Mohamed Ismail
JF-Expert Member
- Mar 16, 2014
- 212
- 221
Ilinichukua muda nikiwa kimya najiuliza maswali siyo chini ya 20 kwamba Harmonize ataingia jukwaani kwa style gani? Sikutegemea kuona akija na helikopta maana alishaitumia kwenye mazoezi. Nikiwa kwenye tafakuri nikaona watu wanapita na farasi mara wengine na vibaiskeli nikahisi huyu mtu hakawii kuja na tembo uwanjani.
Konde ni mtu wa kuthubutu nani alijua kwamba angetoka Wasafi na akasimama kama alivyo sasa? Ni mtu asiyekata tamaa na shupavu ambaye damu yake ina chembechembe za Kinjekitile pamoja na Mtwa Mkwawa.
Nikiwa kwenye runinga niliona mtu anatambaa kwenye kamba kutoka angani huku akipeperusha bendera ya Yanga kwa madoido.... Nikamuambia mtu niliyekuwa naye karibu huyo ndio Konde akaniambia hapana hawezi kuwa yeye itakuwa katumia Komando wa jeshi.
Uwanja ukiwa umekaa kimya na wale wenzangu na mimi wenye roho nyepesi walishindwa kuangalia tukio wakaangalia chini. Mara paap! tuliona yule mmakonde aliyetokea kijijini Chitoli akidondoka kama kitenesi na kudunda na baada ya hapo akaendelea kuwatumbuiza wananchi. Wananchi walinyanyuka kwa furaha wakaona kweli Yanga mpya imezaliwa na kitendo hiki kilifanya wananchi wajisikie vibaya maana waliona kiingilio kimekuwa kidogo kulingana na show babkubwa waliyoipata.
Harmonize ujasiri wake ni kama wa sisimizi wawezao kuvuka mto kwa kuwafanya sisimizi wenzao waliokufa na kuelea majini kama daraja lao. Baadae yule jirani akaniambia huyu mtoto siyo wa kawaida maana hayo ni mafunzo ya kijeshi. Na huwa si chini ya wiki tatu ili mtu aweze kuiva. Na ukienda kwenye mafunzo ya ukomando kwenye Airborne ndio utakutana na hizo Commando rope kwa kutumia Carabiner ambapo hili tukio kitaalamu kijeshi wanaita Rappel seat method.
Mlimwengu mimi nasema hivi kwamba wapenda muziki tumepata jibu maana huyu mmakonde anakuja na mapinduzi ya kijeshi. Na hii imedhihirisha umma kupitia siku ya mwananchi kwamba Harmonize ni mjeshi kamili na mwanamuziki aliyekamilika.
#mlimwengumimi
Konde ni mtu wa kuthubutu nani alijua kwamba angetoka Wasafi na akasimama kama alivyo sasa? Ni mtu asiyekata tamaa na shupavu ambaye damu yake ina chembechembe za Kinjekitile pamoja na Mtwa Mkwawa.
Nikiwa kwenye runinga niliona mtu anatambaa kwenye kamba kutoka angani huku akipeperusha bendera ya Yanga kwa madoido.... Nikamuambia mtu niliyekuwa naye karibu huyo ndio Konde akaniambia hapana hawezi kuwa yeye itakuwa katumia Komando wa jeshi.
Uwanja ukiwa umekaa kimya na wale wenzangu na mimi wenye roho nyepesi walishindwa kuangalia tukio wakaangalia chini. Mara paap! tuliona yule mmakonde aliyetokea kijijini Chitoli akidondoka kama kitenesi na kudunda na baada ya hapo akaendelea kuwatumbuiza wananchi. Wananchi walinyanyuka kwa furaha wakaona kweli Yanga mpya imezaliwa na kitendo hiki kilifanya wananchi wajisikie vibaya maana waliona kiingilio kimekuwa kidogo kulingana na show babkubwa waliyoipata.
Harmonize ujasiri wake ni kama wa sisimizi wawezao kuvuka mto kwa kuwafanya sisimizi wenzao waliokufa na kuelea majini kama daraja lao. Baadae yule jirani akaniambia huyu mtoto siyo wa kawaida maana hayo ni mafunzo ya kijeshi. Na huwa si chini ya wiki tatu ili mtu aweze kuiva. Na ukienda kwenye mafunzo ya ukomando kwenye Airborne ndio utakutana na hizo Commando rope kwa kutumia Carabiner ambapo hili tukio kitaalamu kijeshi wanaita Rappel seat method.
Mlimwengu mimi nasema hivi kwamba wapenda muziki tumepata jibu maana huyu mmakonde anakuja na mapinduzi ya kijeshi. Na hii imedhihirisha umma kupitia siku ya mwananchi kwamba Harmonize ni mjeshi kamili na mwanamuziki aliyekamilika.
#mlimwengumimi