Haro

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
Kuna watu ambao wamekuwa na udhaifu wa kuchanganya matamshi ya herufi kadhaa. Kwa Wamakonde M wao huitamka kama N (mathalan, mtu wao husema ntu) kuna wengine kwenye R wao huweka L na kinyume chake (kuna mwalimu wetu wa shule ya msingi alituchapa kutokana naudhaifu wake wa kuchanganya R na L. Aliandika ubaoni neno MAPERA; sasa akawa analisoma ili nasisi tumfuatilizie, yeye akitamka alikuwa anasema MAPELA na sisi tukawa tunamfuatishia hivyo hivyo. Tulipokuwa tunatamka MAPELA akawa anatwambia tume kosea na kutusahihisha kwa kusema SIYO MAPELA ni MAPELA. Hatimaye tukaishia kuchapwa viboko) Utawasikia wengi wa Wakurya wanakwambi HARO badala ya HALO.

Hivi huu udhaifu chanzo chake ni nini? Je, hauwezi kurekebishika?
 
Kuna watu ambao wamekuwa na udhaifu wa kuchanganya matamshi ya herufi kadhaa. Kwa Wamakonde M wao huitamka kama N (mathalan, mtu wao husema ntu) kuna wengine kwenye R wao huweka L na kinyume chake (kuna mwalimu wetu wa shule ya msingi alituchapa kutokana naudhaifu wake wa kuchanganya R na L. Aliandika ubaoni neno MAPERA; sasa akawa analisoma ili nasisi tumfuatilizie, yeye akitamka alikuwa anasema MAPELA na sisi tukawa tunamfuatishia hivyo hivyo. Tulipokuwa tunatamka MAPELA akawa anatwambia tume kosea na kutusahihisha kwa kusema SIYO MAPELA ni MAPELA. Hatimaye tukaishia kuchapwa viboko) Utawasikia wengi wa Wakurya wanakwambi HARO badala ya HALO.

Hivi huu udhaifu chanzo chake ni nini? Je, hauwezi kurekebishika?
Kijana huo si udhaifu kama unavyo fikiria, bali kunatokana na athari ya Lugha ya kwanza ya mzungumzaji. Wazungumzaji wa Lugha wote wameathiriwa na Lafudhi au Lahaja...! Na ni kitu cha kawaida sana.
 
.. kuna mwalimu wetu wa shule ya msingi alituchapa kutokana naudhaifu wake wa kuchanganya R na L. Aliandika ubaoni neno MAPERA; sasa akawa analisoma ili nasisi tumfuatilizie, yeye akitamka alikuwa anasema MAPELA na sisi tukawa tunamfuatishia hivyo hivyo. Tulipokuwa tunatamka MAPELA akawa anatwambia tume kosea na kutusahihisha kwa kusema SIYO MAPELA ni MAPELA. Hatimaye tukaishia kuchapwa viboko
Pole na viboko vingi!

Tatizo la L/R linapatikana kwa wasemaji wa lugha mbalimbali za Kibantu. Ukipeleka "l/r mixup in pronounciation"n kwa google utakuta ya kwamba pale inatajwa hasa kama tatizo la Wajapani na Wakorea (pia Wachina). Bila shaka sababu yake ni watu hao wanajulikana zaidi kimataifa kuliko Wamakonde au Wagikuyu.

Nimesikia msingi wa tatizo ni ya kwamba katika lugha mbalimbali L na R ni sauti moja tu; au tusdeme hivi: hawana L au R kama lugha nyingine bali sauti ya pamoja. Kwa hiyo pale wakijifunza lugha inayotofautisha L na R wanaweza kuwa na matata.

Nimeiona vikali kati ya Wasafwa wasiosikia tofauti hata kidogo wakati wa kuandika wanaelea hewani tu.

Nadhani mwalimu wako aliweza kusikia kitu ambacho ninyi mlishindwa kusikia kati ya L na R hivyo alikasirika na kufikiri mnamtania. Lakini mwalimu anatakiwa kujua tatizo hili. Pole sana!
 
Au wamakonde. Nakumbuka miaka ya 60's walikuwa wamejaa sana Msasani (ilikuwa kama makao yao makuu). Wao walipaita Mchachani. Na tulipokuwa kwenye mafundisho ya dini kanisa la St. Joseph walishindwa kabisa kusema Bwana Yesu alitushukia. Wao walisema Bwana Yesu alituChukia. Yaani walikuwa wanamkera padri saaana!!!!
 
Au wamakonde. Nakumbuka miaka ya 60's walikuwa wamejaa sana Msasani (ilikuwa kama makao yao makuu). Wao walipaita Mchachani. Na tulipokuwa kwenye mafundisho ya dini kanisa la St. Joseph walishindwa kabisa kusema Bwana Yesu alitushukia. Wao walisema Bwana Yesu alituChukia. Yaani walikuwa wanamkera padri saaana!!!!
Mkuu sahihisho kidogo... Neno Msasani asili yake linatokana na Mzee maarufu aliyekuwa akiishi uko, akijulikana kama Mzee Mussa Hassan. Wamakonde kwa kushindwa kutamka vizuri ndio ikapelekea eneo ilo kuitwa Msasani.
 
Hiyo yote ya Mussa Hassani naifahamu, manaake hapo ndipo nilipokulia enzi hizo. Lakini Mkuu kama wewe umewasikia wamakonde wakitaja Msasani hutabisha. Nimewasikia kwa masikio yangu. Wamakonde waliseto baada ya hapo mahali kupata hilo jina. Ukichimama nchale, ukikaa nchale, ukikimbia nchale, unaikumbuka hiyoooo!
 
Hiyo yote ya Mussa Hassani naifahamu, manaake hapo ndipo nilipokulia enzi hizo. Lakini Mkuu kama wewe umewasikia wamakonde wakitaja Msasani hutabisha. Nimewasikia kwa masikio yangu. Wamakonde waliseto baada ya hapo mahali kupata hilo jina. Ukichimama nchale, ukikaa nchale, ukikimbia nchale, unaikumbuka hiyoooo!
Sijakubishia... Ni katika kuchangia tu.

Shukran.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom