Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,427
Jamani ! chonde chonde! chonde! Viongozi wa CHADEMA,
Nawahakikishieni:
Nina akili timamu wakati huu naandika hapa, nina nia njema na nimefanya utafiti wa kutosha kabla ya kuongea ninachoongea. Ukali wa kichwa cha habari hapo juu ni halisia na sio kuigiza. Tafakarini kwa haraka na kuchukua hatua tafadhali sana sana!
- Naomba kwa heshima kubwa Viongozi wa CHADEMA (waandamizi) wakutane kwa haraka kadiri iwezekanavyo, Waridhiane na kuita vyombo vya habari na kuwaeleza maeneno machache tu "Tumeyamaliza, yaliyopita yamepita, tuko pamoja na tunasonga mbele" au maneno yenye maudhui kama hayo.Ni muhimu kuwaona Mbowe, Dr.Slaa na Zitto wakiwa kwenye press conference kwa pamoja huku wakishikana mikono. Nivyema kufanya hivyo bila kupoteza hata dakika. tafadhali sana!
- Wafute shutuma zote zinazomkabili Zitto bila masharti. Kuhusu wengine wanaokabiliwa na shutuma watumie busara tu kufikiri ni nini wanaweza kufanya.
- Chonde chonde tafadhali; fanyeni hivyio ikiwezekana leo.Msisubiri zile siku kumi na nne zifike.Fanyeni hivyo kabla tuhuma hizo 11 hazijavuja kwa wananchi na kujadiliwa. Mkichukulia masikhara, Muda si mrefu linaweza kutokea kosa kubwa sana la kihistoria litakalobadilisha kabisa historia ya chama chetu na kukifanya kionekane kwa sura tofauti kabisa.Chonde chonde viongozi wa chama fanyeni hivyo kukinusuru chama tafadhali.
- Mtu anaweza kusema hatuwezi kuwachagulia viongozi chakufanya: Tafadhali sana: naomba tusilaumiane, kuzozana au kuendelea kunyosheana vidole katika wakati huu.Tufanye hili kwanza halafu ndo tuendelee na mengine.Ni hatua ya dharura!
Nawahakikishieni:
Nina akili timamu wakati huu naandika hapa, nina nia njema na nimefanya utafiti wa kutosha kabla ya kuongea ninachoongea. Ukali wa kichwa cha habari hapo juu ni halisia na sio kuigiza. Tafakarini kwa haraka na kuchukua hatua tafadhali sana sana!