Hata kama unafanya kazi ya aina gani sio lazima ujulikane, huo ni ushamba!

mcrounmj

JF-Expert Member
Feb 26, 2016
380
885
Poleni na pilikapilika za kuumalizia mwaka twenty twenty.

Jana nilikuwa kwenye usafili wa basi, kutoka mbeya kwenda mwanza. Ni safari ndefu na inachosha maana ni zaidi ya msaa 18.

Kabla sijaenda kwenye maada husika labda niseme, kuna usumbufu mkubwa mno yanaupata mabasi haya ya mikoani. Ndani ya mkoa mmoja unakuta basi linasimamishwa na traffic wa barabarani zaidi ya saba. Hii inachosha na kukera abiria. Inapelekea kuchelewa kufika safari. Miaka ya nyuma tulipata shida sababu ya miundombinu ilikuwa mibovu, barabara zilikuwa za vumbi.

Leo tumeboresha barabara tatizo limejitokeza kwenye usimamizi wa usalama wetu barabarani. Naomba mamlaka zinazohusika mtoe gag order kwa mabasi ya mikoani yakaguliwe mkoa to mkoa, itasaidia sana kuokoa mda wa abiria na mabasi hayo.

Nirudi kwenye maada. Usalama wa taifa ni idara nyeti ambayo kwa kawaida watumishi wake wamefichwa makusudi kwa ajiri ya kutekeleza majukumu yao ya ushushushu katika hali ya kuliweka taifa salama. Matumaini yangu kuwa hata wanapopatiwa mafunzo, hufundwa namna ya kuishi kwenye jamii wakiwa maafisa vificho, wakitumia cover za kazi zingine ili wasigundulike kuwa ni maafisa usalama na waweze kutekeleza majukumu yao ya ukusanyaji intelijensia.

Sasa wapo maafisa uchwara, ambao pengine wamekosa weledi wa matakwa ya idara yao, kwa makusudi wanataka wajulikane na watu kwenye jamii kuwa wao ni maafisa vificho.

Jana katika safari niliyosema, konda katika route zake za kukagua tiketi, mida ya saa tatu usiku akamugumia mzee furani ivi wa makamo ya kama late forty hivi, akiwa siti ya pembeni yangu, yule mzee alikataa kutoa tiketi akidai ni usumbufu. Kondo akaachana naye akakagua kwa abiria mpaka akamaliza wote ndiyo akamurudia. Mzee amekataa kutoa tiketi anadai ampeleke polisi. Konda kuona hivyo akamvaa, we! Yule mzee alitoa maneno, akasema "ivi unanifahamu mimi ni nani, nitapiga simu hili basi ata lisifike linakokwenda, usicheze na mimi hunijui"

Yule konda naye akaunga nukta na kuelewa, ikabidi amchane "mzee kwani kuna ulazima wa kujulikana wewe ni nani, suala la kutoa tiketi tu unataka basi lote abiria wafahamu kuwa wewe ni nani. Kwanza nyie mara nyingi mnakuwaga ni wale vitengo vya chini, afisa wa juu anakuwa na busara na anaheshimu kazi za wengine".

Konda aliongea ukweli ila mchungu kwa afsa kificho uchwara huyu. Hata kama hakuwa afisa usalama ila mazingira aliyoyajenga ni kama yuko kwenye mkondo huo.

Konda alisema kweli. Kwa afisa usalama anyejielewa, kwanza anakuwa mstaarabu kwa kuheshimu majukumu ya wengine lakini pili anatumia weledi kuishi kadri kazi yake inavyomtaka hivyo hawezi kujionyesha kiboya hivyo.

Usalama wa taifa ni idara nyeti, mnao wajibu wa kuhakikisha taifa liko salama. Tumieni cover zenu kuficha identity zenu kwa maslahi mapana ya taifa letu.
 
Awali ya yote pole kwa safari, huyo si afisa wa usalama ila ni mpumbavu flani mwenye ndugu yake aliye katika mnyororo flani wa madaraka sasa anamtumia katika kutishia wengine
 
Mwaka Jana mwez Kama huu tareh za mwshoni nakumbuka Kama ilikuwa tarehe 19 hiv nilikuwa kwenye kampuni moja hivi siku moja Mara mkuu wa wilaya huyu hapa paaahh.

Maswali na majibu yakaanza Mara vibali vya kampuni viko wapi mi nikamjibu kwakwel bosi hayupo labda tumpgie simu dada akawaka kwa kujimwambafy unajua Mimi ni Nani ni mwanamke huyo mkuu wa wilaya hyo si nikajikuta nmemjibu sitaki kujua hata we ni Nani?

Bhana bhana hata sjakaa sawa afisa usalama mmoja tayar kaniniga namimi si nikamniga kidogo kujibalance sasa nikamwambia Mimi hapa muajiriwa tu na wenye kampuni mda huu hawapo yule dada akatoa tamko nataka vibali haraka Basi nikamwambia ngoja nimpgie.

Ile natoa simu tu ikaporwa duh sasa nikamwambia jaman dada mbona hvo yule Tena afsa usalama ananiulza unajua mimi ni Nani? Me si nikaropoka Elimu yako tafadhar mbona sio msitaarabu hapo nipo na Mdogo ake boss wote ni foreigners hawajamuulza Chochote wanakomaa na black mamba mwenzao Mimi sasa.

Baada Kama ya nusu saa wakapga smu polis ocd akaja akatuchukua tukapelekwa polisi tukaa siku SKU kutoa dhamana hawataki kutupeleka mahakamani hawataki tukaweka wakili tukatoka siku ya nne Ila Cha ajabu mpaka leo hamna kesi.

NB: serikali pia ingejaribu kuwa inawapima na ustaarabu na hawa watu kabla ya kuwapa hzo kazi maana wengne kazi yao Ni kuwatiisha wenzao tu na kutoheshmu shuguli za wenzao hata Kama mtu anafanya kazi unayo ona wewe ya ajabu jua ndo analisha familia na kusaidia wazazi kifupi anategemewa hata Kama unamdharau.
 
Mwaka Jana mwez Kama huu tareh za mwshoni nakumbuka Kama ilikuwa tarehe 19 hiv nilikuwa kwenye kampuni moja hivi siku moja Mara mkuu wa wilaya huyu hapa paaahh

Maswali na majibu yakaanza Mara vibali vya kampuni viko wapi mi nikamjibu kwakwel bosi hayupo labda tumpgie simu dada akawaka kwa kujimwambafy unajua Mimi ni Nani ni mwanamke huyo mkuu wa wilaya hyo si nikajikuta nmemjibu sitaki kujua hata we ni Nani?

Bhana bhana hata sjakaa sawa afisa usalama mmoja tayar kaniniga namimi si nikamniga kidogo kujibalance sasa nikamwambia Mimi hapa muajiriwa tu na wenye kampuni mda huu hawapo yule dada akatoa tamko nataka vibali haraka Basi nikamwambia ngoja nimpgie

Ile natoa simu tu ikaporwa duh sasa nikamwambia jaman dada mbona hvo yule Tena afsa usalama ananiulza unajua mimi ni Nani? Me si nikaropoka Elimu yako tafadhar mbona sio msitaarabu hapo nipo na Mdogo ake boss wote ni foreigners hawajamuulza Chochote wanakomaa na black mamba mwenzao Mimi sasa

Baada Kama ya nusu saa wakapga smu polis ocd akaja akatuchukua tukapelekwa polisi tukaa siku SKU kutoa dhamana hawataki kutupeleka mahakamani hawataki tukaweka wakili tukatoka siku ya nne Ila Cha ajabu mpaka leo hamna kesi

NB: serikali pia ingejaribu kuwa inawapima na ustaarabu na hawa watu kabla ya kuwapa hzo kazi maana wengne kazi yao Ni kuwatiisha wenzao tu na kutoheshmu shuguli za wenzao hata Kama mtu anafanya kazi unayo ona wewe ya ajabu jua ndo analisha familia na kusaidia wazazi kifupi anategemewa hata Kama unamdharau
Pole mkuu kwa kadhia iliyokupata aisee, kuna watu wanalazimisha wenzao wawe wachawi tu
 
Kweli kabisa, wengine hata bar mkigombaniana demu ananza kauli zao, 'unanijua mi nani', nikujue iweje?
Mwaka Jana mwez Kama huu tareh za mwshoni nakumbuka Kama ilikuwa tarehe 19 hiv nilikuwa kwenye kampuni moja hivi siku moja Mara mkuu wa wilaya huyu hapa paaahh

Maswali na majibu yakaanza Mara vibali vya kampuni viko wapi mi nikamjibu kwakwel bosi hayupo labda tumpgie simu dada akawaka kwa kujimwambafy unajua Mimi ni Nani ni mwanamke huyo mkuu wa wilaya hyo si nikajikuta nmemjibu sitaki kujua hata we ni Nani?

Bhana bhana hata sjakaa sawa afisa usalama mmoja tayar kaniniga namimi si nikamniga kidogo kujibalance sasa nikamwambia Mimi hapa muajiriwa tu na wenye kampuni mda huu hawapo yule dada akatoa tamko nataka vibali haraka Basi nikamwambia ngoja nimpgie

Ile natoa simu tu ikaporwa duh sasa nikamwambia jaman dada mbona hvo yule Tena afsa usalama ananiulza unajua mimi ni Nani? Me si nikaropoka Elimu yako tafadhar mbona sio msitaarabu hapo nipo na Mdogo ake boss wote ni foreigners hawajamuulza Chochote wanakomaa na black mamba mwenzao Mimi sasa

Baada Kama ya nusu saa wakapga smu polis ocd akaja akatuchukua tukapelekwa polisi tukaa siku SKU kutoa dhamana hawataki kutupeleka mahakamani hawataki tukaweka wakili tukatoka siku ya nne Ila Cha ajabu mpaka leo hamna kesi

NB: serikali pia ingejaribu kuwa inawapima na ustaarabu na hawa watu kabla ya kuwapa hzo kazi maana wengne kazi yao Ni kuwatiisha wenzao tu na kutoheshmu shuguli za wenzao hata Kama mtu anafanya kazi unayo ona wewe ya ajabu jua ndo analisha familia na kusaidia wazazi kifupi anategemewa hata Kama unamdharau
 
kukagua tiketi, mida ya saa tatu usiku
Anakaguaje tiketi muda huo? Kama basi lilijaa siti level anasumbuaje abiria hata mimi ningegombana nae. Tiketi zinakaguliwa mara moja tu. au mlipanda yale mabasi yanapita chunya, makongorosi, Lupa, Kambi katoto, Rungwa, Itigi. Nk
 
Hahahahah mkuu Kama ulikuepo wakati huo nilitaman kumpgia sheihk wangu mmoja ili tumchinjie mbuzi makaburini usiku wa manane Ila baada ya kukaa ndani nikatoka hasira zmepungua Ila na Elimu pia znachangia kutojielewa kabsa.
Pole sana aisee, naelewa vile ulivyoghadhabika.
 
Anakaguaje tiketi muda huo?, kama basi lilijaa siti level anasumbuaje abiria hata mimi ningegombana nae. tiketi zinakaguliwa mara moja tu. au mlipanda yale mabasi yanapita chunya, makongorosi, Lupa, Kambi katoto, Rungwa, Itigi. Nk
Hapana mkuu, njia ya iringa, Dodoma, singida. Harafu jukumu lao la kukagua huwezi waingilia.
 
Back
Top Bottom