Linguistic
JF-Expert Member
- Mar 16, 2021
- 3,671
- 8,237
Mfanyabiashara raia wa Uturuki, Harun Aydin anayehusishwa na Naibu Rais William Ruto ametimuliwa nchini.
Aydin alikamatwa katika uwanja wa ndege alipokuwa akiingia humu nchini kutoka Uganda, Jumamosi, Agosti 7.
Mturuki huyo alikuwa anatarajiwa kufikishwa katika Mahakama ya Kahawa West hii leo Jumatatu, Agosti 9, wakati taarifa ya kutimuliwa kwake ilifichuliwa.
Akithibitisha kisa hicho, wakili wa Aydin, Ahmedinasir Abdullahi alisema alikuwa tayari kumwakilisha katika Mahakama ya Kahawa wakati alifahimishwa kuhusu kutimuliwa kwake.
Grand Mullah alizua kwamba kwa siku mbili ambazo Aydin alikuwa amezuiliwa, hakukubaliwa kumuona.
Mfanyabiashara huyo anaripotiwa kupandishwa kwenye ndege ya shirika la Uturuki mwendo wa saa kumi na moja asubuhi na kutua jijini Istanbul ambapo alipokelewa na maafisa wa usalama ili kuhojiwa zaidi.
Aydin alikamatwa katika uwanja wa ndege alipokuwa akiingia humu nchini kutoka Uganda, Jumamosi, Agosti 7.
Mturuki huyo alikuwa anatarajiwa kufikishwa katika Mahakama ya Kahawa West hii leo Jumatatu, Agosti 9, wakati taarifa ya kutimuliwa kwake ilifichuliwa.
Akithibitisha kisa hicho, wakili wa Aydin, Ahmedinasir Abdullahi alisema alikuwa tayari kumwakilisha katika Mahakama ya Kahawa wakati alifahimishwa kuhusu kutimuliwa kwake.
Grand Mullah alizua kwamba kwa siku mbili ambazo Aydin alikuwa amezuiliwa, hakukubaliwa kumuona.
Mfanyabiashara huyo anaripotiwa kupandishwa kwenye ndege ya shirika la Uturuki mwendo wa saa kumi na moja asubuhi na kutua jijini Istanbul ambapo alipokelewa na maafisa wa usalama ili kuhojiwa zaidi.