Uchaguzi 2020 Hata kama ndio demokrasia, Ubunge umerahisishwa sana mwaka huu wa Uchaguzi

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
714
1,137
Tayari vyama vingi kama si vyote vimefungua pazia kwa watia nia kuelekea ucjaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Kumekuwa na pilikapilika za huku na kule kwa wanachama wa vyama vya siasa kutia nia ya kugombea ubunge.

Kwenye makundi sogozi kwa sasa kumejaa picha za watia nia wakijitangaza kuwa wako tayari kuwatumikia wananchi.
Cha kushangaza ni kuwa hata wasiotarajiwa kuwa wangeweza kutia nia sasa wefanya hivyo.

Wengine tunawajua uwezo wao wa kiuongozi na kiutendaji kwani tumesoma nao shuleni na vyuoni.

Ni watu ambao hata uwezo wa kujijitea wao wenyewe hawana mpaka watetewe na wenzao. Sasa mtu ambae hawezi kujisemea na kujitetea mwenyewe atamtetea nani?

Ubunge umerahosishwa sana kiasi kwamba kila mmoja anaona kama anatosha kuwa mwakilishi jimboni.

Itafika hatua huko mbele tunaweza kuwa na wabunge wasiojiweza kiasi kwamba mbunge akamaliza miaka mitano bila kuchangia chochote bungeni.

Ni wakati wa chama kuweka vigezo muhimu na vigumu kwa watia nia ili kuwa na uhakika na na hao watia nia ambao ni wabunge watarajiwa.
 
Kama kuna kitu ningetamani kifutwe ndani ya katiba yetu ni bunge.

Hili ni dubwana linalogharimu gharama ya kufuru ya kodi yetu bila msaada kwa walipa kodi.

Baada ya kupigania vyama vyao na kugeuka kuwa wawakilishi wa vyama na sii wa wananchi halina tena maana yeyote kuitwa bunge la Wananchi.
 
Watu wameamua kutumia Umaarufu wao Kujipitisha kwenye Ubunge. Sidhani kama Wataweza kuisimamia Serikali, lakini afadhali wengi bado wanatoka kwenye chama cha ndiyoooo. Upinzani ndiyo watazidi kupata nguvu sababu ya Ujengaji wa hoja Bungeni.
 
Wameona bunge lililopita lilivyokuwa genge la kusifu na mipasho. Kwa hiyo hakuna haja ya kutumia akili. Kila hoja iliyoletwa na serikali ikiwemo miswada ya sheria mbovu (ikiwa pamoja na kinga za viongozi kutoshitakiwa) wao ni poa tu. Nchi ya ajabu sana hii!
 
Watu wameamua kutumia Umaarufu wao Kujipitisha kwenye Ubunge,Sidhani kama Wataweza kuisimamia Serikali,Lakini afadhali wengi bado wanatoka kwenye chama cha ndiyoooo..Upinzani ndiyo watazidi kupata nguvu sababu ya Ujengaji wa hoja Bungeni
Kwa Tume hii ya uchaguzi; hakuna mpizani makini atayepata ubunge. Hapa hakuna uchaguzi. Tume itatangaza wabunge inaowataka. Wengi (99%) wa CCM na wapinzani dhaifu na kiduchu ili kujionyesha kuwa demokrasia imetendeka.
 
Kugonga meza tu kama wafanyavyo wabunge wa CCMkuna ugumu gani?
Kama hivi nani anashindwa kusema ndiyooooooo
IMG-20191111-WA0001.jpg
 
Kama kuna kitu ningetamani kifutwe ndani ya katiba yetu ni bunge.

Hili ni dubwana linalogharimu gharama ya kufuru ya kodi yetu bila msaada kwa walipa kodi.

Baada ya kupigania vyama vyao na kugeuka kuwa wawakilishi wa vyama na sii wa wananchi halina tena maana yeyote kuitwa bunge la Wananchi.
Wanaogonga meza hovyo ni wabunge wa CCM ila Cha kushangaza unataka bunge zima la wabunge mpaka wa vyama vingine lifutwe
 
wabunge wetu hawa ndio wanaowakilisha watanzania wote, yaani kwamba, tabia, mienendo na mitazamo yao ndio namna watanzania walivyo, hatutoboi leo.
 
Tayari vyama vingi kama si vyote vimefungua pazia kwa watia nia kuelekea ucjaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Kumekuwa na pilikapilika za huku na kule kwa wanachama wa vyama vya siasa kutia nia ya kugombea ubunge.

Kwenye makundi sogozi kwa sasa kumejaa picha za watia nia wakijitangaza kuwa wako tayari kuwatumikia wananchi.
Cha kushangaza ni kuwa hata wasiotarajiwa kuwa wangeweza kutia nia sasa wefanya hivyo.

Wengine tunawajua uwezo wao wa kiuongozi na kiutendaji kwani tumesoma nao shuleni na vyuoni.

Ni watu ambao hata uwezo wa kujijitea wao wenyewe hawana mpaka watetewe na wenzao. Sasa mtu ambae hawezi kujisemea na kujitetea mwenyewe atamtetea nani?

Ubunge umerahosishwa sana kiasi kwamba kila mmoja anaona kama anatosha kuwa mwakilishi jimboni.

Itafika hatua huko mbele tunaweza kuwa na wabunge wasiojiweza kiasi kwamba mbunge akamaliza miaka mitano bila kuchangia chochote bungeni.

Ni wakati wa chama kuweka vigezo muhimu na vigumu kwa watia nia ili kuwa na uhakika na na hao watia nia ambao ni wabunge watarajiwa.
Kichefuchefu sana
 
Tayari vyama vingi kama si vyote vimefungua pazia kwa watia nia kuelekea ucjaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Kumekuwa na pilikapilika za huku na kule kwa wanachama wa vyama vya siasa kutia nia ya kugombea ubunge.

Kwenye makundi sogozi kwa sasa kumejaa picha za watia nia wakijitangaza kuwa wako tayari kuwatumikia wananchi.
Cha kushangaza ni kuwa hata wasiotarajiwa kuwa wangeweza kutia nia sasa wefanya hivyo.

Wengine tunawajua uwezo wao wa kiuongozi na kiutendaji kwani tumesoma nao shuleni na vyuoni.

Ni watu ambao hata uwezo wa kujijitea wao wenyewe hawana mpaka watetewe na wenzao. Sasa mtu ambae hawezi kujisemea na kujitetea mwenyewe atamtetea nani?

Ubunge umerahosishwa sana kiasi kwamba kila mmoja anaona kama anatosha kuwa mwakilishi jimboni.

Itafika hatua huko mbele tunaweza kuwa na wabunge wasiojiweza kiasi kwamba mbunge akamaliza miaka mitano bila kuchangia chochote bungeni.

Ni wakati wa chama kuweka vigezo muhimu na vigumu kwa watia nia ili kuwa na uhakika na na hao watia nia ambao ni wabunge watarajiwa.
Sababu imejulikana qualification nikumsifu mtawala baaasi
 
Back
Top Bottom