Display Name
JF-Expert Member
- Feb 11, 2014
- 423
- 451
Leo ni birthday ya aliyewahikuwa Rais wa Zimbabwe, Robert G Mugabe. Tujikumbishe machache kuhusu yeye.
Robert G Mugabe alizaliwa tarehe 21/2/1924 huko Kutama, Southern Rhodesia ambayo kwa sasa ndio Zimbabwe. Alisoma Kutama Collage na baadae University of Fort Hare, lakini pia alishawahi kuwa mwalimu huko Zimbabwe na Ghana pia.
Mugabe ni mwanasiasa na mwanamapinduzi wa Zimbabwe na alishawahi kuwa Mwenyekiti wa chama cha ZANU mwaka 1975-1980 na kuwa Makamu wa Rais mwaka 1980-1987, wakati huo Rais wa Zimbabwe alikuwa anaitwa Canaan Banana chini ya chama kilichojulilana kama ZANU.
Robert G Mugabe alikuwa Rais wa Zimbabwe mwaka 1987-2017, chini ya chama cha siasa kinachojulikana kama ZANU-PF, hii ni baada ya kuunga chama cha ZAPU(Zimbabwe African People's Union) na ZANU(Zimbabwe African National Union).
Zimbabwe ilipata Uhuru wake tarehe 18/4/1980 kutoka kwa mkoloni wake ambaye ni Muingereza. Hivyo Mugabe ni Rais wa pili wa Zimbabwe na aliondolewa madarakani mwaka 2017 na kwa sasa Rais ni Emmerson Mnangagwa ambaye alikuwa Makamu wa Rais wakiti Mugabe akiondolewa madarakani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Robert G Mugabe alizaliwa tarehe 21/2/1924 huko Kutama, Southern Rhodesia ambayo kwa sasa ndio Zimbabwe. Alisoma Kutama Collage na baadae University of Fort Hare, lakini pia alishawahi kuwa mwalimu huko Zimbabwe na Ghana pia.
Mugabe ni mwanasiasa na mwanamapinduzi wa Zimbabwe na alishawahi kuwa Mwenyekiti wa chama cha ZANU mwaka 1975-1980 na kuwa Makamu wa Rais mwaka 1980-1987, wakati huo Rais wa Zimbabwe alikuwa anaitwa Canaan Banana chini ya chama kilichojulilana kama ZANU.
Robert G Mugabe alikuwa Rais wa Zimbabwe mwaka 1987-2017, chini ya chama cha siasa kinachojulikana kama ZANU-PF, hii ni baada ya kuunga chama cha ZAPU(Zimbabwe African People's Union) na ZANU(Zimbabwe African National Union).
Zimbabwe ilipata Uhuru wake tarehe 18/4/1980 kutoka kwa mkoloni wake ambaye ni Muingereza. Hivyo Mugabe ni Rais wa pili wa Zimbabwe na aliondolewa madarakani mwaka 2017 na kwa sasa Rais ni Emmerson Mnangagwa ambaye alikuwa Makamu wa Rais wakiti Mugabe akiondolewa madarakani.
Sent using Jamii Forums mobile app