mwanzoni nliwasifia sana hawa jamaa lakini walipoanza kushambulia wafanyakazi wa ngazi za chini kabisa kama walimu nikoana kua hawa watuhawafai kabisa. Inabidi waelimishwe wajue kua adui yao ni yupi kabla hawajaanza kuponda watu.
Mmmh jaman huyu Makamu wa Rais amekuja saa ngapi huko, mbona leo mchana nimemuona akielekea njia ya White Sand"
Aliyekuja ni kamishna wa polisi Paul Chagonja ila sidhani kama kuna jipya atakalolifanya! kwasababu jana wakati akiongea na wananchi baada ya kutembezwa eneo la tukio ametoa kauli za kuwalaumu wananchi kwamba badala kuchoma moto ofisi ya ocd na maduka wangefungua kesi dhidi ya vyama vya ushirika lakn akaahidi kufanya upelelezi na kuubaini ukweli!
ameongea na waathirika wa vipigo na moto? Alisema angeongea nao leo..
habari ya wewe mkuu! Vp kuhusu kikao cha leo hujapata taarifa bado?
Ni kweli mkuu na jambo linaloshangaza kabla ya tukio askari PolisiWasi wasi wangu ni kwamba je, huo upelelezi utakuwa wa haki kweli kwani yeye mwenyewe tayari ameshaanza kuelekeza lawama kwa wananchi na kuwahusisha na uchomaji huo'
-hivi inawezekanaje mtu anayedai jasho lake halafu mtu huyo huyo akateketeza mali zake kwa moto?
-siku ya tukio hakukuwa na vurugu yoyote, kwanini polisi walizuia watu kuja kuokoa mali zao na kuziacha ziteketee kwa moto?
-jana askari walikuwa na operesheni ya kupiga, kuvunja maduka na kupora mali za raia vijijini, hii maana yake nini?
Moto mkubwa ambao taarifa za awali zinasema umetokana na hitilafu ya umeme katika
ofisi ya upelelezi ya wilaya umeteketeza maduka kadhaa na soko zima la Tandahimba ikiwa
ni pamoja na ofisi hiyo ya upelelezi,
Habari za kuaminika kutoka kwa mashuhuda kadhaa zinadai kuwa moto huo ulianza majira
ya saa moja jioni jana. Jambo la kushangaza ni kitendo cha polisi kununua petroli na kwenda
kumwagia baadhi ya maduka huku wakiwazuia watu waliojaribu kwenda kufanya uokozi wa
mali zao.
HABARI YA UHAKIKA - mtu mmoja ambaye ana duka lake eneo hilo
(Abdalah Abdalah Camumkungu) alienda na gari lake eneo la tukio, hata hivyo alichomolewa
kwenye gari lake na kupata kipigo kikali huku akishuhudia askari wakiteketeza gari lake kwa moto.
Pia INASEMEKANA wananchi kadhaa wamelishuhudia tukio hilo la askari kuchoma moto maduka
Wakati huohuo: Leo Mkuu wa Jeshi la Polisi Saidi Mwema akiongozana na makamu wa Rais Dr.
Bilali wamewasili Tandahimba kwenda kutafuta suluhu ya mgogoro huo.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Taarifa za awali tulizozipata wakazi wa Tandahimba zilisema kuwa hao nikwa kurudiarudia neno 'inasemekana' inaonyesha jinsi usivyo n uhakika na unachokisema. Si kweli kwamba mwema na bilali wako tandahimba. Waliokwenda huko ni afande chagonja na rpc. Hebu tulinde heshima ya jf kwa kusema ukweli jamani!
Nashukuru Vijisenti kafafanua hapo juu. INASEMEKANA - ni taarifa ambazo sinakwa kurudiarudia neno 'inasemekana' inaonyesha jinsi usivyo n uhakika na unachokisema. Si kweli kwamba mwema na bilali wako tandahimba. Waliokwenda huko ni afande chagonja na rpc. Hebu tulinde heshima ya jf kwa kusema ukweli jamani!
kwa kurudiarudia neno 'inasemekana' inaonyesha jinsi usivyo n uhakika na unachokisema. Si kweli kwamba mwema na bilali wako tandahimba. Waliokwenda huko ni afande chagonja na rpc. Hebu tulinde heshima ya jf kwa kusema ukweli jamani!
Tandahimba ni mojawapo ya maeneo ambayo ccm inatumia ukilaza wa wananchi kuendeleza utawala wa kiimla. 2015 ndio nafasi yenu kutorudia kosa la kuichagua ccm