Huyo punga amesemaje? Punga la lumumba lililojificha kwenye utangazaji.“ Tuacheni Unafiki Kujifanya tunasikitika na tunaona Huruma Kuugua kwa Tundu Lissu huku tukijua kabisa kuwa Wananchi wake ambao wanahitaji Huduma yake kama Mbunge kwa muda mrefu hawawakilishwi hivyo Wao ndiyo wanaathirika zaidi kuliko Yeye Mmoja tu “
Huyu ndiye Mtangazaji na Mtu aliyejipachika Cheo cha kuwa Mchambuzi na Muuliza Maswali bora na yaliyoenda Kidato ( Shule ) wa Nyanja zote katika Chombo chake cha CMG hasa akiwa pale Clouds 360 akijulikana kama Hassan Ngoma a.k.a Mr. Tanzanite.
Haya nadhani sasa wale ambao ni Watetezi wakuu wa Tundu Lissu mmemsikia Kipanga wa CMG Mtangazaji Hassan Ngoma na Yeye Msimamo wake ameuweka wazi tu kuwa anadhani Wananchi wa Jimbo la Tundu Lissu ndiyo wanatakiwa waonewe Huruma sana kuliko Yeye Mtu Mmoja tu Tundu Lissu na anadhani ilitakiwa mapema mno kama Tundu Lissu alishaona kuwa hatokuwepo Jimboni Kwake kwa muda mrefu basi angeliachia tu hilo Jimbo ili kuwapisha wengine waweze Kuwawakilisha Wananchi wa hilo Jimbo.