Hapo Ulipo Upo?

Mwendabure

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
2,138
1,040
Balungwana Kwema?
Huku kwetu Wilaya mpya ya Mbagala Tanesco wamechukua umeme wao tangu saa 10 jioni, baada ya kutuzuga na umeme wa sikukuu ya Idd. Je hapo ulipo bado umeme upo? Tujuzane ili tulie wote msiba huu usiokwisha.
Karibu!
 
kwetu ulichukuliwa kama dk 45 wameurudisha kwa hiyo sasa hivi poa tu..
 
afadhali wameuchukua tu mana tulikuwa tunaishi kwa wasiwasi kweli. waswahili wanasema "kawaida ni kama sheria"
 
Mie nilirudi nyumbani jioni sikuukuta ila wamerudisha kama saa moja hivi....
 
Kumbe mgao upo mijini tu. Mimi nilikuja huku Mang'ula- Kilombero-Morogoro tangu J3 mpaka leo J1 umeme haujakatika na nilipouliza kama wanapata mgao wakanambia mgao ni huko mijini huku hawajui mgao. Nimeshindwa kuelewa ni kwa nini.
 
kwetu wanaogopa kuukata.............
kila siku upo, mi mfawo huwa nausikilizia kwenu tu.:peace:
 
jamani hapa ukerewe umeme hamna kama siku tatu,tumewagasi tanesco wamesema eti waya wa umeme unaopita chini ya ziwa umeliwa na mamba hadi kukatika.nashangaa hamna mamba aliyepigwa shoti wala kizilai.lakini hiyo sehemu wanayosema kuna mamba kweli na ukienda mida ya saa nne asubuhi anawaona wameota jua.sasa tanesco walijuaje pale waya umekatika?.mimi sijaamini.mia
 
kwetu wanaogopa kuukata.............<br />
kila siku upo, mi mfawo huwa nausikilizia kwenu tu.<img src="/images/styles/JamiiForums/smilies/peace.gif" border="0" alt="" title="Peace" smilieid="238" class="inlineimg" />
<br />
<br />
mmh FB Bosi wa tanesco anakaa mtaani kwenu nini?
 
Back
Top Bottom