Harmonize: Nimewalipa Wasafi Tshs milioni 500 kuvunja mkataba

idawa

JF-Expert Member
Jan 20, 2012
25,284
38,312
Akihojiwa na Clouds FM kwenye XXL amesema imemlazimu kulipa million 500 ili kuvunja mkaba na Kampuni ya Wasafi.

Amesema kampuni ya Wasafi walimzuia kutumia chochote kilichotokana na Wasafi ikiwemo jina la Harmonize, nyimbo zake, akaunti za mitandao ya kijamii na mengineyo.

Ili kuendelea kutumia nyimbo hizo imemlazima kulipa milion 500, amesema kuwa ameuza nyumba zake tatu na baadhi ya aseti na yupo kwenye hatua za kumalizia deni lake ili aweze kupiga nyimbo zake popote pale.

Kuhusu kugombea ubunge amesema kauli ya Rais ni kama sheria hivyo yupo tayari kutekeleza agizo la mheshimiwa.

2020 Harmonize mjengoni.!

Ameongeza kuwa ugomvi wa Vyombo vya habari unarudisha mziki nyuma.

Amewekea mfano Whozu na Marioo kuwa ni wasanii ambao wanashindwa wasimame na media ipi.

Hapa inaonesha kuna wasanii wengi wanapenda kushirikiana Wasafi FM ila wanaogopa kutengwa na Clouds.

 
Asihofu acha awalipe maana domo ana wivu sana, anataka awe mfalme peke yake, kwanza mwakani anakuwa mbunge atapata na uwaziri wa michezo, akichanganya na kipaji chake atapata hizo nyumba mapema tu.
Jana nimemuona Q-Boy amebaki kuwa kinyozi tu Kariakoo. Domo ukimchekea utabaki kupata tu sifa mitandaoni, mademu, na show offs.

Ukichokwa unapigwa chini, unapotea. Harmonize kashtuka mapema. Anaweza kuinuka
 
Clouds
IMG_20191024_155146.jpeg
 
Kosa Lake Ni Kuwekeza Kwa Mtu Halafu Unavuna Kupita Kiasi HALAFU Unakuwa Mnafiki Kwenye Jamii Kwa Kutaka Uonekane Umefanya WEMA SAAANA na UMEMSAIDIA SANA bila kupata faida yoyote
Diamond ni Business man,Mziki ni Biashara na Biashara haina undugu na sheria ni msumeno Mkataba aliusaini mwenyewe na ameuvunja mwenyewe unakuja hapa kumtukana Diamond kwa kosa lipi.
 
Back
Top Bottom