Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
Katika hali isiyo ya kawaida polisi mmoja kule Mara amempiga risasi kiunoni na kumuua mtuhumiwa mmoja wa ujambazi aliekua anakimbia. Mtuhumiwa huyo mwenye jina la Ochieng' pamoja na wenzake wawili walikua wamepanga kufanya tukio la ujambazi katika moja ya maeneo yaliyo karibu na mwambao wa Ziwa Victoria.
Lakini kutokana na whistleblowers katika maeneo hayo, polisi walipewa taarifa na kwenda kuwakabili majambazi hayo, ndipo ndugu Ochieng' akaanza kukimbia, polisi alimtaarifu asimame la sivyo atampiga risasi, Ochieng' akaendelea kukimbia...
Polisi akaamua kupiga risasi tatu juu hewani ili amshtue mtuhumiwa, lakini haikusaidia. Ndipo polisi huyo akaamua kukumbushia mazoezi ya kulenga shabaha, akampiga ndugu Ochieng' kiunoni!! (Haya ni maelezo toka kwa kamanda wa polisi wa eneo husika). Kutokana na maelezo ya kamanda wake, polisi yule alikosea kumlenga mtuhumiwa!!
Chanzo: TBC1
Sasa nimejiuliza sana hivi huyu polisi alipitia mafunzo ya kulenga shabaha kweli? Kama ndio alifuzu kweli? Kama hakupata mafunzo kwa nini amepewa silaha?
Je, kuna hatua gani za kinidhamu na kisheria anapaswa kuchukuliwa? Je, ndugu za Ocheing' hawastahili kupewa fidia?! Nasema haya kwa vile kulikua hakuna majibizano ya risasi baina ya polisi na mtuhumiwa, hivyo the preferable option aliyokua nayo yule polisi ni kumpiga risasi ya mguuni mtuhumiwa ili asiendelee kukimbia!!
Haya yametokea leo huku jeshi la polisi likiadhimisha miaka 95 toka kuanzishwa kwake!! Na muhishiwa rais amesisitiza suala la polisi kuheshimu haki za raia.
Lakini kutokana na whistleblowers katika maeneo hayo, polisi walipewa taarifa na kwenda kuwakabili majambazi hayo, ndipo ndugu Ochieng' akaanza kukimbia, polisi alimtaarifu asimame la sivyo atampiga risasi, Ochieng' akaendelea kukimbia...
Polisi akaamua kupiga risasi tatu juu hewani ili amshtue mtuhumiwa, lakini haikusaidia. Ndipo polisi huyo akaamua kukumbushia mazoezi ya kulenga shabaha, akampiga ndugu Ochieng' kiunoni!! (Haya ni maelezo toka kwa kamanda wa polisi wa eneo husika). Kutokana na maelezo ya kamanda wake, polisi yule alikosea kumlenga mtuhumiwa!!
Chanzo: TBC1
Sasa nimejiuliza sana hivi huyu polisi alipitia mafunzo ya kulenga shabaha kweli? Kama ndio alifuzu kweli? Kama hakupata mafunzo kwa nini amepewa silaha?
Je, kuna hatua gani za kinidhamu na kisheria anapaswa kuchukuliwa? Je, ndugu za Ocheing' hawastahili kupewa fidia?! Nasema haya kwa vile kulikua hakuna majibizano ya risasi baina ya polisi na mtuhumiwa, hivyo the preferable option aliyokua nayo yule polisi ni kumpiga risasi ya mguuni mtuhumiwa ili asiendelee kukimbia!!
Haya yametokea leo huku jeshi la polisi likiadhimisha miaka 95 toka kuanzishwa kwake!! Na muhishiwa rais amesisitiza suala la polisi kuheshimu haki za raia.