Happybirthday ben saanane

mpalu

JF-Expert Member
Sep 15, 2010
2,521
870
Happy b day Ben Saanane kamanda mkuu aliye juu ya vitu vyote akujalie maisha marefu na yenye fanaka


images




leo ni siku ya 10958 duniani.nilizaliwa saatisa(najua maswali ni mengi kwanini jina saanane) alasari siku ya jumanne tarehe kama ya leo.


ni siku ya kipekee kwangu,namshukuru mwenyezi mungu kwa kunipa pumzi ya uhai hadi muda huu.hakika ametenda mambo makuu katika maisha yangu.sifa na utukufu ni kwake jehovah!

nawashukuru wazazi.mzee saanane na mama renath kwa malezi yenu kwangu.sina cha kuwalipa zaidi ya kuwaombea baraka za mwenyezi mungu. Mlinifundisha kuwajibika kwa maamuzi na matendo yangu mwenyewe.mlihuzunika lakini bado mlinipenda hata pale nilipotenda kinyume na mapenzi yenu.mlipotamani nisomee utawa(upadri) niliwaambia huo sio wito wangu,mliponi-descourage kujihusisha na kufutailia sana siasa nikiwa katika umri mdogo tu hasa kipindi cha uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini kenya mwaka 1992 nilitoroka na kuhamia kwa majirani kwa ajili ya kusikiliza redio tu.hamkupenda kabisa niwe karibu na redio kipindi cha jioni hasa kipindi cha dira ya dunia bbc au kipindi cha afrika wiki hii dw-bonn(sauti ya ujerumani).mlitamani niwe padri au daktari.mimi nilihusudu biashara,uchumi na siasa hasa siasa za kimataifa.niliipigania ndoto yangu hii hasa nilipojiunga na masomo ya juu.asanteni kwa kunipa msingi na malezi bora.mmekua nanga yangu nilipopigwa na dhoruba katika siku hizi 10958

ndugu jamaaa na marafiki asanteni kwa kusimama nami katika shida na raha.mungu awape maisha marefu

walimu wangu na hasa mwalimu wangu melchior uisso alichangia kwa kiasi kisichoelezeka katika kukuza ndoto yangu hii.alikua mwalimu wangu wa somo la uraia darasa la sita,kiingereza darasa la tano(alinifanya nipende lugha ya kiingereza),alinifundisha historia darasa la saba na kuchochea kiu na ndoto yangu ya kile ninachokipenda.kwa bahati mbaya mwalimu wangu huyu alifariki nikiwa masomoni nje ya nchi.mwenyezi mungu ampumzishe mahali pema peponi.amen

my facebook family,you are always the best.

leo nitasheherekea siku yangu kwa kufanya shughuli za kijamii hospitali ya madonna kwa dakika 30 na pia dakika 95 kwa heshima ya maombolezo ya mzee nelson mandela.nawashukuru makamanda wote mlioniunga mkono katika zoezi hili.

now.....

to my creator,

my father and my lord, i cannot praise you enough. Your kindness and goodness amazes me. You have loved me more than ever. Despite my unfaithfulness, you have been faithful.

i sleep and wake up daily. Never has a day goneby without me having food on my table. The noisome pestilence day and night have not devoured me. Who am i to deserve such magnanimity? It is your will that i am in my present position not my expertise nor my strength nor my might.

i know your thoughts towards me which are of good and not of evil to give me an expected end. Your promises for my life serve as a shield in all my endeavours.

your holy spirit has been my guide. Even when i miss-walk, you are there to redirect my path.
lord i want to love you more. Grant me the grace to always do that.

my father do not allow the stones or leaves to praise you in my stead.

bless my facebook friends who knows the importance of showing praise and appreciation for even those little things that we overlook daily. Bless everyone that is looking unto you for an intervention today.

i bless you lord. Accept my praise oh lord and do not look at my iniquities.

thank you lord.
your son,
ben saanane

CC. Madam B Mamndenyi chama Ritz TUNTEMEKE Baba V Simiyu Yetu FaizaFoxy Sixgates Zitto mtela
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom