Hashimu Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee CHADEMA(BAZECHA) afutiwa mashtaka na DPP

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,498
9,279
1645605727461.png

Picha: Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema, Hashimu Juma
Mkurugenzi wa Mashitaka nchini Tanzania (DPP), Sylvester Mwakitalu leo amemuomdolea mashitaka ya uchochezi yaliyokuwa yanamkabili Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema, Hashimu Juma, kupitia kifungu cha 90 (1), katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es salaam.

Tarehe 07 OKtoba 2021, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chadema (Bazecha) Hashimu Juma Issa (63) alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka mawili, likiwemo la kuchapisha taarifa za uongo na kuzisambaza kwenye mtandao wa YouTube.

Mshtakiwa huyo alifikishwa Mahakamani hapo Alhamisi Oktoba 7, 2021 na kusomewa mashitaka hayo na Wakili wa Serikali Yusuph Abood mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu.

Wakili Abood alidai mahakamani kuwa Oktoba Mosi katika eneo la Kinondoni B, mtaa wa Ufipa, mshtakiwa alisambaza taarifa kwa lengo la kumchafua na kumdhalilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro.

Alidai kuwa mshtakiwa alichapisha kwenye kompyuta na kusambaza taarifa kuwa "Sirro ni gaidi namba moja nchini Tanzania na fisadi."

Ilidaiwa katika shitaka lingine kuwa Oktoba Mosi katika eneo la Kinondoni B, mtaa wa Ufipa, mshtakiwa alitoa maneno ya uchochezi kuwa "Sirro ni gaidi namba moja nchini Tanzania na fisadi" kwa lengo la kutengeneza chuki kwa wananchi.

Mshitakiwa huyo alikana mashtaka hayo.

Wakili Abood alidai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na uko katika hatua za mwisho.

Issa aliachiwa kwa dhamana baada ya kutakiwa kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh3 milioni kila mmoja, barua ya utambulisho pamoja na kitambulisho cha taifa.

Pia, soma:
1). Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la CHADEMA, Hashimu Issa Juma apelekwa kusikojulikana
2). Mwenyekiti wa BAZECHA akamatwa kwa tuhuma za uchochezi kati ya Serikali na Wananchi
3). Baada ya kufutiwa mashitaka na DPP, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee CHADEMA akamatwa tena na kuswekwa rumande
 
mashitaka ya kuchonga chonga tu...hivi hii nchi ina rais kweli???...mtu anakuwa kiongozi basi asisemwe kisha rais anadai yeye hajilinganishi na Mungu ilhali watendaji wake wanajiona miungu?
 
Kuna habari kakamatwa tena na polisi punde tu alipofutiwa mashtaka na DPP Mwakitalu..
nchi ya hovyo sana hii...yaani polisi iko juu ya mahakama, dpp, wizara ya sheria na hata rais, maana mahakamni kuna picha ya rais!!? na rais, jaji mkuu pamoja na wizara ya sheria wapo wapo tu wanafurahia ushuzi huu kwa sababu wanaona chama cha zamani kinalindwa
 
Back
Top Bottom