Hata kama ningeichoka CCM lakini siyo kwa yule!

Gangongine

JF-Expert Member
Dec 31, 2015
3,854
1,776
CCM ni Chama Kikongwe na kimefanya mengi sana. Yapo mabaya kama ambavyo Chama chochote Duniani( ikiwamo CDM/UKAWA) kinaweza kufanya. Katika miaka ya karibuni kumekuwa na changamoto nyingi kwa vijana kama vile ukosefu wa Ajira, mitaji ya biashara, masoko ya bidhaa za wakulima, pembejeo n.k.

Uchumi wetu unapaswa kuimarishwa uweze kukabili changamoto za makundi yote ya Jamii na kukidhi matarajio ya walio wengi. Mabadiliko yanawezwa kufanywa na Chama Tawala au Chama cha Upinzani chenye nia na uwezo wa dhati wa kuleta mabadiliko ya kweli.mmm wale ndio walete mabadiliko???.....Yule ndiye alete mabadiliko??? Acheni kudanganywa kijinga!! Labda mabadiliko yake mwenyewe kwenye mfuko!

Kwa hali ilivyo na kwa aina ya Wagombea ambao Wapinzani wanatushawishi tuwachague, ni mzaha wa hali ya juu kutuaminisha kwamba wataleta mabadiliko kwa Waanchi badala ya mabadiliko yao binafsi. Na ndio maana watu hao wametumia miaka mingi kuwekeza Fedha kwa njia ya harambee na michango mbalimbali kwa jamii, kwa kuwa wana malengo yao binafsi. Hakuna mtu mjinga apoteze fedha nyingi kuusaka Uongozi wa Nchi halafu eti aje awatumikie Wananchi badala ya kurejesha hesabu zake. Ni aibu kwa kijana kutotambua hili huku akidai ni msomi wa Chuo Kikuu! Usomi wake unamsaidia nini kama anaweza kudanganywa kirahisi mpaka kiasi cha kudeki barabara!

Katika mazingira hayo nasema hata kama ningeichoka CCM namna gani, siwezi kudanganywa kijinga nichague Wagombea wa UKAWA waliopatikana kwa kuokotezwa kutoka kwenye watu waliokataliwa na CCM kutokana na historia yao. Ebu tujiulize kama kweli una lengo la kuleta mabadiliko ya kweli kwa nini ununue uongozi kwa gharama kubwa? Utarudishaje hizo Fedha wakati Ikulu hakuna biashara yoyote? SIDANGANYIKI! SIDANGANYIKI! SIDANGANYIKI!

Nitashawishika na upinzani pale watakapotuletea Sera Mbadala na watakapotuletea wagombea makini ambao kwa kuwaangalia kwa macho tu unaweza kuwa na chembe ya imani kuwa watatumikia Wananchi. Hawa wanaotumia Fedha nyingi kuwekeza kwenye Siasa ni watu wasiofaa na wenye malengo yasiyo na manufaa kwa Nchi yetu. Kama wana Fedha nyingi ni bora wajenge Viwanda, wawekeze kwenye Kilimo, wajenge Vyuo, Hospitali n.k ili watatue changamoto za Ajira, elimu, Afya n.k badala ya kutufanya wajinga kwa kutununua! CCM OYEE! HAPA KAZI TU!!
 
Hii nayo hoja ingawa ccm hiyo hiyo ndo iliwaandaa wawe mafisadi hadi kufikia eneo la kudai wakamatwe kama wao ni mafisadi ila ccm hiyo hiyo ikakataa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani na wengine bado wamepewa wadhifa bungeni huku wazalendo waliogawana fedha za escrow wameshindwa hata kuchangia madawati walau kumi kwenye shule zetu ambazo hazina.hata mashimo ya vyoo huku wakidai milioni kumi ni fedha za mboga kwao.
 
Lkn naona huna tofauti kwani uliye mchagua nae ni visasi tu , si ndie aliyeuza nyumba zetu kwa bei ya kutupwa hadi akawahonga mahawara zake na watoto wake?
Si ndiye huyu aliyenunua kivuko feki kwa mabilioni ambacho kimeshindwa kufanya kazi hadi Leo?
Si ndiye huyu aliyesimamia Barbara zetu za mabilioni lkn nyingi ni feki?
Sasa umechagua nini? Heri ungeniambia kuwa wewe ulimchagua yule ACT.
Lakini kwa huyu mzee ulibugi ila muda utasema
 
Lkn naona huna tofauti kwani uliye mchagua nae ni visasi tu , si ndie aliyeuza nyumba zetu kwa bei ya kutupwa hadi akawahonga mahawara zake na watoto wake?
Si ndiye huyu aliyenunua kivuko feki kwa mabilioni ambacho kimeshindwa kufanya kazi hadi Leo?
Si ndiye huyu aliyesimamia Barbara zetu za mabilioni lkn nyingi ni feki?
Sasa umechagua nini? Heri ungeniambia kuwa wewe ulimchagua yule ACT.
Lakini kwa huyu mzee ulibugi ila muda utasema
Hata baba yako anajua kwamba safari hii tumepata Rais makini na mahiri. Asante Mungu kwa kutokoa na janga la UKAWA na hila zao! Na watu wote waseme Ameeeeeeeeen !
 
Mtachagua kwa kura na kweli mtachagua, ila atakayetangazwa na tume kwa mujibu wa sheria ndiye mshindi. Vigezo na masharti kuzingatiwa!!!
 
Hata baba yako anajua kwamba safari hii tumepata Rais makini na mahiri. Asante Mungu kwa kutokoa na janga la UKAWA na hila zao! Na watu wote waseme Ameeeeeeeeen !
Du! Hata baba yako anajua tumepata Bomu kama unabisha waulize wana kagera.
 
CCM ni Chama Kikongwe na kimefanya mengi sana. Yapo mabaya kama ambavyo Chama chochote Duniani( ikiwamo CDM/UKAWA) kinaweza kufanya. Katika miaka ya karibuni kumekuwa na changamoto nyingi kwa vijana kama vile ukosefu wa Ajira, mitaji ya biashara, masoko ya bidhaa za wakulima, pembejeo n.k.

Uchumi wetu unapaswa kuimarishwa uweze kukabili changamoto za makundi yote ya Jamii na kukidhi matarajio ya walio wengi. Mabadiliko yanawezwa kufanywa na Chama Tawala au Chama cha Upinzani chenye nia na uwezo wa dhati wa kuleta mabadiliko ya kweli.mmm wale ndio walete mabadiliko???.....Yule ndiye alete mabadiliko??? Acheni kudanganywa kijinga!! Labda mabadiliko yake mwenyewe kwenye mfuko!

Kwa hali ilivyo na kwa aina ya Wagombea ambao Wapinzani wanatushawishi tuwachague, ni mzaha wa hali ya juu kutuaminisha kwamba wataleta mabadiliko kwa Waanchi badala ya mabadiliko yao binafsi. Na ndio maana watu hao wametumia miaka mingi kuwekeza Fedha kwa njia ya harambee na michango mbalimbali kwa jamii, kwa kuwa wana malengo yao binafsi. Hakuna mtu mjinga apoteze fedha nyingi kuusaka Uongozi wa Nchi halafu eti aje awatumikie Wananchi badala ya kurejesha hesabu zake. Ni aibu kwa kijana kutotambua hili huku akidai ni msomi wa Chuo Kikuu! Usomi wake unamsaidia nini kama anaweza kudanganywa kirahisi mpaka kiasi cha kudeki barabara!

Katika mazingira hayo nasema hata kama ningeichoka CCM namna gani, siwezi kudanganywa kijinga nichague Wagombea wa UKAWA waliopatikana kwa kuokotezwa kutoka kwenye watu waliokataliwa na CCM kutokana na historia yao. Ebu tujiulize kama kweli una lengo la kuleta mabadiliko ya kweli kwa nini ununue uongozi kwa gharama kubwa? Utarudishaje hizo Fedha wakati Ikulu hakuna biashara yoyote? SIDANGANYIKI! SIDANGANYIKI! SIDANGANYIKI!

Nitashawishika na upinzani pale watakapotuletea Sera Mbadala na watakapotuletea wagombea makini ambao kwa kuwaangalia kwa macho tu unaweza kuwa na chembe ya imani kuwa watatumikia Wananchi. Hawa wanaotumia Fedha nyingi kuwekeza kwenye Siasa ni watu wasiofaa na wenye malengo yasiyo na manufaa kwa Nchi yetu. Kama wana Fedha nyingi ni bora wajenge Viwanda, wawekeze kwenye Kilimo, wajenge Vyuo, Hospitali n.k ili watatue changamoto za Ajira, elimu, Afya n.k badala ya kutufanya wajinga kwa kutununua! CCM OYEE! HAPA KAZI TU!!

Hata kama ningeichoka CCM lakini siyo kwa yule!
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom