Handbrake

beast18

JF-Expert Member
Mar 20, 2016
320
482
haya magar ya siku hizi pasua kichwa sana , nikikumbuka mikangafu yetu ya zamani haiendi bila kutoa handbrake halafu siku hizi gar ukiweka D tu inateleza nashangaa sana , nije kwenye swali sasa , je kuna matatizo yoyote ya kuendesha gar huku sijatoa handbrake , maana nimejaribu jana siku nzima nimeburuza tu zaidi ya kitaa kuwaka cha kuonyesha sijatoa handbrake hakuna tatizo lililojitokeza, wataalamu mnaweza kusema kitu hapa kama kuna tatizo lolote linaloweza kujitokeza kutokana na kuendesha bila kutoa handbrake
 
Hiyo gari uliyoendesha ni mbovu upande wa park brake ndo maana ww uliona iko sawa. Ingekuwa inafanya kazi sawasawa lazima ingekuwa nzito au isingeondoka
gari langu ni zima kabisa mkuu , halina ubovu wowote matter of fact halina muda
 
Hiyo gari itakuwa ni automatic na kuendesha gari kama hujatoa handbrake lazima uisikiw inakuwa nzito
 
Hiyo gari itakuwa ni automatic na kuendesha gari kama hujatoa handbrake lazima uisikiw inakuwa nzito
ni automatic kweli mkuu , ila tofauti sijaiona kubwa sana japo uzito ulikuwepo
 
Je brake ilkuw sawa, maana mm nakmbka nliwah sahau toa handbrake ila kila nkitaka kpiga brake km inakuw inafel hiv yaan had km niipamp ndo ishike vzr,ila nlpokuja kuitoa handbrek ikawa sawa.
 
Je brake ilkuw sawa, maana mm nakmbka nliwah sahau toa handbrake ila kila nkitaka kpiga brake km inakuw inafel hiv yaan had km niipamp ndo ishike vzr,ila nlpokuja kuitoa handbrek ikawa sawa.
kwangu mimi ilikuwa sawa kabisa mkuu, haikunipa shida kabisa
 
Kama ni jipya basi knowledge yako Kuhusu magari bado ni ndogo na kujua tofauti ya gari iliyotolewa kwenye handbrake na kuendeshea handbrake.
tofauti niliiona mkuu, soma vizuri utaona nauliza kama kuna tatizo lolote linaloweza kujitokeza , sijaulizia utofauti mimi
 
Gari linakuwa zito nakupelekea rpm kuwa juu kwa mwendo mdogo. Kama kuna sehemu yenye mwinuko mkali inaweza shindwa kupanda. Madhara yaliyo wazi ni fuel consumption kuongezeka na kama cooling system isipokuwa nzuri gari inaweza ikachemsha.
 
Gari linakuwa zito nakupelekea rpm kuwa juu kwa mwendo mdogo. Kama kuna sehemu yenye mwinuko mkali inaweza shindwa kupanda. Madhara yaliyo wazi ni fuel consumption kuongezeka na kama cooling system isipokuwa nzuri gari inaweza ikachemsha.
asante nimekuelewa vizur mkuu
 
Handbrake kama inafanya kazi sawa sawa gari unapoanza kuiondoa lazima igome kuondoka au kama itaondoka itakuwa nzito na kunakuwa na mlio wa kitu kinachosugua.Hiyo gari yako peleka kwa mafundi kuna adjustment wanafanya ni hela kidogo tu ndugu halafu ujaribu tena kuondoka ikiwa ime lock,then tupe mrejesho.Madhara ni pamoja na kutumia mafuta mengi,pia kutokana na msuguano kwenye hiyo mechanism inaweza kusababisha kupasuka kwa tairi kutokana na joto kuwa kubwa kwenye rims.
 
Handbrake kama inafanya kazi sawa sawa gari unapoanza kuiondoa lazima igome kuondoka au kama itaondoka itakuwa nzito na kunakuwa na mlio wa kitu kinachosugua.Hiyo gari yako peleka kwa mafundi kuna adjustment wanafanya ni hela kidogo tu ndugu halafu ujaribu tena kuondoka ikiwa ime lock,then tupe mrejesho.
ntajaribu ndugu japo kwa experience ndogo nliyonayo magar mengi ya auto yanaenda kiuzitozito ila sio kugoma kabisa, unless hili nalo ni tatizo kwa magari haya
 
haya magar ya siku hizi pasua kichwa sana , nikikumbuka mikangafu yetu ya zamani haiendi bila kutoa handbrake halafu siku hizi gar ukiweka D tu inateleza nashangaa sana , nije kwenye swali sasa , je kuna matatizo yoyote ya kuendesha gar huku sijatoa handbrake , maana nimejaribu jana siku nzima nimeburuza tu zaidi ya kitaa kuwaka cha kuonyesha sijatoa handbrake hakuna tatizo lililojitokeza, wataalamu mnaweza kusema kitu hapa kama kuna tatizo lolote linaloweza kujitokeza kutokana na kuendesha bila kutoa handbrake
Mzee kama gari halikuwa zito nenda kacheck handbrake.. huenda ikawa imekufa yani haifanyi kazi..
 
Mzee kama gari halikuwa zito nenda kacheck handbrake.. huenda ikawa imekufa yani haifanyi kazi..
ilikuwa nzito kiasi flan mkuu japo ilitembea na nlizunguka nayo mjini hvohvo
 
Back
Top Bottom