Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,462
- 21,334
Timu ya Memphis Grizzlies inayoshiriki ligi Kuu ya kikapu ya NBA, imempeleka mchezaji wake wa kati Hasheem Thabeet kwenye timu ya Dakota Wizards inayocheza ligi ya wachezaji wanaochipukia ya NBA Development League.
Thabeet, mwenye urefu wa futi 7 na inchi 3, ambaye alimaliza akiwa wa pili kwa ubora katika mchujo wa kuwania kuingia ligi kuu ya NBA kutokea vyuoni, ameshushwa daraja ili akajifue upya baada ya kuwa na wastani mbovu wa kufunga pointi 2.5, kuwahi ribaundi 2.9 na kuzuia 1.1 katika mechi 50 alizocheza. Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya chuo kikuu cha Connecticut, alifunga pointi 10 ambazo ndizo pointi zake nyingi zaidi katika mechi moja tangu atue NBA Januari 2 katika mechi dhidi ya Phoenix Suns.
Thabeet ameonekana kuwa ni mchezaji anayehitaji kujifunza zaidi kuboresha uwezo wake, lakini kutokana na mjumuisho adimu wa urefu wake na wepesi uwanjani, vilimfanya apewe nafasi kwenye kikosi dhidi ya wachezaji kama Tyreke Evans, ambaye alichezea Chuo Kikuu cha Memphis, Stephen Curry na James Harden.
Grizzlies hivi sasa imekuwa ikimtumia ikimtumia mchezaji kutoka Irani, Hamed Haddadi, ambaye yuko katika mwaka wake wa pili tangu atue NBA, akiwa kama mchezaji wa akiba wa nafasi ya mchezaji wa kikosi cha kwanza, Marc Gasol.
Thabeet, mwenye umri wa miaka 23, amekuwa ni mchezaji wa kwanza aliyeingia NBA kwa ubora wa juu zaidi kutupwa kwenye ligi ya "wanaochipukia" wa NBA. Mchezaji wa Portland, Martell Webster, ndiye aliyekuwa akiishikilia rekodi hiyo tangu mwaka 2005.
Hata hivyo, Webster yeye aliingia NBA akishika namba 6 kwa ubora, wakati Hasheem aliingia akiwa bora zaidi kwa kushika namba 2.
CHANZO: NIPASHE
Thabeet, mwenye urefu wa futi 7 na inchi 3, ambaye alimaliza akiwa wa pili kwa ubora katika mchujo wa kuwania kuingia ligi kuu ya NBA kutokea vyuoni, ameshushwa daraja ili akajifue upya baada ya kuwa na wastani mbovu wa kufunga pointi 2.5, kuwahi ribaundi 2.9 na kuzuia 1.1 katika mechi 50 alizocheza. Mchezaji huyo wa zamani wa timu ya chuo kikuu cha Connecticut, alifunga pointi 10 ambazo ndizo pointi zake nyingi zaidi katika mechi moja tangu atue NBA Januari 2 katika mechi dhidi ya Phoenix Suns.
Thabeet ameonekana kuwa ni mchezaji anayehitaji kujifunza zaidi kuboresha uwezo wake, lakini kutokana na mjumuisho adimu wa urefu wake na wepesi uwanjani, vilimfanya apewe nafasi kwenye kikosi dhidi ya wachezaji kama Tyreke Evans, ambaye alichezea Chuo Kikuu cha Memphis, Stephen Curry na James Harden.
Grizzlies hivi sasa imekuwa ikimtumia ikimtumia mchezaji kutoka Irani, Hamed Haddadi, ambaye yuko katika mwaka wake wa pili tangu atue NBA, akiwa kama mchezaji wa akiba wa nafasi ya mchezaji wa kikosi cha kwanza, Marc Gasol.
Thabeet, mwenye umri wa miaka 23, amekuwa ni mchezaji wa kwanza aliyeingia NBA kwa ubora wa juu zaidi kutupwa kwenye ligi ya "wanaochipukia" wa NBA. Mchezaji wa Portland, Martell Webster, ndiye aliyekuwa akiishikilia rekodi hiyo tangu mwaka 2005.
Hata hivyo, Webster yeye aliingia NBA akishika namba 6 kwa ubora, wakati Hasheem aliingia akiwa bora zaidi kwa kushika namba 2.
CHANZO: NIPASHE