Hata CCM hakina sera kisingekuwa kinagomea au kuvuruga matokeo au kukimbilia mahakamani

mwembemdogo

JF-Expert Member
Feb 28, 2016
2,282
1,251
Nimeshangazwa Na mdau mmoja aliyevibeza vyama vya Upinzani eti vina zaidi ya miaka 24 toka kuanzishwa Kwa mfumo wa vyama vingi nchini.

Nilitegemea mtoa mada angevisifia vyama vya upinzani Kwa mabadiliko makubwa waliyoyafanya ktk nchi Yetu licha ya vikwazo mbalimbali vinavyofanywa Na CCM kupitia serikali yake.Niliamini CCM pamoja Na umri wake tuanzie tu 1977 kina miaka 39 kingekuwa kimejijenga Kwa wananchi kisera kiasi cha wananchi kutokihama Na kujiunga Na vyama vya upinzani lakini imekuwa kinyume chake Kwa sasa wapinzani wana idadi kubwa ya wafuasi licha ya vikwazo wanavyopata kutoka kwenye vyombo vya dola.

Tumeshudia uchaguzi wa mwaka 2015 jinsi ulivyofanyika , uhesabuji kura , utangazwaji matokeo Na jinsi wananchi walivyokuwa Na hamasa Kwa vyama vya upinzani mpaka kupelekea CCM kusafirisha wananchi kuhudhuria mikutano yake .CCM kutokana Na wananchi kujaa Kwa wingi kwenye mikutano ya upinzani ilidiriki kusema eti wanapewa fedha ilichekesha.Wabunge wa upinzani wenyeviti wa mitaa Na madiwani wa upinzani wameongezeka.

Hitimisho niliamini CCM Kwa ukongwe wake wa kidemokrasia kingekuwa mfano wa kuigwa Kwa kutokugomea matokeo kama kilivyofanya Uchaguzi wa Zanzibar , Kukimbilia Mahakamani kuweka mazuio ya Umeya wa Dar, kulazimisha kushinda Na kubatilisha matokeo ya chaguzi kama za meya ya Tanga vitendo hivyo vinadhihirisha kuwa CCM hakina tofauti Na vyama vya Upinzani .CCM ingekuwa Na Sera nzuri sidhani kama kingekuwa kinateseka kupata ushindi katika chaguzi.

Upinzani unazidi kuimarika licha ya mazingira magumu kama ya Tume ya Uchaguzi kutokuwa HURU.
 
Back
Top Bottom