Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Aliyekuwa mgombea Urais wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma ) katika uchaguzi Mkuu wa mwka 2015, Hshim Rungwe ameitaka serikali kutumia busara zaidi kuliko nguvu katika kumaliza tatizo la mauaji ya watu yanayoendelea mkoani pwani.
Mpaka saa zaidi ya watu 35, wakiwamo viongozi na askari wa Jeshi la Polisi, wameshauawa katika Wilaya za Rufiji, Kibiti na Mkuranga.
Siku chache zilizopita katika mahojiano maalumu na Rungwe ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama chake na wakili wa kujitegemea alisema serikali inapaswa kukaa na waziri wa maeneo ambayo mauaji huwa hutokea ili kutafakali historia ya maisha ya waliouawa.
“Mauaji ya Pwani yanasikitisha na yanaacha hofu miongoni mwa watu . ukiyatanzama ni kama ya visasi kwani ungekuwa ni ujambazi wa kawaida watu hao wangekuwa wanaiba chochote . lakini wao shida yao ni kuua tu,” alisema Rugwe.
Alisema tatizo la Kibiti halitadhibitiwa kwa kuazisha kanda maalumu ya kipolisi, bali ni kujua kwanini watu wanauawa na kisha serikali ishughulikie sababu hizo na si kushughulika na wauaji tu.
“mauaji ya chuki na visasi ni mabaya, ndiyo yanayoisumbua Israel, unakuta watu wengine wanalipiza kwa walichofanyiwa na ndugu zao.
Ndiyo maana ninasema wale ambao ndugu zao wameuawa waulizwe maisha na mahusiano ya hao marehemu na watu wengine yalikuwaje, majibu yatakayotolewa ndicho chanzo cha mauaji,” alisema Rungwe.
Mpaka saa zaidi ya watu 35, wakiwamo viongozi na askari wa Jeshi la Polisi, wameshauawa katika Wilaya za Rufiji, Kibiti na Mkuranga.
Siku chache zilizopita katika mahojiano maalumu na Rungwe ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama chake na wakili wa kujitegemea alisema serikali inapaswa kukaa na waziri wa maeneo ambayo mauaji huwa hutokea ili kutafakali historia ya maisha ya waliouawa.
“Mauaji ya Pwani yanasikitisha na yanaacha hofu miongoni mwa watu . ukiyatanzama ni kama ya visasi kwani ungekuwa ni ujambazi wa kawaida watu hao wangekuwa wanaiba chochote . lakini wao shida yao ni kuua tu,” alisema Rugwe.
Alisema tatizo la Kibiti halitadhibitiwa kwa kuazisha kanda maalumu ya kipolisi, bali ni kujua kwanini watu wanauawa na kisha serikali ishughulikie sababu hizo na si kushughulika na wauaji tu.
“mauaji ya chuki na visasi ni mabaya, ndiyo yanayoisumbua Israel, unakuta watu wengine wanalipiza kwa walichofanyiwa na ndugu zao.
Ndiyo maana ninasema wale ambao ndugu zao wameuawa waulizwe maisha na mahusiano ya hao marehemu na watu wengine yalikuwaje, majibu yatakayotolewa ndicho chanzo cha mauaji,” alisema Rungwe.