ze kokuyo
JF-Expert Member
- Jan 24, 2014
- 7,418
- 9,599
Hamas wamevurumisha Mvua ya maroketi kwenda Israel huku waisrael watatu wakijeruhiwa kutokana na Shambulio Hilo la zaidi ya Maroketi 90.
Mtambo wa kujilinda wa Iron dome ulitungua Maroketi 30 huku mengine 73 yakianguka sehemu za wazi. Waisrael watatu wamejeruhiwa baada ya rocket moja kuangukia kwenye Nyumba yao.
Jeshi la Israel lilijibu Shambulio kwa kufanya mashambulizi ya Anga kwa kushambulia maeneo zaidi ya 40 ya Hamas na kusababisha vifo wa wapalestina wawili huku wengine 12 wakijeruhiwa.
- The Washington Post
UPDATES:
Jeshi la Israel hii leo limeondoa vizuizi vyake katika eneo la mpaka wa Gaza, likiashiria kuwa limekubali mpango uliosimamiwa na Misri wa kusitisha mapigano makali yaliyodumu masaa 24 pamoja na wanamgambo wa Hamas, mapigano yaliyotishia kugeuka vita kamili.
Jeshi lililifunga eneo maarufu la ufukwe na kuzuwia watu wasikusanyike kwa wingi huku wakaazi wengi wakibakia karibu na nyumba zao jana kutokana na maroketi kadhaa yaliyofyatuliwa kutokea Gaza
Lakini baada ya saa kadhaa za utulivu, jeshi la Israel limesema kambi za mapumziko ya msimu wa joto zitaanza kuhudumu kama kawaida na wakaazi wanaweza kuendelea na shughuli zao za kawaida
Mtambo wa kujilinda wa Iron dome ulitungua Maroketi 30 huku mengine 73 yakianguka sehemu za wazi. Waisrael watatu wamejeruhiwa baada ya rocket moja kuangukia kwenye Nyumba yao.
Jeshi la Israel lilijibu Shambulio kwa kufanya mashambulizi ya Anga kwa kushambulia maeneo zaidi ya 40 ya Hamas na kusababisha vifo wa wapalestina wawili huku wengine 12 wakijeruhiwa.
- The Washington Post
UPDATES:
Jeshi la Israel hii leo limeondoa vizuizi vyake katika eneo la mpaka wa Gaza, likiashiria kuwa limekubali mpango uliosimamiwa na Misri wa kusitisha mapigano makali yaliyodumu masaa 24 pamoja na wanamgambo wa Hamas, mapigano yaliyotishia kugeuka vita kamili.
Jeshi lililifunga eneo maarufu la ufukwe na kuzuwia watu wasikusanyike kwa wingi huku wakaazi wengi wakibakia karibu na nyumba zao jana kutokana na maroketi kadhaa yaliyofyatuliwa kutokea Gaza
Lakini baada ya saa kadhaa za utulivu, jeshi la Israel limesema kambi za mapumziko ya msimu wa joto zitaanza kuhudumu kama kawaida na wakaazi wanaweza kuendelea na shughuli zao za kawaida