Hata kama nitabaki peke yangu, sitachoka: Naamini kuna siku nitafanikiwa

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Kuna wakati tulikuwa wengi, wengine wakabadilika, wengine wakachoka na wengine wakakata tamaa wakaacha.

Tulijenga hoja pamoja, tulijadili kwa hoja, tuliikosoa serikali na hata vyama vya siasa kwa hoja nzito na lugha za kistaarabu, tuliishauri serikali, tulishauri vyama vya siasa, tuliwashauri viongozi wetu kwa hoja zenye ushawoshi na kueleweka vyema.

Leo hii ukileta mada inayojadili hoja au ushauri kwa serikali, viongozi au vyama, utajikuta unachangia mwenyewe. Watu hawataki tena kuumiza vichwa vyao.

Binafsi bado naamini tutatoka hapa tulipo kwa kuibua mijadala inayofikirisha, kumshauri viongozi, serikali na vyama, na kwa kukosoa kwa njia ambayo ni constructive. Bado naamini, kupoteza muda kwenye kujadili matukio, kulumbana, kulaumiana na kukashifiana hakuwezi kutufikisha popote.

Kwa upande wangu nitaendelea kufanya mambo hata hata kama nitabaki peke yangu, naamini maadam naamini Niko sahihi na ninachohamasisha na kifanya ni kitu kizuri, IPO siku matunda yatapatikana, sitarudi nyuma nitasonga mbele kama so Leo nasi kesho, mabadiliko yataonekana. Kama nawe una imani juu ya jambo lolote zuri, lisimamie hata kama utabaki peke yako, IPO siku utafanikiwa.
 
The strongest man in the world is he, who stand alone. Sikumbuki nani alisema hili.
Kuna mambo mengine yanakatisha tamaa. Wakati mwingine MTU unajiuliza, kwa mini na we we usiache kutumia akili ukawa mpiga porojo maadamu chakula unapata na maisha yanaenda, lakini unakumbuka, hatukuumbwa wanadamu ili rule, wala utakapokufa hauwezi kuacha legacy kwamba eti ulikuwa unakula sana. Ni lazima kila MTU ajitahidi kwa uwezo wake kuhakikisha kuwa anatoa Nchango kamili wa kuifanya dunia kuwa sehemu bora zaidi ya kuishi kuliko alivyoikuta.
 
The strongest man in the world is he, who stand alone. Sikumbuki nani alisema hili.
Tusikubali kukatishwa tamaa na kitu chochote wala kurudishwa nyuma na MTU yeyote. Nguzo ya kufanikiwa ni kusonga mbele hata kama MTU unabaki peke yako
 
Kuna mambo mengine yanakatisha tamaa. Wakati mwingine MTU unajiuliza, kwa mini na we we usiache kutumia akili ukawa mpiga porojo maadamu chakula unapata na maisha yanaenda, lakini unakumbuka, hatukuumbwa wanadamu ili rule, wala utakapokufa hauwezi kuacha legacy kwamba eti ulikuwa unakula sana. Ni lazima kila MTU ajitahidi kwa uwezo wake kuhakikisha kuwa anatoa Nchango kamili wa kuifanya dunia kuwa sehemu bora zaidi ya kuishi kuliko alivyoikuta.
Nikuidhulumu nafsi kupiga porojo penye kuhitaji ukweli. Na mwisho wa siku wote tukipiga porojo tunaumiza kizazi tunachokitengeneza.
 
Nikuidhulumu nafsi kupiga porojo penye kuhitaji ukweli. Na mwisho wa siku wote tukipiga porojo tunaumiza kizazi tunachokitengeneza.
Kwa mfano viongozi wetu kuna vitu wanapatia na vingine wanakosema kama binadamu, ila nasi tunakuwa hatutimizi wajibu wetu, badala ya kutoa way forward ambayo ni constructive, tunalalamika na kulaumu tu. Au ushabiki bila initiation yoyote. Hii haifai na haiwezi kufaa hata siku moja.
 
Kwa mfano viongozi wetu kuna vitu wanapatia na vingine wanakosema kama binadamu, ila nasi tunakuwa hatutimizi wajibu wetu, badala ya kutoa way forward ambayo ni constructive, tunalalamika na kulaumu tu. Au ushabiki bila initiation yoyote. Hii haifai na haiwezi kufaa hata siku moja.
Kweli viongozi wetu wengi ni tia maji tia maji ukianza na mzee wa pumba jpm vipi ni kweli wajawazito hawatosoma tena....??
 
Kweli viongozi wetu wengi ni tia maji tia maji ukianza na mzee wa pumba jpm vipi ni kweli wajawazito hawatosoma tena....??
Sasa na sisi badala tushauri kwa kuchambua faida na hasara na mini kikiwaje kitaleta nini hivyo tufanyeje, tunabaki na kuripoti tu, kushabikia na matamko, tunakuwa hatujasaidia kitu bado
 
Mkuu binafsi yangu nitaikosoa serikali kwenye mambo ambayo inakosea tena nitaikosoa hadharani....bila kujali kitanikuta nini maana bora kufa kwa ninachokiamini kuliko kuishi nikiwa nimepiga magoti(kwa nisichokiamini)
 
Mkuu huu uzi ufanye kama ule wa Rutashubanyuma.
Jiongoleshe tu mwenyewe maana hamna namna tena.
 
Sasa na sisi badala tushauri kwa kuchambua faida na hasara na mini kikiwaje kitaleta nini hivyo tufanyeje, tunabaki na kuripoti tu, kushabikia na matamko, tunakuwa hatujasaidia kitu bado
Sasa unategemea kwa uongozi huu utamshauri nani na wakati kaisha sema hashauriki
 
Back
Top Bottom