HATARI 2015 Kwa wagombea NJAA wa UBUNGE Na UDIWANI

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
Dalili hizi tunazozidi kuziona kila siku Za wananchi kujichukukia sheria mkononi na kuwaadhibu Viongozi Wao waliotumia madaraka ya Ubunge au udiwani kujineemesha wenyewe zinatupa Picha kwamba mwaka 2014 utakuwa mwaka wa TAFAKARI Kwa wananchi wanaowaza kugombea Ubunge Au Udiwani.

Matukio haya ambayo polepole yalianza Kwa kuchoma mali Na thamani Za viongozi kule Mtwara, Sasa yameshika kasi si kuchoma Mali Za walengwa tu Bali mauaji. Viongozi wetu wengi wanazidi kupukutika kuanzia Mwanza, Musoma, Mbeya Na penginepo upepo unazidi kushika kasi Na Hakuna anayependa kuwa shabiki wa mauaji haya lakini ni dhahiri hayadhibitiki Kwa mfumo wa serikali ya kipumbavu ambayo inadiriki kuwasimamisha Kazi mawaziri wanne Kwa Inshu Za Tembo.. Animal Tembo wakati watanzania wanauawa, wanateshwa, wananyanyasika iko Kimya ila Kwenye Tembo wamesimamisha mizigo minne, nani Kati yangu na wewe personal ameshawahi kufaidika direct Na Tembo, funny enough wauaji, wafanya biashara, Na wamiliki wa vyombo vya kusafirishia nyara za Serikali kiharam ni Wao wenyewe hii inakera zaidi ya matapishi..

Lakini Kwa Upande wa pili Waheshimiwa ambao mmejineeshea madaraka mjue hamko safe, mwaka 2014 mjiandae kukabiliana Na wananchi Wenu hao hao waliowachagua, wakati mkijiandaa kuchota kiinua mgongo chenu Cha milioni 600 wananchi watakuwa wakikingojea njiani mgawane au wakichukue chote. Salama yenu mbakie huku huku bongo Na msionekana kabisa jimboni..

HAUWEZI Kuwa salama, Kama Kiongozi Umejineemesha huku umezungukwa Na majirani mafukara Na wakakuacha, that's why 90% ya wabunge wanaishi Mbali Na Makwao. Niambie nani Mbunge asiye Na Nyumba Jijini DSM show me mmoja tu.. !!! Kila Mtu yuko Bongo..! Analiongoza jimbo kupitia cm Yake ya mkononi..

Wale mnao jiandaa kugombea Ubunge Na Udiwani hiyo 2015 kuneemeasha Matumbo yenu mjue mtakabiliana Na Hatari hiyo.. TAFAKARINI UPYA..
 
Back
Top Bottom