akilimtindi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 421
- 83
Nahisi hasira za Wadanganyika hazijatosha kabisa, nilihisi zimefikia kiasi cha kufanya jambo lakini kwa hili nimegundua bado kabisa. Nasema hivi kwasababu sikutegemea kabisa kwa ufuska wote huu uliofanywa na Serikali hii kwa rasilimali za Taifa hili na uliosemwa wazi na wabunge JK akalikalia kimya na wananchi wakanyamaza na kubaki tu wakinong'ona huku chini chini tena kwa woga ule wa mwaka 1947.
Kwa uelewa wangu mwepesi kwenye mambo ya siasa nilitegemea mambo kadhaa, kwanza nilitegemea kabisa kwamba kwa hili lazima JK atafanya jambo la kuonyesha kujibu tuhuma nzito zilizotupiwa serikali yake aidha kwa kuwashauri mawaziri wake wajiuzulu kupunguza munkari wa jamii ya Watanzania kwa ujumla wake, au nilitegemea basi bunge lingeonyesha dalili ya kufanyia kazi hoja iliyotarajiwa kupelekwa mezani kwa Spika tangu wiki iliyopita. Lakini ajabu kubwa ni kwamba bunge limeyeyusha na JK katoa msemo ambao kiukweli sijaamini kwamba kautoa yeye au kasingiziwa, eti kasema huo ni "upepo na utapita tuu.." hii ni dharau kubwa kuliko ninazozijua kwakuwa hii imetoka na kusikika, inamaanisha mnajisumbua na hamuwezi kufanya chochote.
Kikubwa kuliko vyote kilichonifanya nione kwamba hasira zetu bado kabisa ni kitendo cha Wadanganyika kukaa kimya pamoja na matusi hayo kutoka kwa JK, ni ajabu kubwa mno hiyo. Niliamini kabisa kwamba kwa misemo hii kutoka kwa JK wakati huu basi ilikuwa imefika wakati Wadanganyika watoke na kudai wanachokitaka maana kiko wazi tayari. Kwani kulikuwa na ugumu gani leo watu wote wakasema hawaendi popote hadi mawaziri watoke, ama hadi bunge liongeze siku na kuamua kumtwangia PM kura ya kutokumwamini? Kama hasira zimetosha basi nahisi kilichobaki ni mobilization, kimsingi tutakuwa resources tunazo kwa maana ya watu na hasira zao. Kinachotakiwa ni kuelekeza hizo resources kwenye kazi fulani kwa manufaa ya Taifa hili.
Something has to be immediately, we have to hit the iron while it's still Hot otherwise JK atathibitisha alilolisema "huu ni upepo na utapita.." We have to instead prove what Sugu said, .."hii ni dhoruba na haitapita hivi hivi, lazima iondoke na sehemu legelege kama sehemu yote".
I'm not suggesting a strike as far as no mobilization for that at the moment, nashauri ingewezekana kesho wote tutulie walau kwa kesho tu tusifanye chochote tuone JK atasema nini kuhusu sisi Wadanganyika kukaa tu kimya maana itambidi kuongea. Kama kuna mwenye plan mbadala tujadiliane, tupate mawazo kutoka pande zote maana hata CCM hili linawakera waziwazi.
Kwa uelewa wangu mwepesi kwenye mambo ya siasa nilitegemea mambo kadhaa, kwanza nilitegemea kabisa kwamba kwa hili lazima JK atafanya jambo la kuonyesha kujibu tuhuma nzito zilizotupiwa serikali yake aidha kwa kuwashauri mawaziri wake wajiuzulu kupunguza munkari wa jamii ya Watanzania kwa ujumla wake, au nilitegemea basi bunge lingeonyesha dalili ya kufanyia kazi hoja iliyotarajiwa kupelekwa mezani kwa Spika tangu wiki iliyopita. Lakini ajabu kubwa ni kwamba bunge limeyeyusha na JK katoa msemo ambao kiukweli sijaamini kwamba kautoa yeye au kasingiziwa, eti kasema huo ni "upepo na utapita tuu.." hii ni dharau kubwa kuliko ninazozijua kwakuwa hii imetoka na kusikika, inamaanisha mnajisumbua na hamuwezi kufanya chochote.
Kikubwa kuliko vyote kilichonifanya nione kwamba hasira zetu bado kabisa ni kitendo cha Wadanganyika kukaa kimya pamoja na matusi hayo kutoka kwa JK, ni ajabu kubwa mno hiyo. Niliamini kabisa kwamba kwa misemo hii kutoka kwa JK wakati huu basi ilikuwa imefika wakati Wadanganyika watoke na kudai wanachokitaka maana kiko wazi tayari. Kwani kulikuwa na ugumu gani leo watu wote wakasema hawaendi popote hadi mawaziri watoke, ama hadi bunge liongeze siku na kuamua kumtwangia PM kura ya kutokumwamini? Kama hasira zimetosha basi nahisi kilichobaki ni mobilization, kimsingi tutakuwa resources tunazo kwa maana ya watu na hasira zao. Kinachotakiwa ni kuelekeza hizo resources kwenye kazi fulani kwa manufaa ya Taifa hili.
Something has to be immediately, we have to hit the iron while it's still Hot otherwise JK atathibitisha alilolisema "huu ni upepo na utapita.." We have to instead prove what Sugu said, .."hii ni dhoruba na haitapita hivi hivi, lazima iondoke na sehemu legelege kama sehemu yote".
I'm not suggesting a strike as far as no mobilization for that at the moment, nashauri ingewezekana kesho wote tutulie walau kwa kesho tu tusifanye chochote tuone JK atasema nini kuhusu sisi Wadanganyika kukaa tu kimya maana itambidi kuongea. Kama kuna mwenye plan mbadala tujadiliane, tupate mawazo kutoka pande zote maana hata CCM hili linawakera waziwazi.