Kivuli cha Karamagi: Wabunge waukataa muswada wa umeme, mafuta
*Wakataa muswada wa sheria ya umeme
*Wasema hauna maslahi kwa taifa
Na Waandishi Wetu
WABUNGE wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wameukataa kwa mara nyingine muswada wa sheria ya umeme, wenye lengo la kufungua milango kwa wawekezaji wa nje kuwekeza katika sekta hiyo badala ya huduma hiyo kutolewa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pekee.
Wakizungumza katika semina ya siku mbili iliyofanyika jijini Dar es Salam jana, wabunge hao walionyesha kukerwa na muswada huo, wakidai kuwa bado una harufu ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi.
Akizungumza mara baada ya kuwasilishwa kwa mada mbalimbali zinazohusu muswada huo, Mbunge wa Karatu, Dk Willibroad Slaa ( Chadema) alisema hajaona tofauti yoyote katika muswada huo na uliowasilishwa mara ya kwanza, ambao ulipitiwa na kutoa mapendekezo ya mabadiliko katika baadhi ya vipengele.
Aliongeza kuwa mswada huo pia hauonyeshi mpango wowote wa kuweka umeme maeneo ya vijijini ambako ndiko kuna wananchi wengi.
"Mswada ni ule ule na umesainiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, sijaona mabadiliko licha ya tulipoupitia Dodoma kutoa mapendekezo ya sehemu za kuufanyia mabadiliko. Pia umeshindwa kutoa dhamana ya mpango wa kuendeleza umeme vijijini,"alisema Dk Slaa.
Aliangaliza kuwa hakuna kwa sasa kampuni yoyote ya uwekezaji inayoweza kupeleka umeme vijijini, hivyo aliitaka serikali kuhakikisha kuwa inatekeleza jukumu hilo yenyewe na kuongeza kuwa kuukubali mswada huo ni sawa na kuiweka nchi mikononi mwa wawekezaji.
"Sijawahi kuona nchi yoyote duniani inayobinafsisha sekta ya umeme, Tanzania tumeamua kutoa mali zetu kiholela. Hii ni aibu tunawanyenyekea wawekezaji na hatima yake tunajikuta tunaingia kwenye mikataba mibovu. Naomba tuisaidieTanesco ili iweze kujiendesha...," alisema Dk Slaa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Anne Kilango alisisitiza kuwa hawezi kuukubali muswada huo kwa sababu una mapungufu mengi na kwamba hauna maslahi kwa wananchi.
"Mwenyekiti naomba niukatae muswada huu kwa mara ya pili, awali mjini Dodoma niliukataa bila kutoa sababu, sasa nimefanya utafiti nimeandika mada nikilinganisha na mataifa mengine, ambayo nitaiwasilisha kwenye Kamati za Kudumu za Bunge," alisema na kuongeza:
"Tuionee huruma Tanesco, sisi ndio tumeifikisha hapo ilipo, "halafu tunataka kumletea Tyson apigane na mtoto wetu wa miaka 10 ambaye ni mgonjwa mahututi akiwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi'. Hii ni sawa na kukubali mtoto wako auawe, sisi ni wazazi gani tusio na huruma".
Alimtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kutoyakanyaga maneno yake aliyotoa mara baada ya kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo ili kuinusuru Tanesco.
Alisema Waziri Ngeleja aliahidi jambo la kwanza kulishughulikia atakapo ripoti kazini ni suala la Tanesco, hivyo ni wakati muafaka wa kushughulikia suala hilo badala ya kuwashawishi wabunge wapitishe muswada huo ambapo hauna maslahi kwa wananchi.
"Tunataka ushindani lakini si sasa muda haujafika kuruhusu utokee katika sekta ya umeme," alisisitiza Kilango.
Awali Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Halima Mamuya alieleza kusikitishwa kwake kwa serikali kuwatumia wabunge kuwapa posho kwa kuandaa semina zenye lengo la kuwashawishi kupitisha vitu ambavyo havina maslahi kwa wananchi.
Alisema serikali imekuwa na kawaida ya kuandaa semina na kuwapa wabunge posho ya Sh 80,000 kisha kuwaletea vitu mbalimbali ikiwamo miswada muhimu inayogusa maslahi ya wananchi, ili wabunge hao wayapitishe na kutoa mfano wa semina kama hiyo iliyowahi kususiwa mjini Dodoma ambapo alisema siku hiyo walipewa posho hiyo, lakini baada ya kususia semina hiyo, aliyekuwa waziri wa nishati na madini alitamka wazi na kuhoji kwanini walichukua posho zao wakati waliisusia semina hiyo.
"Muheshimiwa mwenyekiti, mimi nilinyanyasika sana, maneno haya yananikera siku ile wabunge tuliandaliwa semina kama hii, wakati tunaingia tu mlangoni waandaaji walitusainisha posho na kutuletea miswada hiyo siku hiyo hiyo, hatukuwa na muda wa kuisoma hivyo walifikiri tungepitisha hivi hivi,"alisema.
"Lakini baada ya mambo kubadilika, waziri alisema kwanini tumechukua posho zao wakati tumeisusia semina yao, niliirudisha pesa ile, lakini walikataa kupokea na badala yake walisema niipeleke kwa watoto yatima, huu ni unyanyasaji mkubwa."
Mamuya alisema muda wa wabunge kutumiwa kwa posho za vikao umepitwa na wakati, badala yake serikali ibadilike kwani sasa ni enzi ya Watanzania kujua mambo na si enzi ya kupitisha mambo kwa maslahi ya wachache.
Naye Mbunge wa Nkasi CCM, Ponsiano Nyami alisema kuwa suala la umeme kufika maeneo ya vijijini mara baada ya wawekezaji kuingia katika sekta hiyo, ni kiini macho na ni sawa na kuwadanganya wananchi ambao wamekuwa wakiteseka kwa miaka mingi kusubiri huduma hiyo.
Aliishauri serikali kuacha kutegemea umeme unaotokana na maji kwa kuwa sasa hauna uhakika kutokana na hali ya hewa kutoeleweka.
Semina hiyo ilihudhuriwa na wabunge wote pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye alifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mkuu Tanesco, Dk Idrisa Rashid, Mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco, Balozi Fulgence Kazaura, maafisa mbalimbali kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Maji (Ewura), pamoja na maafisa mbalimbali wa serikali.
Source: Mwananchi
Maswali ya ziada:
Kwanini bado wanarudisha mswada ule ule ambao ulisainiwa na Waziri Karamagi? Kuna watu wana kampuni zao wanataka kuja kuinunua TANESCO? Au kuna watu serikalini walishakula mshiko (10%) ili kuhakikisha kwamba kampuni fulani zinapata upenyo wa kuingia Tanzania kuja kuwekeza kwenye umeme? Maswali ni mengi kuliko majibu.
Waziri Ngereja asipokuwa makini anaweza kujikuta anamfuata Karamaji kwa kuwa hiyo wizara ni bomu kwa sasa na inagusa sekta ambazo ziko sensitive kwa wananchi. Kazi kwake na ninamtakia kila la heri!
Mama Kilango mfano wa kuigwa na ndiyo tunataka wabunge wanaokwenda na dataz ili kuiumbua serikali inapokurupuka halafu baadaye inakuja kusukumia mzigo kwa washauri/wasaidizi kwamba hawakutoa ushauri unaofaa. Nina uhakika mikataba mibovu tuyoiona leo hii isingeweza kupitishwa kama ingekuwa inapitia Bungeni na wala akina Lowassa wasingepata nafasi ya kujitetea kwamba hawakushauriwa vizuri!
*Wakataa muswada wa sheria ya umeme
*Wasema hauna maslahi kwa taifa
Na Waandishi Wetu
WABUNGE wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wameukataa kwa mara nyingine muswada wa sheria ya umeme, wenye lengo la kufungua milango kwa wawekezaji wa nje kuwekeza katika sekta hiyo badala ya huduma hiyo kutolewa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) pekee.
Wakizungumza katika semina ya siku mbili iliyofanyika jijini Dar es Salam jana, wabunge hao walionyesha kukerwa na muswada huo, wakidai kuwa bado una harufu ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi.
Akizungumza mara baada ya kuwasilishwa kwa mada mbalimbali zinazohusu muswada huo, Mbunge wa Karatu, Dk Willibroad Slaa ( Chadema) alisema hajaona tofauti yoyote katika muswada huo na uliowasilishwa mara ya kwanza, ambao ulipitiwa na kutoa mapendekezo ya mabadiliko katika baadhi ya vipengele.
Aliongeza kuwa mswada huo pia hauonyeshi mpango wowote wa kuweka umeme maeneo ya vijijini ambako ndiko kuna wananchi wengi.
"Mswada ni ule ule na umesainiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, sijaona mabadiliko licha ya tulipoupitia Dodoma kutoa mapendekezo ya sehemu za kuufanyia mabadiliko. Pia umeshindwa kutoa dhamana ya mpango wa kuendeleza umeme vijijini,"alisema Dk Slaa.
Aliangaliza kuwa hakuna kwa sasa kampuni yoyote ya uwekezaji inayoweza kupeleka umeme vijijini, hivyo aliitaka serikali kuhakikisha kuwa inatekeleza jukumu hilo yenyewe na kuongeza kuwa kuukubali mswada huo ni sawa na kuiweka nchi mikononi mwa wawekezaji.
"Sijawahi kuona nchi yoyote duniani inayobinafsisha sekta ya umeme, Tanzania tumeamua kutoa mali zetu kiholela. Hii ni aibu tunawanyenyekea wawekezaji na hatima yake tunajikuta tunaingia kwenye mikataba mibovu. Naomba tuisaidieTanesco ili iweze kujiendesha...," alisema Dk Slaa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Anne Kilango alisisitiza kuwa hawezi kuukubali muswada huo kwa sababu una mapungufu mengi na kwamba hauna maslahi kwa wananchi.
"Mwenyekiti naomba niukatae muswada huu kwa mara ya pili, awali mjini Dodoma niliukataa bila kutoa sababu, sasa nimefanya utafiti nimeandika mada nikilinganisha na mataifa mengine, ambayo nitaiwasilisha kwenye Kamati za Kudumu za Bunge," alisema na kuongeza:
"Tuionee huruma Tanesco, sisi ndio tumeifikisha hapo ilipo, "halafu tunataka kumletea Tyson apigane na mtoto wetu wa miaka 10 ambaye ni mgonjwa mahututi akiwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi'. Hii ni sawa na kukubali mtoto wako auawe, sisi ni wazazi gani tusio na huruma".
Alimtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kutoyakanyaga maneno yake aliyotoa mara baada ya kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushika wadhifa huo ili kuinusuru Tanesco.
Alisema Waziri Ngeleja aliahidi jambo la kwanza kulishughulikia atakapo ripoti kazini ni suala la Tanesco, hivyo ni wakati muafaka wa kushughulikia suala hilo badala ya kuwashawishi wabunge wapitishe muswada huo ambapo hauna maslahi kwa wananchi.
"Tunataka ushindani lakini si sasa muda haujafika kuruhusu utokee katika sekta ya umeme," alisisitiza Kilango.
Awali Mbunge wa Viti Maalumu kwa tiketi ya Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Halima Mamuya alieleza kusikitishwa kwake kwa serikali kuwatumia wabunge kuwapa posho kwa kuandaa semina zenye lengo la kuwashawishi kupitisha vitu ambavyo havina maslahi kwa wananchi.
Alisema serikali imekuwa na kawaida ya kuandaa semina na kuwapa wabunge posho ya Sh 80,000 kisha kuwaletea vitu mbalimbali ikiwamo miswada muhimu inayogusa maslahi ya wananchi, ili wabunge hao wayapitishe na kutoa mfano wa semina kama hiyo iliyowahi kususiwa mjini Dodoma ambapo alisema siku hiyo walipewa posho hiyo, lakini baada ya kususia semina hiyo, aliyekuwa waziri wa nishati na madini alitamka wazi na kuhoji kwanini walichukua posho zao wakati waliisusia semina hiyo.
"Muheshimiwa mwenyekiti, mimi nilinyanyasika sana, maneno haya yananikera siku ile wabunge tuliandaliwa semina kama hii, wakati tunaingia tu mlangoni waandaaji walitusainisha posho na kutuletea miswada hiyo siku hiyo hiyo, hatukuwa na muda wa kuisoma hivyo walifikiri tungepitisha hivi hivi,"alisema.
"Lakini baada ya mambo kubadilika, waziri alisema kwanini tumechukua posho zao wakati tumeisusia semina yao, niliirudisha pesa ile, lakini walikataa kupokea na badala yake walisema niipeleke kwa watoto yatima, huu ni unyanyasaji mkubwa."
Mamuya alisema muda wa wabunge kutumiwa kwa posho za vikao umepitwa na wakati, badala yake serikali ibadilike kwani sasa ni enzi ya Watanzania kujua mambo na si enzi ya kupitisha mambo kwa maslahi ya wachache.
Naye Mbunge wa Nkasi CCM, Ponsiano Nyami alisema kuwa suala la umeme kufika maeneo ya vijijini mara baada ya wawekezaji kuingia katika sekta hiyo, ni kiini macho na ni sawa na kuwadanganya wananchi ambao wamekuwa wakiteseka kwa miaka mingi kusubiri huduma hiyo.
Aliishauri serikali kuacha kutegemea umeme unaotokana na maji kwa kuwa sasa hauna uhakika kutokana na hali ya hewa kutoeleweka.
Semina hiyo ilihudhuriwa na wabunge wote pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye alifungua semina hiyo, Mkurugenzi Mkuu Tanesco, Dk Idrisa Rashid, Mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco, Balozi Fulgence Kazaura, maafisa mbalimbali kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Maji (Ewura), pamoja na maafisa mbalimbali wa serikali.
Source: Mwananchi
Maswali ya ziada:
Kwanini bado wanarudisha mswada ule ule ambao ulisainiwa na Waziri Karamagi? Kuna watu wana kampuni zao wanataka kuja kuinunua TANESCO? Au kuna watu serikalini walishakula mshiko (10%) ili kuhakikisha kwamba kampuni fulani zinapata upenyo wa kuingia Tanzania kuja kuwekeza kwenye umeme? Maswali ni mengi kuliko majibu.
Waziri Ngereja asipokuwa makini anaweza kujikuta anamfuata Karamaji kwa kuwa hiyo wizara ni bomu kwa sasa na inagusa sekta ambazo ziko sensitive kwa wananchi. Kazi kwake na ninamtakia kila la heri!
Mama Kilango mfano wa kuigwa na ndiyo tunataka wabunge wanaokwenda na dataz ili kuiumbua serikali inapokurupuka halafu baadaye inakuja kusukumia mzigo kwa washauri/wasaidizi kwamba hawakutoa ushauri unaofaa. Nina uhakika mikataba mibovu tuyoiona leo hii isingeweza kupitishwa kama ingekuwa inapitia Bungeni na wala akina Lowassa wasingepata nafasi ya kujitetea kwamba hawakushauriwa vizuri!