HAMIS Kigwangalla: Jana Rais Kikwete aliniachia kiti, nikakaa na marais wengine. Can u belive that?

Hamisi Kigwangalla

Nipo hapa jijini Yokohama, Japan. Nipo kwenye msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete kwenye mkutano mkubwa na maarufu duniani kuhusu Afrika unaojulikana kama TICAD V (Tokyo International Conference on African development). Kwa dakika chache jana Mhe. Rais Jakaya Kikwete aliniachia kiti chake, nikaa kwenye round table na marais wengine zaidi ya 50 wa nchi za Afrika! Can you imagine that? Kulia kwangu alikuwa Mhe. Michael Satta (Rais wa Zambia - a very charming fella!) na kushoto kwangu alikaa Mhe. Yoweri Museveni (Rais wa Uganda).

Leo tena nimepata fursa ya kuingia kwenye kikao kimoja na Mhe. Rais Jakaya Kikwete na humo tulikuwa kwenye bilateral meeting na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Mhe. Ban-Ki Moon. Pia nimepata fursa ya kujadili mambo kwenye vikao na Marais Jacob Zuma (South Africa), Ali Bongo Ondimba (Gabone); Rais wa World Bank, Dr. Jim Yong Kim; Rais wa Benki ya Afrika, Dr. Donald Kaberuka; Rais wa JICA, Dr. Akihiko Tanaka etc. Ziara hii imenifundisha mambo mengi ambayo sintoyasahau katika maisha yangu.

Nimepata pia fursa ya kumuelewa vizuri zaidi Rais wetu na namna anavyoielewa dunia, kukubalika kwake kimataifa, nafasi yake kati ya viongozi mashuhuri duniani na nafasi yetu kama Taifa katika dunia. Hongera Rais wetu Jakaya Kikwete, umenifanya nijisikie 'so proud to have you as our president, and to be a Tanzanian in a global world!' Ziara hii kwenye mkutano huu mkubwa wa kimataifa hapa Japan imenipanua zaidi uelewa wangu kuhusiana na diplomasia ya kimataifa na namna changamoto zinazotukabili sote kama raia wamoja wa dunia moja na namna zinavyopatiwa ufumbuzi wa pamoja, kwa namna ya umoja wetu kama binadamu.


MWISHO WA KUNUKUU. source ukurasa wa facebook kwenye wall ya kigwangala

Naona hapo baba ya rizmoko na hiyo suti si ile ya maleberali ya kiarabu?
 
Safari ya kwanza umeanza leta shida km wabunge wengine...CCM inabidi wabadili sera yao ndani ya kukataa wakaskazini..Sasa Kigwangala angekuwa km Eli si angemkalisha chini JK?Wabunge wa tabora wanazidi kujionesha kuwa hocyo sana miezi hiii..mganga wao kafa nini ?Au ndumba imeingia virus?

Hapa kuna shida na huyu mbunge kwa tabia zake za asili.....ingekuwa dunia haina protokali,pangeshakuwa na vujo nyingin sana..Kama ni maraisi tupu ni marais tupu,huwezi ingia na mke ahat upige magoti.N anchi husika haitokuwa tayari kwani ni diplomatic row,wanaweza onekana wantaka weka rais wao ktk nchi nyingine.

Wewe na JK ni aibu kwa taifa.Hata ungekuwa "haki sawa wake mpya" hilo lisingewezekana.
 
Sasa kukalia kiti ndo nini.. ushirikina mwingine bana... afu unaeleza as if ni kitu cha pekee sana.. ungesema walau kitu kuhusu hotuba yake kama alitoa.. kuhusu alivyowakilisha nchi yetu... sio eti nimekalia kiti chake... what has it to do with our country's development?
 
Sasa kukalia kiti ndo nini.. ushirikina mwingine bana... afu unaeleza as if ni kitu cha pekee sana.. ungesema walau kitu kuhusu hotuba yake kama alitoa.. kuhusu alivyowakilisha nchi yetu... sio eti nimekalia kiti chake... what has it to do with our country's development?

Umesema kweli...huyu jamaa anakuwa kakalishwa pale kishirikina..ama kwa ushirika na JK,au kwa mambo bonafsi...pengine aliambiwa mganga wake achukue nyota ili arithi urais.Inaelekea alifanya kwa kulazimisha.sasa ana hofu au anataka aje sema kuwa kaandaliwa kuwa rais na awapige bao akina Membe na wengine.
 
Hapa HK kinamna anatoa ushuhuda jinsi JK na wenzake anavyokacha mikutano? Simuelewi HK..
 
Hata mimi ningdapata heshima hiyo ningefurahi. Lakini sioni kwanini mtu uwe excited namna hiyo mpaka kuandika Facebook? Eti can you believe that? Halafu hii dhana ya raisi anakubalika kimataifa nayo ni ya ajabu. Kwani yeye ni raisi wa kimataifa au ni raisi wa Tanzania? Lazima nje wamkubali maana anawapa resources zetu bure!
 
Hiyo si habari, habari ni: 1-Kikwete alikuwa wapi kuacha kikao muhimu kama hicho, ambacho ndicho kilichompeleka? 2- Wewe ulichangia nini, au kukaa na Ban pekee ndiyo umetimiza lengo? 3-Tanzania imetoka na faida gani katika haya yote, au ni kushibisha ego zenu tu?

Mimi huyu jamaa HK sijawahi kumuelewa hata vitu anavyoandika fb ni vitu vyepesi mno hakuna weledi wala ile radha ya maneno ya kiuongozi kabisa.
 
Good kigwangala hongera sana, japo kuna mamluki watakuja kuponda sana, lakini ukweli kuwa ni heshima kubwa kwako na wengi wana ndoto japo zakuja kupangana na mbunge tu ila hawajapata,hongera kwa uliyojifunza yasiishie kwenye majarida yafanyie kazi

Kajifunza nini? Nyanya zinaendeleaje hapo? Vp u.p....... Anasemaje?
 
485403_10151883106273243_582897025_n.jpg
Kigwangalla mdomo wake umechubuka kama anagonga gongo kwa mama muuza
 
Kikwete ana nafasi kimataifa kwa sababu ya rasilimali zetu sasa ameshindwa kuitumia fursa hyo kutuletea maendeleo yenye tija tz hayo mengine ya kukaa round table cc hayatuhusu kama taifa kikubwa tumenufaika nn na huo mkutano kama taofa acha ulimbuken kukaa na viongoz wakubwa unafurahi na watanzania wanalala giza huku bullshit
 
Huyu ni janga jingine.

Hapo ndipo ninapomshusha sana JK, unamchukua mtu kama Kigwangala, a great hypocrite unaongoza naye, unategemea huko unakoenda watakuelewa vipi. Sishangai sana maana mara nyingi watu wa namna moja huchaguana kwa sababu ya kufanana kwao, huenda na Rais wetu ni wa namna hiyo hiyo. Taifa linaonekana kama kama ni nchi isiyo na watu wenye upeo na uwezo maana tunawakilishwa na watu wa ajabu kama akina Kigwangala kwenye mikutano ya kimataifa.

Viongozi watakaokuja baada ya 2015 watakuwa na kazi kubwa ya kuihakikishia Dunia kuwa Tanzania ina watu wenye akili nzuri na walio makini.

Hamisi Kigwangalla

Nipo hapa jijini Yokohama, Japan. Nipo kwenye msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete kwenye mkutano mkubwa na maarufu duniani kuhusu Afrika unaojulikana kama TICAD V (Tokyo International Conference on African development). Kwa dakika chache jana Mhe. Rais Jakaya Kikwete aliniachia kiti chake, nikaa kwenye round table na marais wengine zaidi ya 50 wa nchi za Afrika! Can you imagine that? Kulia kwangu alikuwa Mhe. Michael Satta (Rais wa Zambia - a very charming fella!) na kushoto kwangu alikaa Mhe. Yoweri Museveni (Rais wa Uganda).

Leo tena nimepata fursa ya kuingia kwenye kikao kimoja na Mhe. Rais Jakaya Kikwete na humo tulikuwa kwenye bilateral meeting na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Mhe. Ban-Ki Moon. Pia nimepata fursa ya kujadili mambo kwenye vikao na Marais Jacob Zuma (South Africa), Ali Bongo Ondimba (Gabone); Rais wa World Bank, Dr. Jim Yong Kim; Rais wa Benki ya Afrika, Dr. Donald Kaberuka; Rais wa JICA, Dr. Akihiko Tanaka etc. Ziara hii imenifundisha mambo mengi ambayo sintoyasahau katika maisha yangu.

Nimepata pia fursa ya kumuelewa vizuri zaidi Rais wetu na namna anavyoielewa dunia, kukubalika kwake kimataifa, nafasi yake kati ya viongozi mashuhuri duniani na nafasi yetu kama Taifa katika dunia. Hongera Rais wetu Jakaya Kikwete, umenifanya nijisikie 'so proud to have you as our president, and to be a Tanzanian in a global world!' Ziara hii kwenye mkutano huu mkubwa wa kimataifa hapa Japan imenipanua zaidi uelewa wangu kuhusiana na diplomasia ya kimataifa na namna changamoto zinazotukabili sote kama raia wamoja wa dunia moja na namna zinavyopatiwa ufumbuzi wa pamoja, kwa namna ya umoja wetu kama binadamu.


MWISHO WA KUNUKUU. source ukurasa wa facebook kwenye wall ya kigwangala
 
Ungetupia kapicha basi maana nyie hamueleweki,zaidi ni ulimbukeni tuu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kikwete anakubalika bana! Kilicho baki ni chuki binafs tu.

Ni hatari sana rais wa nchi ya dunia ya tatu kukubalika na wakubwa. Mara nyingi huwa ni pale anapotumikia maslahi yao.
 
Back
Top Bottom