Hana Pesa ya Kuendeleza eneo lake Kinondoni

erique

JF-Expert Member
Apr 23, 2010
582
565
Habari za mizunguko ya leo wadau.
Yupo rafiki yangu, yeye ana eneo lake maeneo ya Kinondoni, karibu kabisa na msikiti wa Mtambani. Kiwanja hicho kimepimwa na tayari kinayo hati.

Sasa, ukweli ni kwamba huyu rafiki yangu hana pesa ya kuendeleza eneo hilo, na pia hataki kupauza.Mimi nimemshauri atafute mdau mwenye pesa aweze kupaendeleza, kisha kuwepo na kisha kuwe na makubaliano ya aina fulani kati ya muendelezaji na huyo mwenye kiwanja.

Sasa naomba mawazo yenu juu ya suala hili, na hasa jinsi ya kupata muwekezaji atakayeweza kuendeleza hilo eneo, na hata juu ya aina ya makubaliano yanayofaa kuingia kati ya pande hizo mbili.

Karibuni mtushauri.
 
Back
Top Bottom