Hata kama ni kukusanya kodi kwa hili Serikali mmepotea

Jimmy George

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
1,733
1,643
Habari wana JF

Nasema humu JamiiForums naamini itawafikia wahusika maana humu kuna watu wa aina mbalimbali.

Kipindi hiki serikali inasisitiza wananchi kulipa kodi ya jengo pamoja na ardhi na kwa upande wa kodi ya majengo wametoa karatasi zinazoonyesha fedha unayotakiwa kulipa kutokana na tathimini wanazodai wamefanya kulingana na thamani ya nyumba yako. Tatizo lipo kwenye tathimini kwani thamani ya nyumba iliyoandikwa ni tofauti na uhalisia.

Hapa mtaani kwetu nyumba nyingi zinafanana kwa ukubwa wa viwanja na hata ujenzi wa nyumba yaani ramani lakini gharama zimekuja tofauti. Kuna jirani yangu nyumba yake ni ya kawaida lakini wanasema nyumba ina thamani ya milioni 128 hivyo kodi yake ni laki 1 na elfu 92 wakati nyumba ambayo inaendana na yake wanasema ina thamani ya milioni 12 na kodi yake ni elfu 18.

Mimi nawaomba wahusika wafanye tathimini upya kama kweli serikali inawajali wananchi wake wa hali ya chini maana kodi hizi zinatuumiza sana
 
Habari wana JF

Nasema humu JamiiForums naamini itawafikia wahusika maana humu kuna watu wa aina mbalimbali.

Kipindi hiki serikali inasisitiza wananchi kulipa kodi ya jengo pamoja na ardhi na kwa upande wa kodi ya majengo wametoa karatasi zinazoonyesha fedha unayotakiwa kulipa kutokana na tathimini wanazodai wamefanya kulingana na thamani ya nyumba yako. Tatizo lipo kwenye tathimini kwani thamani ya nyumba iliyoandikwa ni tofauti na uhalisia.

Hapa mtaani kwetu nyumba nyingi zinafanana kwa ukubwa wa viwanja na hata ujenzi wa nyumba yaani ramani lakini gharama zimekuja tofauti. Kuna jirani yangu nyumba yake ni ya kawaida lakini wanasema nyumba ina thamani ya milioni 128 hivyo kodi yake ni laki 1 na elfu 92 wakati nyumba ambayo inaendana na yake wanasema ina thamani ya milioni 12 na kodi yake ni elfu 18.

Mimi nawaomba wahusika wafanye tathimini upya kama kweli serikali inawajali wananchi wake wa hali ya chini maana kodi hizi zinatuumiza sana

Hiyo tathimini ya nyumba wanapiga wenyewe au wanashirikiana na mwenye nyumba?
 
Nimuda muafaka sasa kukaima nakuitikia kale kakiitikio ketu pendwa ka ule wimbo wetu maarufu ulio rindima miaka ya 2015 so tymeipenda wenyewe tuendelee tu maana hakuna namna
 
Wananchi hatukatai kulipa kodi ila zinapoletwa kodi za mwanaukome tunalipaje sasa. Wenzao wanakusanya kidogo kwa watu wengi na kupata pesa nyingi. Gharama za bandarini wanazihamishia kwenye majengo.
 
Mdau ungefafanua zaidi hizo nyumba ilituchambue vizuri yaani hizo nyumba zite zina vigae ,tiles,madirisha aluminium,vyumba vingapi,zina ukuta uliozunguka kiwanja,geti, nk.hebu tufahamishe ili wahusika waone
 
Mdau ungefafanua zaidi hizo nyumba ilituchambue vizuri yaani hizo nyumba zite zina vigae ,tiles,madirisha aluminium,vyumba vingapi,zina ukuta uliozunguka kiwanja,geti, nk.hebu tufahamishe ili wahusika waone
Nyumba hizi za hapa kwetu zina wastani wa vyumba vinne mpaka sita hakuna vigae,mageti ya kuweza kulaza magari,madirisha na milango ya kawaida na kuta zake ni fupi ambazo huwa zinatenganisha nyumba na nyumba tu....
 
Back
Top Bottom