HAPPY BIRTH DAY Frédéric Chopin;

Steven Sambali

JF-Expert Member
Jul 31, 2008
352
170
Frédéric Chopin.Frédéric Chopin (jina la Kipoland: Fryderyk ; 22 Februari, 1810 kulingana na cheti cha kuzaliwa - 17 Oktoba, 1849; pengine, tarehe 1 Machi au 10 Machi zimetajwa kama siku yake ya kuzaliwa) alikuwa mtunzi wa Opera na mpigaji kinanda mashuri kutoka nchini Poland. Ni mtunzi muhimu kabisa kwa nchi ya Poland. Ingawaje kuna baadhi ya tungo zake zilikuwa vigumu sana kuzipiga, na zilibahatika kuwa moja kati ya tungo zilizowahi kutungwa vema.

Alizaliwa katika kijiji kidogo cha Żelazowa Wola karibu na Warshava wakati sehemu ile ilikuwa chini ya utawala wa Urusi. Baba alikuwa Nicolas Chopin Mfaransa aliyeishi Poland kama mwalimu na mamake Justyna Krzyżanowska aliyetoka katika familia ya makabaila maskini wa Poland. Frederic alianza mapema kupiga kiananda akaonyesha uwezo mkubwa. Alipofikia umri wa miaka 20 alisafiri Ufaransa alipotoa maonyesho ya muziki yake. 1830 baba alimshauri asirudi Poland kwa sababu ya uasi wa Wapoland dhidi ya utawala wa Kirusi. Baada ya kukandamizwa kwa uasi huu Frederic alibaki nje ya nchi yake ya kuzaliwa akaendelea kuishi na kufanya kazi mjini Paris hasa.

Ni hapa Paris ya kwamba alikuwa maarufu kama mtunga muziki. Alianzisha mapenzi na wanawake mbalimbali lakini hakubahatika kufunga ndoa. Afya yake ilikuwa hafifu muda wote akafa mjini Paris kwa sababu ya ugonjwa wa kifua kikuu mwaka 1849 akiwa na umri wa miaka 39 pekee. Alizikwa Ufaransa lakini moyo wake ulipelekwa Poland na kuzikwa huko katika kanisa mjini Warshava.

From Wikipedia: http://sw.wikipedia.org/wiki/Frédéric_Chopin

Hii video hapa chini ni mashindano ya Chopin hapa Warshava mwaka 1995 ambapo kijana wa Kirusi aitwaye Alexei Sultnov (RIP) alipiga kijanda hadi nikampenda ingawa sikuwa mpenzi wa Chopin. Ila kwa jambo ambalo hadi leo sielewi, walikataa kutoa nafasi ya kwanza na wakasema wawili wameshika nafasi ya pili. Sultanov aliikataa nafasi ya pili kwani aliamini (wengi tuliamini) kuwa alikuwa kapata nafasi ya kwanza.

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=Yps4hKjt8cE"]YouTube- Alexei Sultanov -Warsawa Recital part.4,Chopin Fantasie Impr[/ame]
 
Leo hii hapa Warsaw (Warszawa au Warshava) wamefungua jumba la makumbusho la huyu Chopin katika kusherehekea miaka 200 tangu kuzaliwa kwake. Jumba hilo limefanywa la kisasa saaana kiasi kwamba kweli lipo karne ya 21. Mfano kuna sehemu ukiweka kitabu che NUTA za mziki wa Chopin, basi kinanda kinajipiga chenyewe.

Kwenye lile jumba la Thieta ambalo kama sikosei ndiyo la taifa na kubwa kuliko yote, kuna concert kubwa sana na wamekuja wapiga vinanda wengi maarufu duniani. Nafikiri bei yake haitakuwa nzuri sana kwa walalahoi.

http://blog.taragana.com/e/2010/03/...posers-home-city-on-his-200th-birthday-95461/
 
aminia kaka unajua kumchambua huyu jamaa...duh heko yake na mungu amlaze mahali pema peponi...Wapolo wabaguzi ndo maana hawakumpa Mrusi ....
 
aminia kaka unajua kumchambua huyu jamaa...duh heko yake na mungu amlaze mahali pema peponi...Wapolo wabaguzi ndo maana hawakumpa Mrusi ....


Mkuu, nisingelipenda sana kutumia neno WABAGUZI. Ni kweli wana mapungufu yao ingawa tangu waingie EU kwa sasa wanabadilika sana. Timu zao zimejaa weusi kibao na moja ya timu maarufu hapa Poland/Warsaw iitwayo LEGIA, moja ya ma-Captain wa timu hiyo ni jamaa aitwaye Dickson Chotto ambaye pia ni beki wa timu ta Taifa ya Zimbabwe. Pia kama ulimuona Kalu Uche huko Angola, jamaa kachezea sana hapa Poland, mji wa Krakow na baadaye akahamia hapa Warsaw.

Nirudie tena kuwa ni kweli wanamapungufu yao ila kwa sasa wanabadilika sana. Kwa mfano zamani ukipata kesi na Mpolish basi una hali mbaya. Ila tangu waanze kushtakiwa kwenye mahakama ya Ulaya na kushindwa kesi karibu zote na hapo kulipa fidia kubwa sana, wameanza kuwa wakali na waangalizi wa sheria. Nimeshashuhudia club, Mweusi karuhusiwa kuingia na Mpolish kakataliwa na sababu eti jamaa ni MREFU.
 
sasa kwa nini hakupewa kuwa mshindi na jamaa ni mkali sana hata ukiangalia Wikipedia anatoboa kweli lkn poa poa..RIP alex..
 
sasa kwa nini hakupewa kuwa mshindi na jamaa ni mkali sana hata ukiangalia Wikipedia anatoboa kweli lkn poa poa..RIP alex..

Magulumangu,
Ni kweli kijana Alex alikuwa mkali sana na alizibeba roho za Wapolish wengi. Tatizo ni kuwa ile kamati ya maandalizi na usimamizi wa hayo mashindano pamoja na hivyo vizee Vi-Profesa vya mziki, ndiyo vilikuwa vikoministi na roho korosho sana. Vilikasema eti hakuna mtu aliyefikia upigaji wa juu hadi apewe nafasi ya kwanza. Ilikuwa kichekesho kwa sababu walikuwa wanashindanishwa watu na si watu wanashindana kufikia usawa fulani.

Huyu kijana Alex alikuwa ni Chain Smoker mkubwa sana. Alikuja kuuguwa sifahamu hadi leo ni nini kwa sababu sikufuatilia sana ila kuna wale Wapenzi wake hapa Poland walikusanya hela ili zipelekwe Russia zimsaidie katika matibabu. Labda ndiyo uzuri na ubaya wa mambo mengine kwani kama si kudhurumiwa ushindi, labda tungelikuwa tumeshamsahau.

Wafaransa nao wamesherehekea Bday ya Chopin:
http://www.english.rfi.fr/culture/20100301-paris-celebrates-chopins-birthday
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom