Happy Fathers day

Majighu2015

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
2,924
3,904
Leo ni siku ya wababa duniani. Baba ni nguzo muhimu sana kwenye familia naamini mlio wengi mmefanikiwa kwa baba zenu kuwa bega kwa bega na nyie. Pale ulipokosea baba alikuchapa ili akili ikae vizuri na kukusaidia pale ulipokwama ili malengo yako yatimie. Namshukuru sana baba yangu kwa support yake aliyonipa mpaka kifika hapa nilipo. Tuwaombee wababa wote wazidi kuwa vichwa katika familia zao ili ziweze kusonga mbele.
Unampa neno gani baba yako katika siku hii muhimu kwake.

HAPPY FATHERS DAY
 
1466349390183.jpg
 
Asante Mungu kwa ajili ya baba yangu (R.I.P) my super hero sababu uliyonifanyia siwezi kukulipa, ninatamani Mungu angekuweka weka niendelee kufaidi hekima zako, Mungu wabariki akina baba wote, wakumbushe kutimiza wajibu wao katika familia zao.
 
Tangu nijielewe kila mwaka siku kama ya leo ilikuwa ni lazima nitoke nae tunapiga story mbili tatu kuhusu maisha lakini mwaka huu hayupo tena RIP baba yangu kipenzi nilikupenda sana na ninakukosa sana.
 
Siku ya baba Dunian" Hongereni wenye ma baba sijawahi hata kula mboga aliyonunua baba " Lov u en hate u papaaaa
Kula mboga aliyonunua baba is not a big deal. At some point kwenye maisha yangu ilinitokea hiyo tena sio masuala ya kula tu hata issue za kusoma lakini mpaka sasa siwezi kumlaumu baba akati mimi bado sijawa baba wala sina familia. Kuna changamoto kubwa sana zinawakuta wazee wetu na sio kwamba eti alikuwa anaamua tu kutokuhudumia familia. Kulifaham hilo lazima kwanza uje kuwa na familia. Ila for now be patient bro.
 
Kula mboga aliyonunua baba is not a big deal. At some point kwenye maisha yangu ilinitokea hiyo tena sio masuala ya kula tu hata issue za kusoma lakini mpaka sasa siwezi kumlaumu baba akati mimi bado sijawa baba wala sina familia. Kuna changamoto kubwa sana zinawakuta wazee wetu na sio kwamba eti alikuwa anaamua tu kutokuhudumia familia. Kulifaham hilo lazima kwanza uje kuwa na familia. Ila for now be patient bro.
Anacho maanisha baba alikataa majukumu ya ubaba juu yake kwahyo hata mboga y mchicha 200 ilimshinda / hakuitoa.
 
Tangu nijielewe kila mwaka siku kama ya leo ilikuwa ni lazima nitoke nae tunapiga story mbili tatu kuhusu maisha lakini mwaka huu hayupo tena RIP baba yangu kipenzi nilikupenda sana na ninakukosa sana.
RIP baba..Sote tunaelekea huko mkuu. Enzi mema yake maisha yaendelee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom