Hapa Itakuwakuwaje?... "Maamuzi ya Mgonjwa au Daktari?"

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
i5uebo.jpg


Picha kwa hisani ya Haki-hakingowi.blogspot.com


Kazi nzuri sana kutoka kwa Kipanya. Sasa maamuzi yetu kama "madaktari" ni yepi? Tung'oe kichwa haraka iwezekanavyo au tuache "cancer" isambaratike mwili mzima kwa "kuogopa kuua" au tuendelee kumpatia mgonjwa muda wa kufikiria "akiwa toilet?"
 
Hapo ni kung'oa kuchwa tu mapema iwezekanavyo, ikiwa na maana ya kumng'oa huyu mdudu CCM.
 
Toilet anaenda na kidude cha damu/maji hicho?...maana option nyingine kukichomoa umwachie aende hivyo hivyo.....:cool:
 
Nadhani mganga hajafanya diagnosis vizuri, kansa hii imeshaenea mpaka kwenye vidole vya miguu
 
Hatakubali kukatwa halafu amwachie nani hayo mapene?Atafia huko toilet.
 
Daktari kachelewa kumpa nusu kaputi ... angejadiliana naye huku tayari anapima na nguvu ya kaputi
 
i5uebo.jpg


Picha kwa hisani ya Haki-hakingowi.blogspot.com


Kazi nzuri sana kutoka kwa Kipanya. Sasa maamuzi yetu kama "madaktari" ni yepi? Tung'oe kichwa haraka iwezekanavyo au tuache "cancer" isambaratike mwili mzima kwa "kuogopa kuua" au tuendelee kumpatia mgonjwa muda wa kufikiria "akiwa toilet?"

...tatizo kwenye 'protokali' ya taaluma hii, inabidi mgonjwa atoe kwanza consent yake, kufuatiwa na consent ya wanafamilia, mwisho ndio madaktari kutoa AMRI yao!

...afanaileki huo msumeno nyuma ya Dokta!

:D
 
Daktari kachelewa kumpa nusu kaputi ... angejadiliana naye huku tayari anapima na nguvu ya kaputi

Kuna taratibu za consent dadangu lakini nafeel uchungu wako,msumeno nyuma ya doctor umeuona? ha ha
 
Last edited by a moderator:
...tatizo kwenye 'protokali' ya taaluma hii, inabidi mgonjwa atoe kwanza consent yake, kufuatiwa na consent ya wanafamilia, mwisho ndio madaktari kutoa AMRI yao!

...afanaileki huo msumeno nyuma ya Dokta!

:D

...:) mchongoma, tatizo huyu mgonjwa kaanza kutumia sababu ya "kwenda toilet kufikiria" zaidi ya miaka miwili sasa. kila kukitokea dharura ya kutufanya tumng'oe kichwa anakimbilia toilet... tusipoangalia hii consent ya mgonjwa itaishia kutuangamiza sote (kwa gharama na maambukizi)... mi-cancerous cells inazidi kuenea mwili wote na hata kuambukiza wanajamii. Si huwa kuna kipindi madakatari wanaruhusiwa kuzima mashine pale wanapoona mgonjwa hatibiki, au..?!
 
Mgonjwa haulizwi TIBA wala DAWA. Naona hapa daktari KP anatafuta "KUWEZESHWA" tu!
 
...:) mchongoma, tatizo huyu mgonjwa kaanza kutumia sababu ya "kwenda toilet kufikiria" zaidi ya miaka miwili sasa. kila kukitokea dharura ya kutufanya tumng'oe kichwa anakimbilia toilet... tusipoangalia hii consent ya mgonjwa itaishia kutuangamiza sote (kwa gharama na maambukizi)... mi-cancerous cells inazidi kuenea mwili wote na hata kuambukiza wanajamii. Si huwa kuna kipindi madakatari wanaruhusiwa kuzima mashine pale wanapoona mgonjwa hatibiki, au..?!

...kwa mtaji huo ni kupiga mionzi (Chemotherapy) kuua seli za ubongo, akishakuwa brain dead unazima mashine!
 
Kuna taratibu za consent dadangu lakini nafeel uchungu wako,msumeno nyuma ya doctor umeuona? ha ha

Kyoryere .... huyu ni mgonjwa wa taifa ... consent tumeshaitoa sisi watanzania ... hamna kwenda msalani wala nini ... just check kama msumeno umenolewa vizuri ... embu tizama vizuri .. unakata upande mmoja ama kote kote
 
[COLOR="DarkRed[COLOR="Red"]"]...tatizo kwenye 'protokali' ya taaluma hii, inabidi mgonjwa atoe kwanza consent yake, kufuatiwa na consent ya wanafamilia, mwisho ndio madaktari kutoa AMRI yao![/COLOR]...afanaileki huo msumeno nyuma ya Dokta!

:D[/COLOR]

Nadhani tulipofikia daktari haitaji kutaka consent ya mgonjwa wala familia.
Huyu mgonjwa aliwahi kuugua magonjwa nyemelezi tele kama ujinga, uvivu na hapo alipo pamoja na hiyo kansa ya ufisasi nasikia ana ugua umasikini pia.

Siku zote amekuwa mbishi kufuatilia tiba.Daktari hana ujanja ila kumpa tiba muafaka hata kama ni kung'oa kichwa.

Hata hivyo huyo daktari nina shaka nae.Ana tofauti gani na waliomtangulia tangu uhuru?Nawasikia kila wakipata nafasi ya udakitari mkuu hapo huwa wanaahidi kuyaendeleza yote ya watangulizi wao.

Sidhani kama huyo daktari hata akipata consent ya mgonjwa atakata kichwa, ugua ya mgonjwa ndio kula yake.
 
tatizo kubwa zaidi nafikiri dakatri hana uwezo wa kumhudimia mgonjwa huyu! daktari anaendeshwa na mgonjwa! na kauli ya mgonjwa ndiyo inayokubalika...
hasara kubwa ugonjwa umeanzia pabaya
 
Kuna taratibu za consent dadangu lakini nafeel uchungu wako,msumeno nyuma ya doctor umeuona? ha ha


Huyu mgonjwa hawezi kutoa consent kwa sababu tayari ubongo wake umeathiriwa na cancer hivyo maamuzi yake yanaweza kuwa si sahihi....kwikwikwikwi
 
Je Doctor amuache mpaka afe kifo cha kawaida?, mpaka afe na Doctor nae atakuwa ameisha ipata hiyo Cancer maana kila siku yupo nae. Dawa yake ni kwa Doctor kuweka maji ya betri kwenye hiyo chupa ya damu bila mgonjwa kujua.
 
Back
Top Bottom