Hapakuwa na haja ya kuwaondoa wamachinga na kuvunja vibanda pembezoni mwa mji

konda msafi

JF-Expert Member
Sep 5, 2018
1,666
8,561
Kusema ukweli sioni sababu ya kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo waliokuwepo huku pembezoni mwa mji kwenye vituo vya daladala kama vile Banana, Mombasa, Gongo la mboto, Mbagala, Mbezi etc.

Huku pembezoni walikuwa wanaathiri nini mpaka mumewaondoa pia? Kuwaondoa katikati ya mji kama Posta na Kariakoo ilikuwa sahihi lakini sio huku pembezoni mwa mji ambako ndio makazi ya watu.

Viongozi jaribuni kulifikiria upya hili swala. Hawa jamaa licha ya kujipatia kipato walikuwa wanasaidia sana. Wengine hatuna muda wa kwenda sokoni kununua matunda au yale mahitaji madogo madogo tuliyokuwa tunayapata kwenye vituo vya daladala tukiwa tunaelekea nyumbani tukiwa tunatoka makazini.

Sasa hivi vituo vya daladala vimepoa sana utadhani tupo vijijini. Binafsi wafanyabiashara kwenye vituo vya daladala naona walikuwa wanaupendezesha mji na wanarahisisha sana maisha.

Badala ya kupoteza muda kwenda sokoni tulikuwa tunapata mahitaji yetu bila shida kabisa na kwa bei nafuu.

Viongozi hebu jaribuni kuliangalia hili suala kwa mapana, sioni tatizo la machinga kufanya biashara pembezoni mwa mji na zaidi ya yote sisi raia wa kawaida tunawahitaji.
 
Wanasaidia sana hawa jamaa ila hilo halihalarishi kufanya biashara maeneo ambayo si sahihi.

Kama Serikali imeamua kuwatoa sioni haja ya kufanya nusunusu. Muhimu sasa ni kuidai Serikali maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa machinga mara baada ya kuwaondoa barabarani.
 
Wanasaidia sana hawa jamaa ila hilo halihalarishi kufanya biashara maeneo ambayo si sahihi.

Kama Serikali imeamua kuwatoa sioni haja ya kufanya nusunusu. Muhimu sasa ni kuidai Serikali maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa machinga mara baada ya kuwaondoa barabarani.
Mkuu hebu jaribu kurudia kusoma nilichokiandika. Kama umenielewa basi naomba unijibu kwa niaba ya hao viongozi. Huku pembezoni mwa mji kuna shida gani kwa wamachinga kufanya biashara? Nini wanaathiri?
 
Wanasaidia sana hawa jamaa ila hilo halihalarishi kufanya biashara maeneo ambayo si sahihi.

Kama Serikali imeamua kuwatoa sioni haja ya kufanya nusunusu.... Muhimu sasa ni kuidai Serikali maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa machinga mara baada ya kuwaondoa barabarani.
Ingewatoa tu katikati ya miji. Huku pembezoni hawana madhara bali wana faida.
 
Mkuu hebu jaribu kurudia kusoma nilichokiandika. Kama umenielewa basi naomba unijibu kwa niaba ya hao viongozi. Huku pembezoni mwa mji kuna shida gani kwa wamachinga kufanya biashara? Nini wanaathiri?
Tutafute permanent solution ya hili tatizo.
Mfano pale Mbezi mwisho kutokana na kua na Wafanyabiashara barabarani kitendo cha kutoka stand ndogo mpaka Morogoro road ilikua inachukua mpaka dakika 15 au zaidi wakati kiuhalisia ni sehemu ya chini ya dakika 5.

Au sehemu nyingine ni Arusha kutoka pale friends corner mpaka round about ya Krokoni wafanyabiashara walikua wanapanga bidhaa hadi barabarani. Kuna siku walivunja kioo cha nyuma cha gari la dada la watu na bado wakamharass kisa alikanyaga nyanya za watu wakati ukiangalia kiuhalisia barabara is almost impassable.

Tutafute permanent solution ya matatizo yetu. Yes it's painful but tupate muarobaini wa hili tatizo.
 
Kusema ukweli sioni sababu ya kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo waliokuwepo huku pembezoni mwa mji kwenye vituo vya daladala kama vile Banana, Mombasa, Gongo la mboto, Mbagala, Mbezi etc.

Huku pembezoni walikuwa wanaathiri nini mpaka mumewaondoa pia? Kuwaondoa katikati ya mji kama Posta na Kariakoo ilikuwa sahihi lakini sio huku pembezoni mwa mji ambako ndio makazi ya watu.

Viongozi jaribuni kulifikiria upya hili swala. Hawa jamaa licha ya kujipatia kipato walikuwa wanasaidia sana. Wengine hatuna muda wa kwenda sokoni kununua matunda au yale mahitaji madogo madogo tuliyokuwa tunayapata kwenye vituo vya daladala tukiwa tunaelekea nyumbani tukiwa tunatoka makazini.

Sasa hivi vituo vya daladala vimepoa sana utadhani tupo vijijini. Binafsi wafanyabiashara kwenye vituo vya daladala naona walikuwa wanaupendezesha mji na wanarahisisha sana maisha.

Badala ya kupoteza muda kwenda sokoni tulikuwa tunapata mahitaji yetu bila shida kabisa na kwa bei nafuu

Viongozi hebu jaribuni kuliangalia hili suala kwa mapana, sioni tatizo la machinga kufanya biashara pembezoni mwa mji na zaidi ya yote sisi raia wa kawaida tunawahitaji.
Mbona maeneo uliyoyataja yako ndani ya jiji?
 
Kusema ukweli sioni sababu ya kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo waliokuwepo huku pembezoni mwa mji kwenye vituo vya daladala kama vile Banana, Mombasa, Gongo la mboto, Mbagala, Mbezi etc.

Huku pembezoni walikuwa wanaathiri nini mpaka mumewaondoa pia? Kuwaondoa katikati ya mji kama Posta na Kariakoo ilikuwa sahihi lakini sio huku pembezoni mwa mji ambako ndio makazi ya watu.

Viongozi jaribuni kulifikiria upya hili swala. Hawa jamaa licha ya kujipatia kipato walikuwa wanasaidia sana. Wengine hatuna muda wa kwenda sokoni kununua matunda au yale mahitaji madogo madogo tuliyokuwa tunayapata kwenye vituo vya daladala tukiwa tunaelekea nyumbani tukiwa tunatoka makazini.

Sasa hivi vituo vya daladala vimepoa sana utadhani tupo vijijini. Binafsi wafanyabiashara kwenye vituo vya daladala naona walikuwa wanaupendezesha mji na wanarahisisha sana maisha.

Badala ya kupoteza muda kwenda sokoni tulikuwa tunapata mahitaji yetu bila shida kabisa na kwa bei nafuu

Viongozi hebu jaribuni kuliangalia hili suala kwa mapana, sioni tatizo la machinga kufanya biashara pembezoni mwa mji na zaidi ya yote sisi raia wa kawaida tunawahitaji.
Usiturudushe nyuma, tunasonga mbele. Lazima taratibu zifuatwe katika kufanya biashara.
 
Kusema ukweli sioni sababu ya kuwaondoa wafanyabiashara ndogo ndogo waliokuwepo huku pembezoni mwa mji kwenye vituo vya daladala kama vile Banana, Mombasa, Gongo la mboto, Mbagala, Mbezi etc.

Huku pembezoni walikuwa wanaathiri nini mpaka mumewaondoa pia? Kuwaondoa katikati ya mji kama Posta na Kariakoo ilikuwa sahihi lakini sio huku pembezoni mwa mji ambako ndio makazi ya watu.

Viongozi jaribuni kulifikiria upya hili swala. Hawa jamaa licha ya kujipatia kipato walikuwa wanasaidia sana. Wengine hatuna muda wa kwenda sokoni kununua matunda au yale mahitaji madogo madogo tuliyokuwa tunayapata kwenye vituo vya daladala tukiwa tunaelekea nyumbani tukiwa tunatoka makazini.

Sasa hivi vituo vya daladala vimepoa sana utadhani tupo vijijini. Binafsi wafanyabiashara kwenye vituo vya daladala naona walikuwa wanaupendezesha mji na wanarahisisha sana maisha.

Badala ya kupoteza muda kwenda sokoni tulikuwa tunapata mahitaji yetu bila shida kabisa na kwa bei nafuu.

Viongozi hebu jaribuni kuliangalia hili suala kwa mapana, sioni tatizo la machinga kufanya biashara pembezoni mwa mji na zaidi ya yote sisi raia wa kawaida tunawahitaji.
Tunajenga masoko kwa pesa nyingi wengine mnakuja kuona hamna muda wa kwenda sokoni, hii nchi ni ngumu sana
 
MATAGA wamekuja kivingine. Ati hawana muda wa kwenda sokoni hivyo wamachinga warudishwe barabarani kuendelea kuuza mbogamboga kwenye vumbi. Aisee?! Ubwenyeye Wa kijinga.
 
MATAGA wamekuja kivingine. Ati hawana muda wa kwenda sokoni hivyo wamachinga warudishwe barabarani kuendelea kuuza mbogamboga kwenye vumbi. Aisee?! Ubwenyeye Wa kijinga.
Soma uelewe nilichoandika.
 
Naipongeza sana Serikali kwa kuwaondoa wamachinga sehemu zisizostahili kufanyia biashara. Pia nampongeza sana Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam. Jiji linaonekana sasa.

Halafu wewe Mtoa mada jaribu kutembelea nchi zenye ustawi mzuri uone kama ni kila sehemu ni pakuuzia nyanya na vitunguu. Eti ilikuwa inaturahisishia!!!
 
Naipongeza sana Serikali kwa kuwaondoa wamachinga sehemu zisizostahili kufanyia biashara. Pia nampongeza sana Mkuu wa Mkoa Dar Es Salaam. Jiji linaonekana sasa.

Halafu wewe Mtoa mada jaribu kutembelea nchi zenye ustawi mzuri uone kama ni kila sehemu ni pakuuzia nyanya na vitunguu. Eti ilikuwa inaturahisishia!!!
Aisji South Africa huyu na alikusifia sana ila nyumbani hataki kupendeze
 
walichafua sana jiji aisee asaivi hadi hewa inapatikana mnasnindwa hata na ka nchi kadogo Rwanda, lazima kuwe na mpangilio jamani
 
Sijui kulikuwa na logic gani kuwasafisha hadi huku pembeni.
Maeneo unayoyataja yako ndani ya jiji?
Kama jibu ni ndio, basi sheria za jiji ni moja na zinafanya kazi sawia kwa jiji lote.
.
Unaposema katikati na pembezoni sijui unapima kwa kutumia taratibu gani za usimamizi wa jiji.
 
Ni uonevu tu umefanyika,
Hapo kariakoo sasa hivi hapapitiki kwa malori na ofisi za usafirishaji mizigo yaani wanaziba kabisa barabara
Kumbe ni malori ya wakubwa humo serikalini
Wamachinga wameonewa sana ila mungu yupo atahukumu
Haya malori ni kero na adha kuliko machinga juzi kati hapa mgonjwa amefia ndani ya gari kwasababu ya malori yameziba njia na ukiwaambia sogezeni tupute wanakwanbia dereva hayupo,
Polisi au jiji wakija wanachukua chao wanasepa
Iko siku watu wanachukua hatua mkononi
Ndio kitaeleweka
 
Back
Top Bottom