Hans pope alipaswa kutokuwa wazi ni mgombea gani anayemtaka na kuacha demokrasia ichukue mkondo wake. Nina uhakika wa asilimia 100% kuwa wanasimba hawatarudia makosa kwani miaka minne ya maumivu kila mpenzi wa simba anaijua. Sio siri mpira sasa hivi unahitaji pesa. Cha msingi ni wanachama kuweka utaratibu ambao kutakuwa na kipindi cha mpito kwa hizi kilabu mbili kubwa simba na yanga kutoka mikononi kwa matajiri na kuanza kujitegemea. Na uwezo wa hizi timu kujitegemea upo kukiwa na misingi mizuri ya kukusanya kodi ya majengo na kuanza kuuza vitu kama jezi, skafu, na matangazo mbalimbali. Baada ya rage na manji kushindwa kuzifanya simba na yanga zianze kujitegemea sioni kiongozi mwingine mwenye uwezo huo kwa siku za karibuni.