Baraka Mina

JF-Expert Member
Sep 3, 2020
581
574
Mnamo tarehe 27 Januari 1960 Rais wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. Samia Suluhu Hassan alizaliwa huko Makundichi Zanzibar.

Leo anatimiza umri wa miaka 62. Ni Rais wa kwanza mwanamke nchini kwetu na mfano wa kuigwa kwa wasichana, wanawake na watu wa rika na jinsia mbalimbali kwa namna moja ama nyingine.

Tunaamini kuwa leo asubuhi 27 Januari 2022 Saa 12:00 Asubuhi - 03:00 Asubuhi kupitia mahojiano maalum katika kipindi cha Jambo Tanzania katika Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) utakuwa na mengi ya kutueleza yakuhusuyo wewe, maendeleo endelevu ya nchi yetu na mustakabali bora wa nchi yetu pendwa ya Tanzania.

Tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu awe nawe katika uongozi wa awamu ya sita, akujalie afya njema, furaha, maisha marefu na nguvu za kuwatumikia watanzania bila kuchoka wala kukatishwa tamaa katika kuhakikisha taifa hili linapata maendeleo.

Heri ya Kumbukumbu ya Siku ya Kuzaliwa Rais wetu na daima Kazi Iendelee.

IMG-20210324-WA0123.jpg

IMG-20211106-WA0018.jpg
 
Hepi bethidei mama yetu, unafanya vizuri kwa Tanzania, ningependa kutumia nafasi hii kukupongeza pia Mungu akupe miaka mingi zaidi tushuhudie utukufu wake kupitia kwako..Amen
 
HONGERA KWAKE, But ni anajiandaa kwenda mkoani Mara, awaulize watendaji kuhusu hii...

 
Shida Ni kubariki kesi ya kigaidi bila facts.Una nafasi nzuri kuruhusu mchakato kuboresha Katiba pendekezwa ya wananchi na sio draft ya CCM.Happy birthday Madame Presida.
Kishalewa madaraka, bado ana nafasi lakini milango itafunga soon na atakuja kujuta
 
Mauaji yanayojitokeza nchini, polisi dhidi ya raia, raia kwa raia, watoto kuua wazazi n.k Ni mwitikioa wa kuiga tabia ya serikali kuonea, kutesa, kuteka, kubambikia kesi na kuua watu wake.

Happy birthday day kwako SSH...Urais si lelemama. Sio kila mtu anaweza
 
Shida Ni kubariki kesi ya kigaidi bila facts.Una nafasi nzuri kuruhusu mchakato kuboresha Katiba pendekezwa ya wananchi na sio draft ya CCM.Happy birthday Madame Presida.
Tatizo la Mbowe sijui hiyo katiba mpya alikua ana haraka nayo ya nini kwenye awamu hii, katiba ya zamani haifutwi sasa unadhani hiyo mpya wata ifuata? Nadhani Mbowe ana taka madaraka tu.

Kingine ni kwamba alikua ana pima kina cha maji, wakati wa Magu alikua kimya.
Namuombea atoke ili aendeshe siasa za kistaarabu.
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom