilithibitishwa na Chagonja last week. Taratibu zinasema kuwa askari yeyote atakayeshitakiwa katika mahakama ya kiraia atatakiwa kufukuzwa kazi mara moja. Lakini wana haki ya kukata rufaa katika bodi ya ajira ya jeshi la polisi, inayoongozwa na IGP.
Kuhusu Zombe, yeye taratibu za ajira yake zipo tofauti kwa sababu alishafika katika cheo cha ngazi za juu. Yeye kufukuzwa kwake inabidi mpaka kipatikane kibali kutoka ngazi za juu serikalini (sina uhakika ni ngazi ipi hasa), ndio maana anahesabika kuwa amesimamishwa kazi mkapa kesi yake itakapomalizika ndipo hatima yake itakapojulikana

Mkuu unaweza nipa source ya kauli ya Chagonja?, nature ya hii case ni tofauti. Nilichokuwa na nailichowahi kusikia ni kuwa hawa wote bado ni waajiriwa wa jeshi la polisi na wanapata nusu mshahara kila mwezi mpaka kesi ikiimalizika. Sasa hatma ya wale watatu ni kwamba watarudi kazini, watalipwa malimbikizo yao ya nusu mshahara kwani hawana hatia. Nafikiri kushitakiwa kwenye mahakama ya kiraia itakuwa ni kama askari kafanya uhalifu nje uraiani, lakini hawa wanakabiliwa na kufanya uhalifu wakiwa wanatekeleza majukumu yao.
 
Back
Top Bottom