Hata Mugabe wakati anaharibu uchumi wa nchi yake alishangiliwa sana na kuitwa mzalendo,leo wanalia!

Mikataba ya kinyonyaji unaweza kuipinga mahakamani au ukamwita aliyekuzidi kete mkakaa mezani mkarekebisha,mpaka sasa ni Acacia tu ndiye kashika mpini sisi tumeshika makali
kwa hiyo rais aache tu kufuatilia haya mambo?
 
Upo naive na masuala haya! Hakuna haki mahakamani.
Kwa hiyo kesi hii itaamuliwa wapi?

Acacia mpaka jana wameipinga ripoti hiyo kwa nguvu zote,wanasema aliyeiandika pengine ana tatizo la ndoto za mchana!
 
Wew na wewe ni mbwa wa kizungu tu kama wakina puppy,bulldogy,pety,wolf, si bora tule nyasi kuliko kula ugali wa masimango kwa hili nitasimama na magufuli likituchachia bhas ameonesha kujar kuliko uwoga kama wako usiwe pono amka bwana
 
Kwaiyo tuache wachukue madini pasipo kulipa kodi Kama uchumi unayumba kwa kusimamia mapato basi
 
Yaani watu munaombea balaa tu! sijui ni kwa faida ya nani?
Mleta thread mjinga na zuzu, haoni hata tofauti, yaonekana kaathirika na huu ufisadi, sio siri yeye na wenzake wamejaa humu..angejuwa tofauti alichofanya JPM na Mugabe sidhani hata kama angeandika hivi..
 
Somji upo na babu yakoE="Somji Juma, post: 21611027, member: 47372"]
1982e100bf1c2ca0dcf5215e122404e6.jpg


c8ba1eb00eb0ecc4ff59e138e6636dc9.jpg
[/QUOTE]
Somji
 
Ajaambiwa aache ila atumie njia sahihi

kwa hiyo hajatumia njia sahihi kutaka marekebisho ya sheria za mikataba na za madini yafanyike? mbona mmerogwa kwa kuwa na fear of unknown? kwa huu uoga pasipo watu kama magufuli kila kitu kitakuwa cha wazungu.
 
Kuna watu wanaona ni sawa kuendesha nchi kwa mikataba ya kinyonyaji,alipokosea mugabe ndipo tutakaporekebisha sisi
Ulisaini mwenyewe hukulazimishwa,CCM ilikubali masharti yote ,Tatizo lipo wapi,Umekubali kuuza gari mwenyewe baadae unasema umeonewa,Tumia akili mkuu
 
mkuu, tatizo letu Watanzania liko hapa....tumo kwenye 10 hovyo katika nchi ambazo raia wake wana IQ ndogo duniani.
Na kweli wenye IQ kubwa walichotufanyia yameonekana kwenye ripoti zote 2, kuibiwa na wengi kukubali ila wachache kukataa sababu ya pesa, kutaka kuishi maisha feki na uchumi feki wakati hali halisi haikubali labda uibe tu, kukaa chini ya miti na fremu kupiga domo mpaka jioni, kushinda kwenye misiba kama vile ndio ukombozi wa maisha, kupenda kukimbilia ajali kama vile kuna makinikia pale, kupenda short cuts kupindukia, vyeti feki, wafanyakazi hewa, uzinzi wa kwa viongozi wa upinzani, kupinga kila kitu, ufisadi, rushwa, kujenga majumba 70 kwa mshahara wa laki saba n.k. n.k.
Twakubali IQ zetu ndogo kwa hili, maana kwa kawaida mtu huwezi kumpa mwekezaji hati miliki ya rasilimali na maliasili zote na wewe kubaki mtupu...
Kwa hili nakubali wala sikatai, sisi IQ zetu ni ndogo mno..na atakayebisha kwa hili basi IQ zake ni ndogo zaidi ya udogo..
 
Mugabe wakati anaivuruga Zimbabwe ,alishangiliwa na kusifiwa sana kwa kuitwa shujaa,kila aliyemuonya alionekana mbaya,leo tunavuruga uchumi kwa sababu za kupika na tena zinapikwa na wanasiasa,tunasahau kwamba robo ya mapato au karibu robo ya mapato ya TRA hutoka ACACIA(kwa mwaka),hatuangalii kesho tutapata dawa hospitali na tumeamua kutofata utaratibu wa sheria ili maisha yaendelee,nchi imehamishiwa kwenye TV.

Hugo Chavez naye wakati anavuruga uchumi wa Venezuela alishangiliwa sana,leo hata chakula hakuna katika nchi hiyo!

Akina kambona wakati wanaupinga ujamaa,walionekana wabaya sana mpaka baadae Nyerere alipoona ujamaa ni mfumo mfu, akarudi kwenye ubepari ulioungwa mkono na kambona,lakini kipindi hicho kambona aliimbwa kwa kila jina baya, nchi ikafilisika watu wakawa masikini kwelikweli,

Hata leo, tunaibomoa nchi huku tukishangilia,tutayaona matunda ya kuibomoa nchi hii ndani ya miezi michache ijayo,kama tulivyoona pale bandarini,kwenye sukari na sekta nyingine na mpaka sasa kuna baadhi ya ofisi za umma hasa dispensary,zimebaki na wafagizi tu,watumishi wengine tumefukuza
Hivi umefufuka lini? kama mtu huyu anatokea Lumumba tafadhari mnyang'anyeni kadi.
 
Mwenye macho hambiwi tazama,siku zenyewe za machozi jasho na damu bado zinakuja

Mpk sasa mheshimiwa kasha tu disappoint ktk mengi,swala la ACACIA limezima discussion za bajeti,uhakiki wa vyeti na ajira na naona sasa swala la mikopo ya elimu ya juu watz mshalinyooshea mikono mtanyooka tu kila idara

5 yrs ndo hiyo inaisha, Noah nazo haziwaachi wanaharakati salama

T.R.A wanataka kodi hadi kwa waendesha baiskeli
Naa....
 
Unashauriwa ujifunze kwa waliofanikiwa na sio walioshindwa kama mugabe watu wenye mawazo hasi kama wewe hutakiwi kuyatoa ktk watu waliochoka na unyonyaji wa nchi hii.ebu badirikeni bwana.
 
Back
Top Bottom