kivyako
JF-Expert Member
- Feb 2, 2012
- 14,341
- 12,045
Da pole sana kaka mi ilinitokea Sinza siku moja kwenye lodge moja hivi. Nilikuwa na Shem wenu ndani ya chumba tukagombana coz ma gal alikuwa anawivu sana.
Baada ya kugombana nikabidi mi nisepe zangu nikaona hamna dalili ya kupata mzigo hapa but kipindi naondoka Shem wenu alikuwa yupo anaoga.. Mi nipo njiani nakaribia pale meeda nikaona kundi kubwa la watu km 10 hivi wananifata na kuita mwizi mwizi mi nikashangaa vp. Ghafla namuona mlinzi wa lodge anasema kuna demu mmoja Anasema umemwibia pochi yenye laki 2..watu baada ya kusikia hivyo wakaanza kunipiga mdogo mdogo kwamba lazima tukuchome wewe, watu wakawa wanaongezeka na kipondo kinaongezeka yani sipati hata muda wa kujitetea.
Mara gafla akatokea jamaa mmoja tulipiga naye mzumbe chuo amani Mimi mtu huyu namjua twendeni turudi lodge Kwa huyo binti aliyeibiwa, basi tukarudi watu kama 20 ivi hapo nishapigwa sana jamani.. Tukafika guest house pale, Dada wa reception akasema yule msichana kaondoka sasa hivi kafatwa na mwanaume akiwa na gari..kuhusu pochi kumbe kaiona ilikuwa chini ya mto. Sitoisahau that day
Huyo ni shem wetu kweli?