Hasara za kutokuwa na uchaguzi Huru na Wazi (ukosefu wa Tume huru)

Shocker

JF-Expert Member
Sep 15, 2012
1,930
3,803
Uchunguzi wa muda mfupi, tuseme uchunguzi binafsi umeonyesha wale viongozi wanaopita bila ya ridhaa za wananchi au wameshinda uchaguzi kwa njia za udanganyifu uliotokana na wao au tume ya Uchaguzi, viongozi hao hawana maadili mazuri na kazi zao na maendeleo yao binafsi huonekana muda mfupi tu baada ya kuanza kuzoea mazingira.

Viongozi wanaoingia kwa njia hizi kuanzia raisi mpaka anaefagia njia, huingia kazini kwa makeke na majigambo makubwa sana kiasi ya kuwakubalisha wananchi kuwa sasa tutaendelea lakini wapi baada ya mwaka tu tamaa ya maendeleo kwa wananchi inaanza kuondoka na hatimae hukatika kabisa. Na badala yake wale wavukishwa daraja wanazidi jeuri na kuanza kumiliki mali magari na majumba makubwa tu, hilo liweke kando.

Kasi ya uwajibikaji huondoka yale majigambo huzima mfano hai ni Zanzibar, sasa serikali inaelekea kushindwa na ile kasi yake haipo imeanza kutoweka, leo hii Zanzibar inaongoza kwa uchafu kuanzia mijini, vijijini hata mashamba ni uchafu kwa kwenda mbele, wale waliokodiwa kutoka Tanganyika kazi imashinda haijulikani wapo wapi na yule Waziri inaonekana yupo kimya kama alieambia Nyamaza na tulia.

Nadharia ya yajayo nafurahisha sasa inaonekana wazi kabisa yajayo yanakirihisha.
 
Madhara ni MAKUBWA sana na ndiyo yaliyopelekea Kutafuta Wabunge Fake 19 ili kuunda KAMBI ya UPINZANI
Bunge halina KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani
Bunge halina Mawaziri Vivuli
Bunge halina Bajeti Vivuli
Bunge halina Bajeti Kuu Ya Serikali kutoka Upinzani ni VIOJA NA MAAJABU ya TANZANIA
 
Madhara ni MAKUBWA sana na ndiyo yaliyopelekea Kutafuta Wabunge Fake 19 ili kuunda KAMBI ya UPINZANI
Bunge halina KIONGOZI wa Kambi ya Upinzani
Bunge halina Mawaziri Vivuli
Bunge halina Bajeti Vivuli
Bunge halina Bajeti Kuu Ya Serikali kutoka Upinzani ni VIOJA NA MAAJABU ya TANZANIA
Hakuna bunge hapo hilo ni genge la majangili
 
Kuna mbunge wa kupita bila kupingwa aliomba bungeni apunguziwe kazi za kuzuia mvua kwani zinamchoosha sana!🐒🐒🐒
109_20210616_105039.jpg
 
Katika bunge la hovyo kuwai kutokea tz ni bunge la huyu bwana ndugai...!! Yani mule ndani ni mipasho kwakwenda mbele na swala la katiba sioni kama kuna msemaji wa hili uko bungeni!!!! Hii nchi ilitakiwa vijana tuwe na sera zetu na namna nzuri yakushinikiza serikali kwenye mambo muhimu" katiba, ajira, na kilimo. Maana wanaoasirika na katiba asilimia 70 ni vijana kule bungeni sisikii wakiongelea ajira,kilimo chenye Tija na katiba.... Na wanaogopa kwasababu katiba mpya ni lazima iwanyooshe sioni sababu ya mbunge kuwa analipwa zaidi ya milioni10 kwa mwezi wakati mwalimu, dr, wauguzi wakiwa na mshahara wa hovyo kabisa... Hili kwenye katiba ni lazima lirekebishwe kazi ya ubunge pia ni wito kwann wasilipwe milioni 1na laki2 pale dodoma pawe na nyumba zijengwe kwaajili ya wao kifikia kipindi cha bunge kuanza... Kama police wanavyoishi kota na wao wawe na kota.. Posho iwe mafuta,vocha, na mavazi, hii ingefanya tupate watu wa kweli wenye uchungu na nchi hii lakini pia ingepunguza bajeti kuwa kubwa nakuchezea kodi za wananchi... Bunge limekuwa ni sehemu ya wahuni kujificha huko na kula cake ya taifa, hili linakera sana!!! Kimsingi katika inatakiwa ila namna yakuidai katiba nafikiri ichi ndo kipengele tunaidaije ikiwa wabunge wenyewe hawana ata muda kuijadili katiba zaidi yakula pesa na makofi imeisha
 
Back
Top Bottom