brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,876
- 7,366
????????Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WEKUNDU wa ,Msimbazi Simba sc wameshamaliza mazungumzo na
wachezaji wawili kutoka nchi za Uganda na Kenya na kinachosubiriwa
ni safu mpya ya uongozi itakayopatikana juni 29 mwaka huu baada ya
kufanyika uchaguzi.
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba sc, Keptein wa zamani wa Jeshi la wananchi la Tanzania, (JWTZ), Zacharia Hans Poppe ameuambia
mtandao huu jioni hii kuwa tayari wamepata `jembe` moja la kazi
kutoka Uganda na lingine kutoka Kenya ( hakutaja majina).
Kuhusu wachezaji waliokuwa nao msimu uliopita, mwanajeshi huyo
wa zamani wa JWTZ alisema kuwa wameamua kuwabakisha wachezaji
13. Wachezaji wa zamani tuliobaki nao ni 13 tu, kwahiyo tutachukua
wengine 12 wa hapa nchini na hao wawili kutoka nje.
Sisi tunaendelea vizuri na usajili, kimsingi nawaasa wenzangu
waingize timu nzuri ya Uongozi ambayo tunaweza kufanya nayo kazi
Wawe makini kwasababu wachezaji hawa tunaowasajili ni kwaajili
ya msimu ujao. Waangalie viongozi ambao tutakubaliana kimawazo na sisi,
kwasababu tunaweza kuwa na malumbano tena.
Poppe aliongeza kuwa wagombea wengi wanaowania nafasi za
uongozi walishawahi kuwa viongozi wa Simba, hivyo wanachama
waangalie ni nani alikuwa na mafanikio katika kipindi chake.
Binafsi najua Aveva ni kiongozi mzuri na akiwa na makamu wake Kaburu, basi timu itakuwa nzuri na tutatengeneza gurudumu la Simba.
Nikianza na Kaburu, mtu huyu aliweza kuitengeneza timu ya U20
ambayo imezaa wachezaji kama Ramadhani Singano `Messi`, Harun
Chanongo, Said Ndemla na wengineo. Haya ni matunda yanayotokana
na jitihada kubwa alizofanya Kaburu.
Aveva alikuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili wakati ambao Simba alikuwa na mafanikio ambayo hayajapatikana mpaka leo.
Ni kipindi ambacho Simba iliweza kuwa na makombe nane. Ni kipindi
ambacho alikuwepo Kassim Dewji aliyejenga jengo ambalo
linawaingizia kipato viongozi wa sasa.
Timu ya Aveva na Kaburu nadhani inaweza kuleta matokeo ambayo
yalipatikana kipindi kile, ambayo hayajapatikana mpaka leo. Kwahiyo nafikiri hawa ni watu ambao wanaweza kuleta maendeleo bila tatizo.
Alisema Poppe.
Akimzungumzia Jamhuri Kiwhelo na Richard Wambura, Poppe alisema
hawajawahi kupata mafanikio katika uongozi wao.
Wambura alipata mafanikio gani wakati wa uongozi wake. Mimi sioni
kama kuna kitu alifanya akiwa Simba. Wadau waseme hawa walifanya A,B C, D. Mimi nimesema Aveva na Kaburu walifanya nini.
Julio anagombea umakamu mwenyekiti, sijui amefanya nini. Yeye kazi
yake ilikuwa ukocha na alikuwa analipwa mshahara. Wasichague mtu
kwasababu tu ana wafuasi wengi, eti wanampenda sura au maneno
yake. Sisi tunataka uhalisia, je, alifanya kitu gani?. Alihoji Poppe.
Poppe aliweka wazi msimamo wake kuwa endapo wanachama hawatawachagua Aveva na Kaburu itakuwa juu yao, lakini yeye
hatakuwepo katika uongozi wa Simba tofauti na safu ya hao wawili.
Msimamo wangu nausema wazi. Sitaweza kufanya kazi na viongozi
tofauti na hao wawili. Kwasababu naelewa uongozi wowote tofauti na
hao wawili hautaleta mabadiliko yoyote.
Sipo tayari kupoteza tena muda wangu na pesa zangu kama nilivyofanya kipindi kilichopita. Alisisitiza Poppe.
Uchaguzi wa Simba sc utafanyika jijini Dar es salaam juni 29 mwaka
huu ambapo Rais mpya , makamu wa rais na wajumbe wapya wa
kamati ya utendaji watapatikana tayari kwa safari nyingine ya miaka
minne ya uongozi.
Nini maoni yako mdau ukizingatia muda wa kampeni bado? Kuna demokrasia kweli hapa?
WEKUNDU wa ,Msimbazi Simba sc wameshamaliza mazungumzo na
wachezaji wawili kutoka nchi za Uganda na Kenya na kinachosubiriwa
ni safu mpya ya uongozi itakayopatikana juni 29 mwaka huu baada ya
kufanyika uchaguzi.
Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba sc, Keptein wa zamani wa Jeshi la wananchi la Tanzania, (JWTZ), Zacharia Hans Poppe ameuambia
mtandao huu jioni hii kuwa tayari wamepata `jembe` moja la kazi
kutoka Uganda na lingine kutoka Kenya ( hakutaja majina).
Kuhusu wachezaji waliokuwa nao msimu uliopita, mwanajeshi huyo
wa zamani wa JWTZ alisema kuwa wameamua kuwabakisha wachezaji
13. Wachezaji wa zamani tuliobaki nao ni 13 tu, kwahiyo tutachukua
wengine 12 wa hapa nchini na hao wawili kutoka nje.
Sisi tunaendelea vizuri na usajili, kimsingi nawaasa wenzangu
waingize timu nzuri ya Uongozi ambayo tunaweza kufanya nayo kazi
Wawe makini kwasababu wachezaji hawa tunaowasajili ni kwaajili
ya msimu ujao. Waangalie viongozi ambao tutakubaliana kimawazo na sisi,
kwasababu tunaweza kuwa na malumbano tena.
Poppe aliongeza kuwa wagombea wengi wanaowania nafasi za
uongozi walishawahi kuwa viongozi wa Simba, hivyo wanachama
waangalie ni nani alikuwa na mafanikio katika kipindi chake.
Binafsi najua Aveva ni kiongozi mzuri na akiwa na makamu wake Kaburu, basi timu itakuwa nzuri na tutatengeneza gurudumu la Simba.
Nikianza na Kaburu, mtu huyu aliweza kuitengeneza timu ya U20
ambayo imezaa wachezaji kama Ramadhani Singano `Messi`, Harun
Chanongo, Said Ndemla na wengineo. Haya ni matunda yanayotokana
na jitihada kubwa alizofanya Kaburu.
Aveva alikuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili wakati ambao Simba alikuwa na mafanikio ambayo hayajapatikana mpaka leo.
Ni kipindi ambacho Simba iliweza kuwa na makombe nane. Ni kipindi
ambacho alikuwepo Kassim Dewji aliyejenga jengo ambalo
linawaingizia kipato viongozi wa sasa.
Timu ya Aveva na Kaburu nadhani inaweza kuleta matokeo ambayo
yalipatikana kipindi kile, ambayo hayajapatikana mpaka leo. Kwahiyo nafikiri hawa ni watu ambao wanaweza kuleta maendeleo bila tatizo.
Alisema Poppe.
Akimzungumzia Jamhuri Kiwhelo na Richard Wambura, Poppe alisema
hawajawahi kupata mafanikio katika uongozi wao.
Wambura alipata mafanikio gani wakati wa uongozi wake. Mimi sioni
kama kuna kitu alifanya akiwa Simba. Wadau waseme hawa walifanya A,B C, D. Mimi nimesema Aveva na Kaburu walifanya nini.
Julio anagombea umakamu mwenyekiti, sijui amefanya nini. Yeye kazi
yake ilikuwa ukocha na alikuwa analipwa mshahara. Wasichague mtu
kwasababu tu ana wafuasi wengi, eti wanampenda sura au maneno
yake. Sisi tunataka uhalisia, je, alifanya kitu gani?. Alihoji Poppe.
Poppe aliweka wazi msimamo wake kuwa endapo wanachama hawatawachagua Aveva na Kaburu itakuwa juu yao, lakini yeye
hatakuwepo katika uongozi wa Simba tofauti na safu ya hao wawili.
Msimamo wangu nausema wazi. Sitaweza kufanya kazi na viongozi
tofauti na hao wawili. Kwasababu naelewa uongozi wowote tofauti na
hao wawili hautaleta mabadiliko yoyote.
Sipo tayari kupoteza tena muda wangu na pesa zangu kama nilivyofanya kipindi kilichopita. Alisisitiza Poppe.
Uchaguzi wa Simba sc utafanyika jijini Dar es salaam juni 29 mwaka
huu ambapo Rais mpya , makamu wa rais na wajumbe wapya wa
kamati ya utendaji watapatikana tayari kwa safari nyingine ya miaka
minne ya uongozi.
Nini maoni yako mdau ukizingatia muda wa kampeni bado? Kuna demokrasia kweli hapa?