GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,516
- 108,791
GSM binafsi tena hapa hapa JamiiForums nakumbuka nilianzisha Uzi Kuwaonya kuhusu Kumleta Yanga SC Haji Manara nikawaambia kuwa mmeandaa Bomu ambalo litakuja Kulipuka na Kuwagharimu Yanga SC na sasa yametimia.
Kamarada (Comrade) wangu (Kitasnia) Msomi Mwerevu Hassan Bumbuli nawe nilikuonya hapa hapa JamiiForums kuwa kutokana na ule ujio wa Haji Manara hapo Yanga SC kwa Uweledi wako na Hadhi yako ungeachana tu na Yanga SC na urejee zako MWANANCHI ( MCL ) hasa katika Gazeti lako la Mwanaspoti lakini ukanipuuza na sasa yametimia kwani nilichokitabiri Kwenu kimetimia.
Hopeless ( Mpuuzi ) Haji Manara wala sitopoteza muda mwingi nawe kwani nawe nilikuonya na Kukuambia kuwa Kitendo chako cha Kuwashambulia (tena personally kabisa) akina Mohammed Dewji (Mwekezaji Simba SC) na Barbara Gonzalez (CEO Simba SC) halafu Wao wanakunyamazia ni Ishara tosha ya Laana Kubwa na Mbaya itakayokutafuna na sasa nilichokitabiri Kimetimia.
Kamarada (Comrade) Hassan Bumbuli hivi unajisikiaje Nwenzako Haji Manara Kununuliwa Gari jipya aina ya PRADO, kuhamishwa kutoka Mikocheni alikokuwa akiishi mwanzo na sasa akipangiwa Nyumba Slip Way Masaki na akikuzidi Mshahara mara 15 wakati Kazi Kubwa na Nyingi za Yanga SC (hasa zile za Kiutendaji) zinafanywa na Wewe tu?
Huenda pia (Kamarada Hassan Bumbuli) ile laana ya Kumtukana vibaya Mtendaji Mwenzako (aliyekuwa Mhamasishaji) wa Yanga SC Antonio Nugaz ikawa inaanza Kukutafuna na Kukuumiza kwani kiukweli hukupaswa Kumtusi vile na nakumbuka pamoja na Kumtukana kote kule (Nugaz) bado alikuomba Radhi yaishe ukakataa na mwishowe akasema anamuachia Mwenyezi Mungu na sasa Mola/ Maulana nae ameanza Kumjibia.
Hata hivyo Kamarada (Comrade) Hassan Bumbuli nikushukuru tu kwa zile Video Mbili ulizomtumia (mpostia) Hajj Manara akiwa Dubai (Uarabuni) Kwao na Gharib Said Mohammed (GSM) huku Kaka yake 'akiupiga mwingi' kwa Manara wakiwa Wamesimama katika Hafla ya Kifamilia na ile ya Juzi kule Kisiwani Zanzibar aliyokuwa akimlazimisha Kumvuta karibu Injinia Hersi Said na Injinia akawa anakataa hali iliyopelekea jana katika Mchezo wenu dhidi ya Azam FC Injinia Hersi amkimbie na amkwepe Manara kwa Kukaa nae karibu.
Niliwahi kuwaambieni wana Yanga SC (wa hapa Jamvini JamiiForums) kuwa kama kuna Kazi rahisi na nyepesi Kwangu basi huwa ni kupata Habari Ngumu na zilizojificha kabisa za Kuihusu Yanga SC kama Timu, Wachezaji wake na mpaka Watendaji wake kwani huko nina Watu wengi wengi 'very Loyal' Kwangu na huwa hawanifichi Jambo lenu kama hili la Leo na yaliyopita.
Najua Kesho au Keshokutwa au huko mbeleni mtajitahidi Kukanusha hili ila nami GENTAMYCINE nawaambia kuwa nina 'Skendo' yenu nyingine ila kwa sasa naiweka (nawaweka) Kiporo nasubiri ama Mfungwe au Mtoke Sare na Coastal Union FC Jumapili hii (ijayo) kule Mkoani Tanga ili mkianza Kuvurugana (Kugombana) tu basi nami nikoleze Moto wangu kwa Kuiweka hadharani kwani 'Unyama Unyaman' kwa sasa.
Kamarada (Comrade) wangu (Kitasnia) Msomi Mwerevu Hassan Bumbuli nawe nilikuonya hapa hapa JamiiForums kuwa kutokana na ule ujio wa Haji Manara hapo Yanga SC kwa Uweledi wako na Hadhi yako ungeachana tu na Yanga SC na urejee zako MWANANCHI ( MCL ) hasa katika Gazeti lako la Mwanaspoti lakini ukanipuuza na sasa yametimia kwani nilichokitabiri Kwenu kimetimia.
Hopeless ( Mpuuzi ) Haji Manara wala sitopoteza muda mwingi nawe kwani nawe nilikuonya na Kukuambia kuwa Kitendo chako cha Kuwashambulia (tena personally kabisa) akina Mohammed Dewji (Mwekezaji Simba SC) na Barbara Gonzalez (CEO Simba SC) halafu Wao wanakunyamazia ni Ishara tosha ya Laana Kubwa na Mbaya itakayokutafuna na sasa nilichokitabiri Kimetimia.
Kamarada (Comrade) Hassan Bumbuli hivi unajisikiaje Nwenzako Haji Manara Kununuliwa Gari jipya aina ya PRADO, kuhamishwa kutoka Mikocheni alikokuwa akiishi mwanzo na sasa akipangiwa Nyumba Slip Way Masaki na akikuzidi Mshahara mara 15 wakati Kazi Kubwa na Nyingi za Yanga SC (hasa zile za Kiutendaji) zinafanywa na Wewe tu?
Huenda pia (Kamarada Hassan Bumbuli) ile laana ya Kumtukana vibaya Mtendaji Mwenzako (aliyekuwa Mhamasishaji) wa Yanga SC Antonio Nugaz ikawa inaanza Kukutafuna na Kukuumiza kwani kiukweli hukupaswa Kumtusi vile na nakumbuka pamoja na Kumtukana kote kule (Nugaz) bado alikuomba Radhi yaishe ukakataa na mwishowe akasema anamuachia Mwenyezi Mungu na sasa Mola/ Maulana nae ameanza Kumjibia.
Hata hivyo Kamarada (Comrade) Hassan Bumbuli nikushukuru tu kwa zile Video Mbili ulizomtumia (mpostia) Hajj Manara akiwa Dubai (Uarabuni) Kwao na Gharib Said Mohammed (GSM) huku Kaka yake 'akiupiga mwingi' kwa Manara wakiwa Wamesimama katika Hafla ya Kifamilia na ile ya Juzi kule Kisiwani Zanzibar aliyokuwa akimlazimisha Kumvuta karibu Injinia Hersi Said na Injinia akawa anakataa hali iliyopelekea jana katika Mchezo wenu dhidi ya Azam FC Injinia Hersi amkimbie na amkwepe Manara kwa Kukaa nae karibu.
Niliwahi kuwaambieni wana Yanga SC (wa hapa Jamvini JamiiForums) kuwa kama kuna Kazi rahisi na nyepesi Kwangu basi huwa ni kupata Habari Ngumu na zilizojificha kabisa za Kuihusu Yanga SC kama Timu, Wachezaji wake na mpaka Watendaji wake kwani huko nina Watu wengi wengi 'very Loyal' Kwangu na huwa hawanifichi Jambo lenu kama hili la Leo na yaliyopita.
Najua Kesho au Keshokutwa au huko mbeleni mtajitahidi Kukanusha hili ila nami GENTAMYCINE nawaambia kuwa nina 'Skendo' yenu nyingine ila kwa sasa naiweka (nawaweka) Kiporo nasubiri ama Mfungwe au Mtoke Sare na Coastal Union FC Jumapili hii (ijayo) kule Mkoani Tanga ili mkianza Kuvurugana (Kugombana) tu basi nami nikoleze Moto wangu kwa Kuiweka hadharani kwani 'Unyama Unyaman' kwa sasa.