Hashpuppi, tapeli wa Nigeria akiri makosa ya utakatishaji fedha

Sam Gidori

Senior Member
Sep 7, 2020
165
414
Raia wa Nigeria, Ramon Abbas, maarufu kwa jina la Hashpuppi amekiri makosa ya utakatishaji fedha katika mahakama nchini Marekani.

Hashpuppi, aliyejipatia umaarufu kwa maisha yake ya anasa mitandaoni, ambapo ana wafuazi zaidi ya milioni 2.5 katika mtandao wa Instagram, amekiri makosa ya utapeli unaofikia jumla ya dola milioni 24 za Marekani (sawa na zaidi ya Tsh. bilioni 55).

Nyaraka za mahakama zilizowekwa wazi zinaonesha katika tukio moja, Hashpuppi alijaribu kumtapeli dola milioni 1 za Marekani (zaidi ya Tsh. bilioni 2.3) mtu mmoja aliyetaka kufadhili shule moja ya watoto nchini Qatar baada ya kujifanya benki kwa kuonesha nyaraka feki na kutengeneza tovuti feki.

Hashpuppi anatajwa kuwa mmoja wa matapeli wakubwa zaidi wa mtandaoni duniani. Umaarufu wake na wezo wake wa kutengeneza mtandao kumemwezesha kufanikisha matukio makubwa ya utapeli kwa ufanisi mkubwa.

Tapeli huyo alikamatwa mwezi Juni akiwa nchini Dubai, anaweza kukabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 jela na atapaswa kulipa fidia kamili kwa wahanga.

 
Raia wa Nigeria, Ramon Abbas, maarufu kwa jina la Hashpuppi amekiri makosa ya utakatishaji fedha katika mahakama nchini Marekani.

Hashpuppi, aliyejipatia umaarufu kwa maisha yake ya anasa mitandaoni, ambapo ana wafuazi zaidi ya milioni 2.5 katika mtandao wa Instagram, amekiri makosa ya utapeli unaofikia jumla ya dola milioni 24 za Marekani (sawa na zaidi ya Tsh. bilioni 55).

Nyaraka za mahakama zilizowekwa wazi zinaonesha katika tukio moja, Hashpuppi alijaribu kumtapeli dola milioni 1 za Marekani (zaidi ya Tsh. bilioni 2.3) mtu mmoja aliyetaka kufadhili shule moja ya watoto nchini Qatar baada ya kujifanya benki kwa kuonesha nyaraka feki na kutengeneza tovuti feki.

Hashpuppi anatajwa kuwa mmoja wa matapeli wakubwa zaidi wa mtandaoni duniani. Umaarufu wake na wezo wake wa kutengeneza mtandao kumemwezesha kufanikisha matukio makubwa ya utapeli kwa ufanisi mkubwa.

Tapeli huyo alikamatwa mwezi Juni akiwa nchini Dubai, anaweza kukabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 jela na atapaswa kulipa fidia kamili kwa wahanga.

Wanaija ni next level kwenye hizi ishu.. Dunia inawajua vema

 
Anawatapeli watu halafu ana post kwenye social media magari mazuri anayoyamiliki na Mali zake. Shenzi sana! Waafrika ifike mahali tuchukie njia za mkato ili kupata mafanikio. Unapost gari za mabilioni ya hela huku huna hata kiwanda Wala kampuni ya kuzalisha. Unawaza nini? Mfano upi unaotaka kizazi kijacho kiige toka kwako? Au unajifikiria wewe tu na tumbo lako? We should live to create a positive impact, but not to receive praises from people. Because at the end of it, it's all vanity.
 
shida bhana wizi na utapeli ni kama kazi au ajira ya kudumu,huwezi kusema ufanye mara moja utusue uache ufanye shughuli za kawaida,ni lazima tuu utataka kuendelea!na bora angekuwa anatapeli noti za kiafrika za hao jamaa ni 🔥🔥🔥
 
Nashangaaga sana Mtu ni drug dealer au tapeli alafu unaonesha mtandaoni una maisha mazuri kweli???? serikali sio falaa kiasi hichoo kuna ile familia ilifungwa Maisha kisa ujinga huo huoo...
 
Nashangaaga sana Mtu ni drug dealer au tapeli alafu unaonesha mtandaoni una maisha mazuri kweli???? serikali sio falaa kiasi hichoo kuna ile familia ilifungwa Maisha kisa ujinga huo huoo...
Hahaha mkuu ile familia ya kitajiri ilikula nyundo mzito sana hizi mambo za kujishaua na pesa chafu kwene mitandao ya kijamii sio kabisa
 
Hushpuppi kakamatwa kijinga sana kwa sababu ya hashuo za kujionesha birthday mitandaoni.

Wamarekani walikuwa wanam suspect lakini walikuwa hawana ushahidi.

Alivyosherehekea birthday yake ya kweli Instagram, wakaangalia data zake alizoombea visa kwenda Marekani wakaona tarehe ni ile ile.

Wakamfuatilia mpaka kumdaka.

Kupiga hela kwake kukawa rahisi kuliko kujizuia kujionesha online.

Alijisahau akajiona hakamatiki.

Ndiyo maana kuna ma Mafia wana kanuni za kutojionesha. Wanafanya zali halafu wanaishi simple. Hawana social media wala kujionesha.

Tatizo, mtu anayeiba ili ajioneshe, akifanikiwa kuiba, halafu asiweze kujionesha, anajiona hajafanikiwa kufikisha alichotaka.
 
Raia wa Nigeria, Ramon Abbas, maarufu kwa jina la Hashpuppi amekiri makosa ya utakatishaji fedha katika mahakama nchini Marekani.

Hashpuppi, aliyejipatia umaarufu kwa maisha yake ya anasa mitandaoni, ambapo ana wafuazi zaidi ya milioni 2.5 katika mtandao wa Instagram, amekiri makosa ya utapeli unaofikia jumla ya dola milioni 24 za Marekani (sawa na zaidi ya Tsh. bilioni 55).

Nyaraka za mahakama zilizowekwa wazi zinaonesha katika tukio moja, Hashpuppi alijaribu kumtapeli dola milioni 1 za Marekani (zaidi ya Tsh. bilioni 2.3) mtu mmoja aliyetaka kufadhili shule moja ya watoto nchini Qatar baada ya kujifanya benki kwa kuonesha nyaraka feki na kutengeneza tovuti feki.

Hashpuppi anatajwa kuwa mmoja wa matapeli wakubwa zaidi wa mtandaoni duniani. Umaarufu wake na wezo wake wa kutengeneza mtandao kumemwezesha kufanikisha matukio makubwa ya utapeli kwa ufanisi mkubwa.

Tapeli huyo alikamatwa mwezi Juni akiwa nchini Dubai, anaweza kukabiliwa na kifungo cha hadi miaka 20 jela na atapaswa kulipa fidia kamili kwa wahanga.


DIAMOND PLATINUMZ siku yakimkuta ya kumkuta, sijui watetezi wake watsemaje?
tumuombe SSH ana kazi kubwa kupambana na haya magenge yaliyolindwa awamu ilee.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom