Harusi zisiwe usumbufu, ukitaka kuoa kwa harusi kubwa wewe na familia yako mjipange kwanza vizuri

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,580
46,167
Huu utamaduni wa kuchangisha watu pesa wakati mtu anapooa huenda ulikuwepo tangu karne na sisi tukaurithi kutoka kwa babu zetu au kutoka kwa wakoloni wetu lakini kadri muda unavyoonda unageuka kuwa usumbufu mkubwa.

Fikiria mtu anatuma meseji kwenye WhatsApp group la harusi alilokuunganisha bila ridhaa yako, anatuma kwenye WhatsApp yako ya binafsi, anatuma pia texts za kawaida, zote hizo ujumbe ni mmoja kukumbusha kulipa mchango wa kijana wao ambao wakati mwingine hata haujatoa ahadi ya kuutoa!

Ukitaka harusi kubwa kadiria kulingana na kipato chako na cha familia yenu, wengine wa mbali wawe ni kujazia tu, epuka kuwapa watu usumbufu usio wa lazima.
 
Tuwe na tabia ya kufanya mambo kwa uwezo tulionao, hata kama utaongezewa basi isiwe ya usumbufu.
Yafaa nini kufanya harusi kuuuuubwa,

kwenda honeymoon hotel nzuriiiii,

Halafu unarudi uswahilini kuendelea na maisha yaleyaleeee, Madeni ya kutosha, kisa harusi kubwa.

TUJIKUNE TUNAPOFIKISHA MKONO NDUGU!
 
Ndo mana me nilikwenda kufunga ndoa kijijini kwetu nikaja na wife hadi dar maisha yanaendelea na sikutaka kumsumbua mtu mchango wowote.
Nilijipanga mwenyewe kwa kipato changu nikapata 2M
Mchele 250kg @1000= 250000
Ng’ombe 1 @ 250000
Viungo na mengineyo 300000
Mc na mapambo na music 200,000
Bia kwa watu wangu wa kalibu na wageni maalumu 300,000
Ukumbi ni nje pamewekwa turubai

Jumla tsh. 1M
Nilichofanya ni kuita watu kwa mualiko wa kuja kula tu na kuhudhuria sherehe yangu basi.
Leo mtu aniletee message ya mchango tamijibu utumbo hata tuma tena.

Nakumbuka jamaa zangu waliniambia fungia ndoa dar na kucheki cost around 8M minimum, then nitegemee michango ya wadau ndonifanye sherehe nikaona huo ujinga sina wakati me mtu wa kijijini.
 
Kiukweli siku hizi michango ya harusi imegeuka kero.

Cha ajabu tabia za wataka michango wote huwa zinafanana hamna mwenye unafuu hasa tabia ya wengi kugeuza mchango kuwa kama deni ambalo usipokuwa makini linaeza kuwa chanzo cha kuondoa ukaribu uliokuwepo awali.
 
Ni ulimbukeni na kufuata mikumbo tu
Tuwe na tabia ya kufanya mambo kwa uwezo tulionao, hata kama utaongezewa basi isiwe ya usumbufu.
Yafaa nini kufanya harusi kuuuuubwa,
kwenda honeymoon hotel nzuriiiii,
Halafu unarudi uswahilini kuendelea na maisha yaleyaleeee, Madeni ya kutosha, kisa harusi kubwa.
TUJIKUNE TUNAPOFIKISHA MKONO NDUGU!
 
Imenikuta kwa jamaa tulisoma wote advance, last week kanitumia sms ya mchango bila hata salamu kana kwamba huwa tunaongea mara kwa mara. Mbaya zaidi kaniunga kwenye group la michango.

Sina shida na michango. Tatizo ni kukosa uungwana na utu.
Hii inatokeaga sana,
Jamaa huna mawasiliano naye hata ya salaam, ghafla unaombwa mchango.
 
Ki ukweli inakera unaunganishwa bila ridhaa yako. Kuna group moja niliunganishwa. Mmoja akawa na harusi tukachangia na mwengine akawa na harusi tukachangia wengine wakawa hawachangii.na wa 3 akawa na harusi mmoja alimpa za uso kwenye group wewe ulikuwa huchangii na sisi hatukuchangii.akajitoa
Ila mimi najiuliza kwa nini usifanye shuhuli kulingana na uwezo wako.hata iwe ndogo tu tatizo ni nini?
 
Nashauri serikali yetu iingilie kati.

HAIWEZEKANI,
Serikali yetu inahangaika kupata pesa kutekeleza miradi ya maendeleo,

Afu Kuna mtu anahangaika kuteketeza pesa kwa ajili ya harusi.
 
Back
Top Bottom