Harmonize anahamasisha matumizi ya madawa ya kulevya kwenye nyimbo zake. Serikali hamlioni hili?

Harmonize ametoa wimbo unaohamasisha matumizi ya bange lakini cha ajabu mpaka sasa serikali bado haijamchukulia hatua zozote za kinidhamu.

Huyu jamaa ulimbukeni na ushamba vinampeleka puta sana, hayo mambo ya mabangi yake angebaki nayo huko huko lakini si kuja kututangazia upumbavu wake.
Weka link tuusikilize tuone kama unashawishi kweli hadi mtu akashawishika kuivuta.
Nani anaikumbuka movie ya Chris Turker na Ice Cube FRIDAY ?
 
Si yeye tu, kariba ya wasanii wote wanaimba mambo ya kuhamasisha maovu na machafu... asipodhihirika kwenye sauti utampata kwenye video ukimkosa kwenye video utamshika kwenye jina utampata kwenye maudhui na kama ukimkosa kwenye vyote utampata kwenye lifestyle mfano chakula, mavazi, lugha, hobby, na kadhalika

ngalia orodha

"Nikishalewa sitaki nighasiwe..."

"Bora/acha nilewe..."

"Je watakubali... kula kwangu hadi nikimbizwe..."

"Raha nikikuta simba wanacheza... nitakula jicho..."

"Mimi ndo rafiki wa Lucifer utaniambia nini?..."

"Shetani mwenyewe akiniona anatoka mkuku..."

"Man down..."

"Masikini jeuri..."

"Kasimama dede..."

"Mbona hutokei..."

"Mitungi mikasi"

"Sukari..."

"Kamatia chini..."

"Mwagia ndani..."

Orodha ni ndefu lakini kiujumla hawa wasanii ukiangalia vizuri vaa yao ongea yao na kazi wanazofanya ndo utagundua kwanini wajanja wanakwambia MZIKI DHAMBI
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom