Hapa Utajifunza Kitu

Paul Kijoka

JF-Expert Member
Oct 25, 2010
1,399
255
*HII IMENIGUSA by Mutakyahwa Kijoka (FB)*

*Kulikuwepo msichana kipofu aliyechukia na kujichoka sana.*

*Alimchukia kila mtu isipokuwa mchumba wake. Mara zote alikuwa karibu naye.*

*Msicha huyo alimwambia mchumba wake, 'Kama ningebahatika kidogo, ningekubali kuolewa na wewe.'*

*Siku moja, mtu ambaye hakumjua alimfadhiri macho 2. Alipoondolewa bandeji kwenye vidonda na macho kupona kabisa, alifurahi kuona kila kitu, ikiwemo mchumba wake wa kiume.*

*Mchumba wake alimuuliza, sasa unaona kila kitu, ukubali kuolewa na mimi?'*

*Msichana Mwenye kuona sasa, alimgeukia mchumba wake na kugundua naye alikuwa Kipofu. Ule mwonekano wa macho yaliyofumbwa kwa upofu, yalimtisha msichana yule.‍♂ Msichana yule hakutegemea hivyo. Ile fikra ya kuona mwinekano ule wa upofu ulimfanya Msichana akatae‍♂ kuolewa na yule mvulana kipofu.*

*Mchumba wake aliondoka kwa kilio na baada siku chache badae alimwandikia Msichana huyo kijibarua ✍ ukisema: 'Yajali sana macho yako, rafiki yangu, si unaona sasa ni macho yako, hapo awali yalikuwa yakwangu.'*

*Hivi ndivyo ubongo wa binadamu yeyote kufanya kazi pale kipato, cheo au aina yoyote ya fursa pindi inapojitokeza.*

*Ni wachache tu hukumbuka maisha yaliyopita, na kukumbuka wale walikuwa karibu yao wakati wa shida na maumivu.*

*Maisha ni Zawadi*

*Kuanzia sasa kabla hujaongea maneno yasiyo ya huruma -*

*Mfukirie Bubu au asiyeongea.*

*Kabla hujalalamikia radha mbaya ya chakula kilicho mbele yako - Mfikirie mtu asiye na chakula .*

*Kabla hujalalamika kuhusu mume au mke wako - Mfikirie anaye mlilia MUNGU apate mume au mke ila hajapata.*‍♂

*Leo hii kabla hujalalamika kuhusu maisha au kuishi -*

*Mkumbuke fulani aliyekufa akiwa kichanga au kabla ya kuzaliwa.*

*Kabla hujalalamika kuhusu Watoto wako -*

*Mfikirie yule ambaye angetaka kuwa na mtoto lkn ni tasa au mgumba.*‍♂

*Leo hii kabla hujalalamika kuhusu uchafu wa nyumba ambao haujafanywa na mtu fulani -*

*Wafikirie wale wanaolala mitaani kwenye mitaro, magofu, nk.*

*Kabla hujajisikia kuçhoshwa na kuendesha umbali mrefu*

*Mfikirie anayetembea kwa mguu umbali huo huo.*‍♀

*Nawakati unapochoka na kulalamikia kazi yako -*

*Wafikirie wale wasio na ajira, wenye lemavu na wale wanaoitamani kazi uliyonayo-*

*Kumbuka sote tu watenda dhambi na tunawajika kwa MUUMBA*

*Na wakati maoni mbaya wanapokuingia kumbuka -*

*Mtangulize Mungu aliyeahi na karibu yako.*

*Na kabla hujafunga huu Ujumbe, tafadhari, watumie watu wengineo wengi au share ili nao wafurahie... Waweza kubadirisha mtazamo kuhusu maisha.*


*Imetafisiriwa na Mutakyahwa Kijoka (fb).*
 
Hapo Pointi ni moja tu, mtangulize Mungu wako, mengine yoote ni chachandu ya kupendezesha Chakula kinoge, yaani kila ukipata changamoto basi mfikirie mwenye tatizo kubwa zaidi, halafu iweje
 
Back
Top Bottom