Hard talk: Kuhusu Sheria za Ardhi pekee

sagaciR

JF-Expert Member
Jun 17, 2017
644
875
Sina maana ya kutotambua wanasheria wasomi wengine ila nampongeza sana Dragoo kwa mchango wake wa kuanzia uzi maarufu sana hapa jukwaa la sheria wenye maneno "Legal documents na uchambuzi wa masuala ya kisheria".

Kwa kuwa uzi tajwa hapa juu, unahusu sheria yoyote (to mention few Company, Land, Criminal, Tort, Contract, Insurance, Tax, Legal books, papers etc) basi nimeona sio mbaya kama tukiwa na platform/ roundtable ya maada maalumu kwa ajili ya Sheria za Ardhi pekee.

Mwalimu wangu wa chuo kikuu mwaka wa pili (2nd year) alitusisitiza kupenda sheria za Ardhi kwa maneno/usemi ufuatao:-

"We live on the land, we walk on the land, we build on the land, we are buried on the land therefore we must know land laws/land law is inevitably"

Kifungu cha 2 cha sheria ya Ardhi Na. 4/1999 pomoja na Na. 5/1999 kinatoa maana ya Ardhi kwa maneno haya:-

"Ardhi inajumuisha ardhi iliyo juu ya uso wa nchi na ardhi iliyo chini ya uso wa nchi, pamoja na maada zote isipokuwa madini na petroli ambavyo ni sehemu ya uso wa nchi au chini ya uso wa nchi, vitu vyenye kuota kiasili juu ya ardhi, majengo na miundo mingineyo iliyokaziwa kwa kudumu juu ya ardhi"

Kutoa elimu ya kisheria kwa umma sio biashara (na ndo maana hakuna kodi) ila Kutoa huduma ya kisheria ni biashara (na ndo maana ina kodi)

KARIBUNI KWA MASWALI NA UCHANGIAJI WA HOJA ILI TUPEANE ELIMU YA KISHERIA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
a
Sina maana ya kutotambua wanasheria wasomi wengine ila nampongeza sana Dragoo kwa mchango wake wa kuanzia uzi maarufu sana hapa jukwaa la sheria wenye maneno "Legal documents na uchambuzi wa masuala ya kisheria".

Kwa kuwa uzi tajwa hapa juu, unahusu sheria yoyote (to mention few Company, Land, Criminal, Tort, Contract, Insurance, Tax, Legal books, papers etc) basi nimeona sio mbaya kama tukiwa na platform/ roundtable ya maada maalumu kwa ajili ya Sheria za Ardhi pekee.

Mwalimu wangu wa chuo kikuu mwaka wa pili (2nd year) alitusisitiza kupenda sheria za Ardhi kwa maneno/usemi ufuatao:-

"We live on the land, we walk on the land, we build on the land, we are buried on the land therefore we must know land laws/land law is inevitably"

Kifungu cha 2 cha sheria ya Ardhi Na. 4/1999 pomoja na Na. 5/1999 kinatoa maana ya Ardhi kwa maneno haya:-

"Ardhi inajumuisha ardhi iliyo juu ya uso wa nchi na ardhi iliyo chini ya uso wa nchi, pamoja na maada zote isipokuwa madini na petroli ambavyo ni sehemu ya uso wa nchi au chini ya uso wa nchi, vitu vyenye kuota kiasili juu ya ardhi, majengo na miundo mingineyo iliyokaziwa kwa kudumu juu ya ardhi"

Kutoa elimu ya kisheria kwa umma sio biashara (na ndo maana hakuna kodi) ila Kutoa huduma ya kisheria ni biashara (na ndo maana ina kodi)

KARIBUNI KWA MASWALI NA UCHANGIAJI WA HOJA ILI TUPEANE ELIMU YA KISHERIA

Sent using Jamii Forums mobile app
sante sana. Nakukumbuka huwa unajitokeza sana linapokuja suala la sheria. Ni jambo jema sana kuanzisha uzi huuu.

Naanza mimi na swali?Nikitaka kupima eneo langu nafuata utaratibu gani. Nauliza hivyo kwa vile ukienda kuomba kupimiwa wanasema hatuwezi kupima kiwanja kimoja lazima muwe wengi. hii ni sawa?
 
MSAADA MSAADA MSAADA MSAADA

Habari za muda huu kwa mara nyingine tena

Natafuta kazi ndugu zangu watanzania wenzangu

Ata kama uta-nidalalia iyo kazi tutaelewana malipo ndugu yangu

naombeni msaada wenu mwenye kuweza kunisaidia, maana nimeshaangaika sana kutafuta kazi ila naambulia patupu

Nimezunguka sana kwenye viwanda, site za ujenzi ila naambuliwa patupu, naombeni msaada wenu, ata kama nitapata kazi ya ku-volunteer tuu, pia ntashukuru sana ndugu zangu...

Maana umri pia unakimbia, nisaidieni sana

Elimu yangu: Degree

Fani: CYBER SECURITY (ULINZI NA USALAMA WA MIUNDOMBINU YA TEKNOLOJIA)

Other Award: Diploma in computer science (SAYANSI YA KOMPUTA)

Na nimekuwa mbobezi katika mambo ya

》Penetration Testing, kutafuta vulnerabilities, kufanya sniffing, exploits & tools, nina uelewa wa kutosha kuhusiana na social engineering

》ku-secure system kwa kutumia linux, DNS, na kwa kutumia cryptography

》ku-secure connectivity kama vile switch, router, firewalls, vpn, ips(intrusion prevention system ) pamoja na ids (intrusion ditectin system) nadhani wataalum watakuwa wamenielewa kwenye ivyo vifupo

》Digital forensics inverstigation (computer pamoja na simu)

》Computer Networking

》 System analysis and design

MSAADA WENU WAUNGWANA

MPAKA NIMEAMUA KUWAANGUKIA NDUGU ZANGU MNISAIDIE UJUE NIMESHAKATA TAMAA, MAANA

KULIKO KULIA PEKE YANGU, NIMEONA NIWALILIE WATANZANIA WENZANGU MNISAIDIE NDUGU ZANGU

NIMESHATAFUTA SANA KAZI, KUANZIA APPLICATION ZA ONLINE, MPAKA MANUALLY

NOTE: KAZI YEYOTE ILE NTAFANYA ATA KAMA NI NJE YA TAALUMA YANGU, NA NTAIFANYA KWA UAMINIFU MKUBWA MNO

MUNGU WABARIKI SANA

NO YANGU: 0755836347
NAPATIKANA: DSM-MBEZI MSAKUZI

NISAMBAZIENI KWENYE MA-GROUP MENGINE NIPATE MSAADA
 
a

sante sana. Nakukumbuka huwa unajitokeza sana linapokuja suala la sheria. Ni jambo jema sana kuanzisha uzi huuu.

Naanza mimi na swali?Nikitaka kupima eneo langu nafuata utaratibu gani. Nauliza hivyo kwa vile ukienda kuomba kupimiwa wanasema hatuwezi kupima kiwanja kimoja lazima muwe wengi. hii ni sawa?
Mkuu, retired
Mosi, upimaji wa Ardhi hutegemea na unapima kiwanja/viwanja ama mashamba. Kama ni viwanja maana yake sheria itayotumika ni sheria ya upimaji Ardhi sura 324 pamoja na sheria ya mpingo miji Na 8/2007.

Pili, Zoezi la upimaji viwanja huishia kwa mkurugenzi wa ramani/mpango miji kukubali upimaji huo so huwa ni lazma uandaliwe mchoro wa eneo linalopimwa ndo maana unaambiwa muwe wengi ili kupata ramani ya eneo husika kwa ajili ya huduma za jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, retired
Mosi, upimaji wa Ardhi hutegemea na unapima kiwanja/viwanja ama mashamba. Kama ni viwanja maana yake sheria itayotumika ni sheria ya upimaji Ardhi sura 324 pamoja na sheria ya mpingo miji Na 8/2007.

Pili, Zoezi la upimaji viwanja huishia kwa mkurugenzi wa ramani/mpango miji kukubali upimaji huo so huwa ni lazma uandaliwe mchoro wa eneo linalopimwa ndo maana unaambiwa muwe wengi ili kupata ramani ya eneo husika kwa ajili ya huduma za jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
naomba soft copy ya sheria ya upimaji ardhi na sheria ya mipango miji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, retired
Mosi, upimaji wa Ardhi hutegemea na unapima kiwanja/viwanja ama mashamba. Kama ni viwanja maana yake sheria itayotumika ni sheria ya upimaji Ardhi sura 324 pamoja na sheria ya mpingo miji Na 8/2007.

Pili, Zoezi la upimaji viwanja huishia kwa mkurugenzi wa ramani/mpango miji kukubali upimaji huo so huwa ni lazma uandaliwe mchoro wa eneo linalopimwa ndo maana unaambiwa muwe wengi ili kupata ramani ya eneo husika kwa ajili ya huduma za jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante. Nimekuelewa. Hvyo inabidi watu tuitane tuwe engi vinginevyo kiwanja kimoja hawapimi.
Naomba unieleweshe concept ya planning area....
The Town and Country Planning Ordinance. Cap. 378 makes elaborate provisions on urban development. The Ordinance empowers the relevant Minister to declare an area to be a planning area. Once an area is so declared “no person shall develop any land within a planning area without planning consent.
Kuna maeneo yetu hayajapimwa, si yanaweza kutwaliwa tukala hasara? Tufanyeje?
 
Asante. Nimekuelewa. Hvyo inabidi watu tuitane tuwe engi vinginevyo kiwanja kimoja hawapimi.
Naomba unieleweshe concept ya planning area....
The Town and Country Planning Ordinance. Cap. 378 makes elaborate provisions on urban development. The Ordinance empowers the relevant Minister to declare an area to be a planning area. Once an area is so declared “no person shall develop any land within a planning area without planning consent.
Kuna maeneo yetu hayajapimwa, si yanaweza kutwaliwa tukala hasara? Tufanyeje?
Mosi, planning area ni eneo ambalo limeingizwa kwny mipango ya matumizi kupitia mfumo wa ramani/mchoro ikizingatia huduma za kijamii. Eneo hili linaweza kuwa la makazi, makazi na biashara, biashara ama viwanda, makaburi n.k. Utaratibu huu usimamiwa na sheria ya mipango miji Na. 8-2007.

Pili, Eneo kama likitwaliwa na serikali kwa ajili ya matumizi ya umma kama vile shule, Disp, Office n.k hutwaliwa kwa utaratibu wa sheria ya utwaaji Ardhi sura ya 118 (angalia kifungu cha 4) na utalipwa fidia kama ilivyo kwny katiba ibara ya 24(2) na sheria ya ardhi Na. 4/1999 kifungu cha 3 (g).

Tamati, eneo kupimwa sio kutwaliwa hapana. Kutwaliwa ni utaratibu mwingine. Napia eneo kupimwa sio uvamizi (trespass to land) uvamizi unatokea pale ambapo aliyepima akianza kuwapa umiliki watu wengine (third party).

Sent using Jamii Forums mobile app

NB: The Town and Country Planning Ordinance. Cap. 378 ILISHAFUTWA NA KIFUNGU CHA 80 CHA SHERIA NA. 8-2007. (haitumiki tena, ni repealed law)
 
Mosi, planning area ni eneo ambalo limeingizwa kwny mipango ya matumizi kupitia mfumo wa ramani/mchoro ikizingatia huduma za kijamii. Eneo hili linaweza kuwa la makazi, makazi na biashara, biashara ama viwanda, makaburi n.k. Utaratibu huu usimamiwa na sheria ya mipango miji Na. 8-2007.

Pili, Eneo kama likitwaliwa na serikali kwa ajili ya matumizi ya umma kama vile shule, Disp, Office n.k hutwaliwa kwa utaratibu wa sheria ya utwaaji Ardhi sura ya 118 (angalia kifungu cha 4) na utalipwa fidia kama ilivyo kwny katiba ibara ya 24(2) na sheria ya ardhi Na. 4/1999 kifungu cha 3 (g).

Tamati, eneo kupimwa sio kutwaliwa hapana. Kutwaliwa ni utaratibu mwingine. Napia eneo kupimwa sio ufamizi (trespass to land) uvamizi unatokea pale ambapo aliyepima akianza kuwapa umiliki watu wengine (third party).

Sent using Jamii Forums mobile app

NB: The Town and Country Planning Ordinance. Cap. 378 ILISHAFUTWA NA KIFUNGU CHA 80 CHA SHERIA NA. 8-2007. (haitumiki tena, ni repealed law)
Ubarikiwe sana.
 
may God bless you, ur far too kind, and i like you anyway.... kutoa maarifa bure sio jambo la kila mmoja.
 
MSAADA MSAADA MSAADA MSAADA

Habari za muda huu kwa mara nyingine tena

Natafuta kazi ndugu zangu watanzania wenzangu

Ata kama uta-nidalalia iyo kazi tutaelewana malipo ndugu yangu

naombeni msaada wenu mwenye kuweza kunisaidia, maana nimeshaangaika sana kutafuta kazi ila naambulia patupu

Nimezunguka sana kwenye viwanda, site za ujenzi ila naambuliwa patupu, naombeni msaada wenu, ata kama nitapata kazi ya ku-volunteer tuu, pia ntashukuru sana ndugu zangu...

Maana umri pia unakimbia, nisaidieni sana

Elimu yangu: Degree

Fani: CYBER SECURITY (ULINZI NA USALAMA WA MIUNDOMBINU YA TEKNOLOJIA)

Other Award: Diploma in computer science (SAYANSI YA KOMPUTA)

Na nimekuwa mbobezi katika mambo ya

》Penetration Testing, kutafuta vulnerabilities, kufanya sniffing, exploits & tools, nina uelewa wa kutosha kuhusiana na social engineering

》ku-secure system kwa kutumia linux, DNS, na kwa kutumia cryptography

》ku-secure connectivity kama vile switch, router, firewalls, vpn, ips(intrusion prevention system ) pamoja na ids (intrusion ditectin system) nadhani wataalum watakuwa wamenielewa kwenye ivyo vifupo

》Digital forensics inverstigation (computer pamoja na simu)

》Computer Networking

》 System analysis and design

MSAADA WENU WAUNGWANA

MPAKA NIMEAMUA KUWAANGUKIA NDUGU ZANGU MNISAIDIE UJUE NIMESHAKATA TAMAA, MAANA

KULIKO KULIA PEKE YANGU, NIMEONA NIWALILIE WATANZANIA WENZANGU MNISAIDIE NDUGU ZANGU

NIMESHATAFUTA SANA KAZI, KUANZIA APPLICATION ZA ONLINE, MPAKA MANUALLY

NOTE: KAZI YEYOTE ILE NTAFANYA ATA KAMA NI NJE YA TAALUMA YANGU, NA NTAIFANYA KWA UAMINIFU MKUBWA MNO

MUNGU WABARIKI SANA

NO YANGU: 0755836347
NAPATIKANA: DSM-MBEZI MSAKUZI

NISAMBAZIENI KWENYE MA-GROUP MENGINE NIPATE MSAADA
Please. Ripoti kituo cha karibu cha polisi. Hawa polisi wana upungufu mkubwa sana kwenye haya mambo hasa kwenye digital forensics. Are you still looking for a job?
 
Nifanyaje ili hati yangu ya kimila iwe valid mahakamani in case kuna chochote kimetokea?
Eneo tuseme halijapimwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna kitu ambacho watu huwa wanachanganya kati ya HATI ya manunuzi, na HATI YA UMILIKI WA ARDHI YA KIMILA. Je wewe una hati ya kuuziana eneo (Ambayo kimsingi sio hati ni MKATABA kati ya muuzaji na mnunuzi) ama una hati ya kimila ya umiliki wa Ardhi?.

Umiliki wa Ardhi wa kimilia una njia mbili yaan:-

1. Umiliki wa kuwa na CHETI cha kumiliki Ardhi kilichotolewa na Halmashauri ya Kijiji (Certificate of customary right of Occupancy/CCRO)

2. Umiliki wa kimilia wa bila chati, kwa kuwa Ardhi umekuwa ikitumiwa na ukoo/familia kwa muda mrefu (Deemed Right of Occupancy/DRO)

Je wewe unamiliki kwa mfumo upi?, ili nikujibu kwny target.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimenunua kiwanja mwaka 2007 kupitia wakili na nikajenga ndani ya miezi 2 nikahamia.mwaka Jana ndugu ya aliyeniuzia wanakuja kudai kwamba ndugu yao(marehemu) ajaniuzia na wana documents zote za kiwanja na mm ninazo za kwangu ila zinafanana na za kwao.hivi kuna uwezekano wa kudhurumiwa?
 
Mosi, planning area ni eneo ambalo limeingizwa kwny mipango ya matumizi kupitia mfumo wa ramani/mchoro ikizingatia huduma za kijamii. Eneo hili linaweza kuwa la makazi, makazi na biashara, biashara ama viwanda, makaburi n.k. Utaratibu huu usimamiwa na sheria ya mipango miji Na. 8-2007.

Pili, Eneo kama likitwaliwa na serikali kwa ajili ya matumizi ya umma kama vile shule, Disp, Office n.k hutwaliwa kwa utaratibu wa sheria ya utwaaji Ardhi sura ya 118 (angalia kifungu cha 4) na utalipwa fidia kama ilivyo kwny katiba ibara ya 24(2) na sheria ya ardhi Na. 4/1999 kifungu cha 3 (g).

Tamati, eneo kupimwa sio kutwaliwa hapana. Kutwaliwa ni utaratibu mwingine. Napia eneo kupimwa sio uvamizi (trespass to land) uvamizi unatokea pale ambapo aliyepima akianza kuwapa umiliki watu wengine (third party).

Sent using Jamii Forums mobile app

NB: The Town and Country Planning Ordinance. Cap. 378 ILISHAFUTWA NA KIFUNGU CHA 80 CHA SHERIA NA. 8-2007. (haitumiki tena, ni repealed law)
Mkuu shukrani kwa ufafanuzi wa jambo hili
Upimaji (uwingi au upamoja ni zoezi na mpango mzuri) unakuondolea usumbufu lakini ukija kwenye zoezi la UMILIKI wa VIWANJA/MAENEO ni mtihani mkubwa
Mfano mzuri ni ule wa mipango miji Kigamboni na Makongo Juu kuna usumbufu wilayani. Shughuli zote zilitekelezwa kupitia serikali za mitaa na kuahidiwa ndani ya Miezi sita kila mtu atapata hati huu ni mwaka wa tatu ni kusumbuliwa tu. Malipo yote yalifanyika sasa ukienda wilayani (Kinondoni) wanasema uende Wizarani kwamba Wilayani hakuna ramani hakuna viwanja kwenye Armani. Ni mwaka wa tatu sasa hakuna hati Wakazi wanashindwa kujua nini Kifuate!
*Mh Lukuvi watu wa ardhi wanaumiza sana watu
 
Back
Top Bottom