Hata PAYE ilipopunguzwa watu walishangilia bila kujua ni kiasi gani hasa kimepunguzwa

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Walipotangaza kupunguza PAYE kutoka asilimia 11(kama sikosei) mpaka asilimia 9 watu walishangilia sana utazani punguzo hilo la asilimia 2 linahusu kila mfanyakazi na kwamba ingesaidia sana watumishi.

Siki chache baadae serikali hiyo hiyo iliodai imetoa punguzo ili kumsaidia mtumishi ikaja na nyongeza ya makato ya Bodi ya Mikopo kutoka asilimia 8 mpaka 15.

Wakati huo huo hela zote hizi zikikusanywa zinaenda kwanza kuwekwe kwenye kapu moja pale BOT kabla ya kuzisambaza na zote ni mali ya serikali.Wanavyozigawa wanajua wenyewe kwahiyo wakiamua kujifidia kupitia hiyo nyongeza ya makato hakuna anaejua.

Watu huwa wanashangili bila hata kutafakari kwanza na sijui watu hawa huwa wanakuwa wameandaliwa kushangilia maana mimi sielewi kabisa.

Jana kuna kodi zimefutwa na zingine kupunguzwa ila zikafidiwa kwa kuongeza kodi kwenye mafuta ya petroli na kwenye vinywaji.Yaani badala ya kubuni vyanzo vipya vya mapato kufidia kodi hiyo iliyopunguzwa, wao wakaongeza mzigo wa kodi kwenye bidhaa nyingine ambayo tayari nayo inatozwa kodi huku bidhaa yenyewe ikiwa ni nyeti kabisa na watu wakashangilia!!.

Leo hii kuna watu wanatumia magari tarehe za mwisho wa mwezi baada ya kupata mishahara na ikifika katika ya mwezi wengine hupaki magari kisa wanashindwa kumudu kununua mafuta na wengine hupunguza kabisa matumuzi ya magari yao.

Sasa ukiongeza kodi na bei ya mafuta ikapanda,watu hawa sio ndio watazidi kupaki magari na wakipaki magari au kupunguza mizunguko hiyo kodi unayotarajia kukusanya kutokana na mauzo ya petroli itaweza kweli kufidia hilo pengo?

Bila kubuni vyanzo vipya vya mapato na kila siku tukabaki na kucheza na vyanzo vile vile,tutabakia na kuwa na bajeti kubwa za kisiasa kwenye makaratasi lakini kiuhalisia inakuwa hamna kitu na bajeti hizi zitakuwa hazitekelezeki kama ambayo zimekuwa hazitekelezeki miaka yote.

Hii ni Bajeti ya kung'ata na kupuliza ila itang'ataza zaidi kuliko kupuliza utekelezaji ukianza.

Nadhani wanaoshangilia ama huwa hawatafakari au huwa wanaandaliwa kufanya hivyo kwasababu za kisiasa.

Time will tell.

Wanasema sisi tunapinga kila kitu lakini wanasahau kuwa wao wanaharibu kila kitu.
 
Hii nchi ya ajabu sana... Cha ajabu hata wabunge ambao ni wawakilisbi wetu nao wameingia kwenye mkumbo huo..
 
Wabunge wengi wengi wanajua kusoma na kuandika. Usitegemee wataweza kuchambua bajeti na kuonyesha kasoro zilizopo.
Mkuu,ndio maana nliijisemea:

"One of the big problems of this country is that,the intelligent people have only forums to express their views and ideas, whereas the unintelligent ones have forums as well as power and mandate to implement their ideas."
 
Ni masaa kadhaa yamepita wapinzani hatujaja na credible arguments kupambana na bajeti ya kisomi ya kubalifu ya CCM. Tujipange vizuri vinginevyo hatuna chetu 2020
 
Ni masaa kadhaa yamepita wapinzani hatujaja na credible arguments kupambana na bajeti ya kisomi ya kubalifu ya CCM. Tujipange vizuri vinginevyo hatuna chetu 2020
Sometimes it needs to be intelligent to understand the intelligent person-You are not such intelligent to understand the opposition.

Time will help you to understand.
 
Sometimes it needs to be intelligent to understand the intelligent person-You are not such intelligent to understand the opposition.

Time will help you to understand.
Siku zote CHADEMA tunatumia muda mwingi kupambana na ukweli. Ukweli siju zote hauhitaji nguvu kupambana nao. Wenzetu walipoweza tuwaunge mkono.
 
Nadhani sasa badala ya kulalamika na kila siku kusema,tu serikali ilete ama iangalie vyanzo vipya vya mapato bila kuvitaja..nadhani sisi wapinzani katika majukwaa yetu tuanze kuvitaja,kuorodhesha na namna vyanzo hvyo vipya vitakavyoleta kodi na mapato.lakini si kwa hili ulilosema ama kuliandika,bila kueleza mifano au vitu tufanye ama serikali ianzishe.naomb tuanzie hapo ili tuweze kuisaidia serikali!
 
Ni masaa kadhaa yamepita wapinzani hatujaja na credible arguments kupambana na bajeti ya kisomi ya kubalifu ya CCM. Tujipange vizuri vinginevyo hatuna chetu 2020
Bajeti ya kisomi au mwendelezo wa udanganyifu.tusubiri June 2018 .tutafanya conclusion !!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom