Tupeane pole Watanzania wote kwa nchi yetu kushindwa kuwa na taasisi zinazotenda haki, na hivyo kutupatia uhakika wa jamii yetu kuwa na usalama na amani ya kweli.Pole sana.
Ndoto ya Mwalimu Nyerere ilikuwa kujenga Taifa litakalokuwa la mfano Afrika kwa kutambua na kuheshimu thamani ya utu. Ndoto yake hiyo imeharibiwa kabisa, kiasi cha Tanzania kuwa Taifa la kukemewa na mataifa yaliyostaarabika kwa kukiuka haki za msingi za wananchi wake.