Hapakuwa na Tishio lolote kuelekea 2025 bali kilichokuwapo ni Huzuni ya watoto wetu kuwa nje ya system.

Hatimaye utatu mtakavitu umerejea katika ramani ya madaraka.

Ni vijana watatu waliozaliwa katika familia tatu zenye utakavitu mkubwa.

Mmoja kazaliwa njia panda ya barabara ya Morogoro na tanga, huyu hana sifa ya kuwa waziri popote duniani lakini kinachombeba ni kuwa katoka familia ya kitakavitu.

Mwingine ni mjukuu wa mchonga vinyago , huyu ni kijana mwenye majivuno na majitapo kuwa yeye genge letu lisingeingia peponi, kwani yeye alitumia siku 78 porini akifanya na kupanga mikakati ya kumpokea masihi.

Kijana mwingine ni mzaliwa wa milimani, huyu japo ni mkimya sana lakini hatari yake ni kubwa sana, ndiye wa kwanza katika watoto wetu watatu kurejeshwa katika system anahusika na kukata umeme.

The returns of the noble families childrens.

Ni mimi masikini wa kutupwa mdogo wetu manengelo bin Ruhumbika kutoka kijiji cha mwagiligili wilaya ya Kwimba....Karibuni tuvune Dengu.
Mbona Musukuma hakukumbukwa kwenye uteuzi? Kwani PhD yake haistahili uteuzi?
 
Kwa taarifa za kiintelihensia ni kuwa mama Bhoke ndiye aliyekuwa akivujisha siri za serikali kwa Kigogo. Hivyo kwa sasa Muungano wa kwe2 unaongozwa na team Kigogo
kwisa_mzee_mkavu~p~CYeJ2IntTh4~1.jpg
 
Huyu naye alitaka urais mbona naona kama vile hata haiba haipo?
... hata mimi nimeshangaa sana! Huyo aliwekwa sokoni kama makinda ya bata akafika bei na urais wapi na wapi! Kuna lingine hiyo sababu haingii akilini; most likely alikuwa anaziba nafasi za akina "their highnesses"
 
Ukweli ni kwamba kwenye issue ya kuelekea 2025 chief 'alitupiga changa la macho'/kutufunga kamba. Kati ya waliopigwa chini wote hakuna aliyekuwa tishio kwenye mbio za kuelekea 2025.
 
Back
Top Bottom