Hata madaktari wanahusika na ukosefu wa vitendea kazi na wao wajiiangalie!!

chama

JF-Expert Member
Aug 6, 2010
8,001
2,418
Baada ya hotuba ya mh. Raisi Kikwete inaonyesha wazi serikali imeanza kutekeleza madai ya madaktari; ipo tayari kwa majadiliano; moja ya dai kubwa la ni kukosekana kwa vitendea kazi; ni ukweli mtupu wapo madaktari wasio waaminifu wanahusika mojamoja kwa moja na upotevu/ wizi wa vifaa na kuviuza kwenye hospitali binafsi; ukosefu wa dawa unachangakiwa kwa kiasi kikubwa na wizi wahusika wapo madaktari wafanyakazi wengine ambao leo hii nao bila aibu wameshika bango la mgomo; hata hii la kuharibika CT scan mashine ipo tetesi iliharibiwa kwa makusudi ili wagonjwa waende kwenye hospitali binafsi; ni lazima tumbuke wengi wa madaktari hawa wanafanya kazi kwenye hizi hospitali binafsi; ili kuzuia migomo na kuboresha sekta ya haya machache:

1. Serikali ifunge hospitali za binafsi, mashirika ya kidini tu na taasisi za kujitolea sio za kifamilia ndio yaruhusiwe kuendesha hospiatali; hii itadhibiti upotevu wa vitendea kazi
2. Serikali isitishe kutoa leseni za maduka ya madawa; utitiri wa maduka haya unachangia kwa kiasi kikubwa wizi wa madawa kutoka hospitali za serikali.
3. Serikali tu ndio iwe muagiziaji wa madawa na vifaa kutoka nje; hata kama taasisi inataka kuagiza serikali ni lazima ihusishwe hii itasaidia kujua nani aliagiza na wapi vifaa hivi vimekwenda.
4. Mishahara ipangwe na kuwa reviewed kila baada ya muda maalumu; mikataba ya ajira iwe wazi ili yule asiyekubaliana nayo akatafute mwajiri atakayekidhi mahitaji
5.Ijengwe hospitali maalumu kwa ajili ya watoto na kinamama wajawazito; hospitali kubwa ziboreshwe, viongozi wetu waache mara moja tabia ya kujitibia India na kwingineko hii; itaondoa manung`uniko miongoni mwa watendaji wa sekta ya afya.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Uko sahihi kabisa.Vifaa vingi na adawa ya hospitali za serikali vinaibwa na kuishia hospitali na zahanati binafsi za baadhi ya madaktari waloanzisha hizo zahanati na wahisika ni baadhi ya madaktari
 
sio wote,na hao wanaofanya hivyo wangekuwa wanalipwa vizuri wasingekuwa wanafanya hayo!kama kuna walioiba wala hawagomi wako wanaendelea na shughuli zao ila wazalendo ambao hawaibi ndo wanaogoma ili waboreshewe mazingira maana wenyewe hawataki wizi
 
kama huna data kaa kimya dk ataibaje dawa au vifaa wkt yy si mtunzaji wa hvyo vifaa. kama azimio la Abuja serikali ililiridhia ambalo linataka kila nchi ya Affrica kutenga 15% ya total budget kwny afya inakuwaje ss tutenge 9% tu? je huo si ndo upuuzi wa ccm?
 
Veru tru, baada ya kuviiba na kuviharibu wanailaumu serikali


Baada ya hotuba ya mh. Raisi Kikwete inaonyesha wazi serikali imeanza kutekeleza madai ya madaktari; ipo tayari kwa majadiliano; moja ya dai kubwa la ni kukosekana kwa vitendea kazi; ni ukweli mtupu wapo madaktari wasio waaminifu wanahusika mojamoja kwa moja na upotevu/ wizi wa vifaa na kuviuza kwenye hospitali binafsi; ukosefu wa dawa unachangakiwa kwa kiasi kikubwa na wizi wahusika wapo madaktari wafanyakazi wengine ambao leo hii nao bila aibu wameshika bango la mgomo; hata hii la kuharibika CT scan mashine ipo tetesi iliharibiwa kwa makusudi ili wagonjwa waende kwenye hospitali binafsi; ni lazima tumbuke wengi wa madaktari hawa wanafanya kazi kwenye hizi hospitali binafsi; ili kuzuia migomo na kuboresha sekta ya haya machache:

1. Serikali ifunge hospitali za binafsi, mashirika ya kidini tu na taasisi za kujitolea sio za kifamilia ndio yaruhusiwe kuendesha hospiatali; hii itadhibiti upotevu wa vitendea kazi
2. Serikali isitishe kutoa leseni za maduka ya madawa; utitiri wa maduka haya unachangia kwa kiasi kikubwa wizi wa madawa kutoka hospitali za serikali.
3. Serikali tu ndio iwe muagiziaji wa madawa na vifaa kutoka nje; hata kama taasisi inataka kuagiza serikali ni lazima ihusishwe hii itasaidia kujua nani aliagiza na wapi vifaa hivi vimekwenda.
4. Mishahara ipangwe na kuwa reviewed kila baada ya muda maalumu; mikataba ya ajira iwe wazi ili yule asiyekubaliana nayo akatafute mwajiri atakayekidhi mahitaji
5.Ijengwe hospitali maalumu kwa ajili ya watoto na kinamama wajawazito; hospitali kubwa ziboreshwe, viongozi wetu waache mara moja tabia ya kujitibia India na kwingineko hii; itaondoa manung`uniko miongoni mwa watendaji wa sekta ya afya.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Back
Top Bottom