Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,407
- 31,392
Kuna makosa makubwa sana wanayofanya CCM na hili unalozungumza hapa ni mojawapo.Hivi wananchi waichague chadema kwa lipi hasa? kile chama kinasubiri kuzikwa tu October 2020
Chadema au ACT ni maandishi yanayowakilisha makundi yenye mtazamo au itikadi tofauti
Ukifuta Chadema au ACT hujafanikiwa kufuta kile kinachowasukuma watu kuunga mkono hivyo vyama
CCM ipo madarakani miaka 50 na ushee, miaka 5 watu wameelezwa ''mafanikio na maajbu'' ya sera za CCM
Pamoja na yote hayo, CCM bado inategemea vyombo na taasisi za umma kupata ushindi na hata wakati mwingine kutumia wizi kama ule wa Kinondoni ambako sanduku lilichukuliwa na kurudishwa kituoni na kupokelewa na NEC wakisihirikiana na Polisi.
Hii maana yake ni moja, kwamba, kuna kitu ambacho sehemu ya jamii haikubaliani naCCM, kuzika vyama hakuondoi ile imani ya something is wrong. Usiangalie majina ya vyama , jiulize vinaungwaje mkono?
Kwanini CCM yenye ushahidi wa kutawala na maendeleo bado inakabiliwa na wakati mgumu?
CCM kwa kushirikiana na '' Msioajili wa vyama' waliifuta CUF, je, wamewafuta wanachama?
Hao wa ACT ni akina nani?
jmushi1