Kamende
JF-Expert Member
- Mar 1, 2008
- 416
- 45
Katibu Mwenezi wa CHADEMA wilaya wa Handeni mkoani Tanga Ndugu Omari Gomangilo ametishiwa kuuawa na Mhe. Diwani wa kata ya Komkonga (CCM) Mhe. Ramadhani Kisatu baada ya Mwenezi huyo kutoa mchango wake katika mkutano kwamba haoni sababu ya wananchi kuchangishwa kwa ajili ya huduma za hosipitali wakati hakuna dawa wala vipimo vinavyofanyika hosipitalini hapo.
Akiwa amekwishatoa kauli hiyo iliyoshangiliwa sana na wananchi wa mji mdogo wa Kabuku, Mwenyekiti wa UWT aliyekuwepo eneo hilo alimwita Mhe. Kisatu ambaye alifika mara moja na kuanza kumtishia Gomangilo.
Kisatu kwa kujiamini alimfokea Gomangilo kwa kumwambia kwamba atamfanya kitu mbaya maana kwanza ana hela na anaweza kumficha asionekane milele. Gomangilo alipomuuliza kama atamfanyia kama walivyomfanyia Dr. Ulimboka alimjibu "Nitakachokufanya wazazi wako hawatakaa wakuone tena" Hainichukui muda kukupoteza jumla mimi" alimalizia.
Gomangilo kuona yamekuwa makubwa akaenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Kabuku ambako muda mfupi madiwani 6 wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni walifika na kumsihi wakayamalize nje ya polisi. Hata hivyo Goma alikataa na ndipo polisi walipomuweka ndani Mhe. Kisatu na kumlazimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni kumwekea dhamana hadi Jumatatu kesi hiyo itakapopelekwa mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa.
uchunguzi wa kina umebainisha kwamba Uongozi wa CCM mkoa wa Tanga una ugomvi wa muda mrefu na bwana Omari Gomangilo ambaye amjiunga na CHADEMA baada ya kujivua gamba akiwa kiongozi wa UV-CCM hapo hapo Handeni na anaijua sana CCM. Uongozi wa CCM umekuwa ukifanya bidii kumtisha na kumfanya apunguze kasi lakini ameshindikana.
Taarifa nyingine zimetua mezani kwangu kwamba mwezi Februari mwaka huu Mwigulu Nchemba alipita Komkonga akiwa njiani kwenda Arumeru, ambako alikutana na Mhe. Diwani Ramadhani Kisatu ambapo pamoja na majukumu mengine mipango ya kuzima moto wa CHADEMA ilipangwa.
Wananchi wanasema kuwa kabla Kisatu hajakutana na Mwigulu mwezi Februari alikuwa mtu mpole na mkarimu sana. Lakini baada ya tu ya mwezi Fubruari amebadilika na kuwa mtu mwenye majivuno, anayejiamini kupia kiasi, mwenye matishio na mkatili sana.
Wanajamvi hadi ninaleta ujumbe huu viongozi wa CHADEMA wilaya ya Handeni walikuwa kwenye kikao wakipanga namna ya kuhakikisha usalama wa Katibu Mwenezi wao na wao wenyewe.
Ninaona sasa kwamba kila apitapo Mwigulu anaacha hofu kubwa kwa maisha ya watu na anavuruga sana utengemano na udugu katika jamii.
Akiwa amekwishatoa kauli hiyo iliyoshangiliwa sana na wananchi wa mji mdogo wa Kabuku, Mwenyekiti wa UWT aliyekuwepo eneo hilo alimwita Mhe. Kisatu ambaye alifika mara moja na kuanza kumtishia Gomangilo.
Kisatu kwa kujiamini alimfokea Gomangilo kwa kumwambia kwamba atamfanya kitu mbaya maana kwanza ana hela na anaweza kumficha asionekane milele. Gomangilo alipomuuliza kama atamfanyia kama walivyomfanyia Dr. Ulimboka alimjibu "Nitakachokufanya wazazi wako hawatakaa wakuone tena" Hainichukui muda kukupoteza jumla mimi" alimalizia.
Gomangilo kuona yamekuwa makubwa akaenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Kabuku ambako muda mfupi madiwani 6 wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni walifika na kumsihi wakayamalize nje ya polisi. Hata hivyo Goma alikataa na ndipo polisi walipomuweka ndani Mhe. Kisatu na kumlazimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Handeni kumwekea dhamana hadi Jumatatu kesi hiyo itakapopelekwa mahakamani kwa ajili ya kusikilizwa.
uchunguzi wa kina umebainisha kwamba Uongozi wa CCM mkoa wa Tanga una ugomvi wa muda mrefu na bwana Omari Gomangilo ambaye amjiunga na CHADEMA baada ya kujivua gamba akiwa kiongozi wa UV-CCM hapo hapo Handeni na anaijua sana CCM. Uongozi wa CCM umekuwa ukifanya bidii kumtisha na kumfanya apunguze kasi lakini ameshindikana.
Taarifa nyingine zimetua mezani kwangu kwamba mwezi Februari mwaka huu Mwigulu Nchemba alipita Komkonga akiwa njiani kwenda Arumeru, ambako alikutana na Mhe. Diwani Ramadhani Kisatu ambapo pamoja na majukumu mengine mipango ya kuzima moto wa CHADEMA ilipangwa.
Wananchi wanasema kuwa kabla Kisatu hajakutana na Mwigulu mwezi Februari alikuwa mtu mpole na mkarimu sana. Lakini baada ya tu ya mwezi Fubruari amebadilika na kuwa mtu mwenye majivuno, anayejiamini kupia kiasi, mwenye matishio na mkatili sana.
Wanajamvi hadi ninaleta ujumbe huu viongozi wa CHADEMA wilaya ya Handeni walikuwa kwenye kikao wakipanga namna ya kuhakikisha usalama wa Katibu Mwenezi wao na wao wenyewe.
Ninaona sasa kwamba kila apitapo Mwigulu anaacha hofu kubwa kwa maisha ya watu na anavuruga sana utengemano na udugu katika jamii.